Mabagala
JF-Expert Member
- Nov 27, 2009
- 1,477
- 325
Ni juzi tu nimepigiwa simu na jamaa mmoja ambaye tulivyozidi kuongea na kumsikiliza vizuri sikutaka hata kukumbuka jina lake. Habari ilianza hivi; kanipigia simu akasema ameona namba yangu ya simu sehemu kuwa natafuta kazi, akasema wao wana NGO ya watu wa canada wanadeal na nyumba za watoto yatima, hivyo wanahitaji mtu mwenye ujuzi na elimu kama yangu. Mwisho kabisa anasema atanipa fomu mbili ambazo nitatakiwa kulipa 50,000 ili nipewe hiyo ajira!. Sielewi huu utaratibu na ndio maana sijarudi kwake tena wala sijamtafuta kama nilivyomuahidi kumtafuta baadae. Naomba niwaulize wakongwe katika haya mambo je hizi zimo au ndio kuibiana? maana bora hata angekuwa recruitment agent labda angesema ni utaratibu wao. Anyway kiufupi sijamfatilia tena.
Naombeni mawazo yenu tafadhali
Naombeni mawazo yenu tafadhali