FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,883
- 109,212
Vijana kuweni makini na poleni sana kwa mihangaiko. Yaani hawa matapeli, mtu anatafuta kazi hajui ataipata lini, wao wanataka kumtapeli, akatowe wapi hizo pesa jamani nae anatafuta kazi? si ataenda kukopa kwa nia njema kabisa, sasa akishatapeliwa huko alikokopa ataonekana yeye ndio tapeli na hatokuwa na pahala pa msaada tena.
Halafu, naomba vijana wakiwatokea tena watu kama hawa, muwawekee mitego ya kuwakamatisha, kubalini tu kuwa mkutane wapi muwapelekee pesa za polisi. Hawafai kabisa hawa watu.
Nawaonea huruma sana vijana. Poleni sana na msikate tamaa na Mwenyeezi Mungu atawapa kazi za halali na zenye heri kwenu na familia zenu. msirudishwe nyuma na hawa majambazi iwe ndio kichocheo cha kuwafanya mfanye bidii zaidi.
Halafu, naomba vijana wakiwatokea tena watu kama hawa, muwawekee mitego ya kuwakamatisha, kubalini tu kuwa mkutane wapi muwapelekee pesa za polisi. Hawafai kabisa hawa watu.
Nawaonea huruma sana vijana. Poleni sana na msikate tamaa na Mwenyeezi Mungu atawapa kazi za halali na zenye heri kwenu na familia zenu. msirudishwe nyuma na hawa majambazi iwe ndio kichocheo cha kuwafanya mfanye bidii zaidi.