Ili haki iwe imetendeka, Mahakama ziwe zinafuatilia utekelezaji wa hukumu zake kwani kuna taasisi zinagoma kutekeleza

Mzee wa Twitter

JF-Expert Member
Nov 5, 2023
1,283
2,043
Wadau nawasabahi. Naomba niingie kwenye madam moja kwa moja. Hoja yangu ni juu ya utekelezaji wa hukumu za mahakama. Kumekuwa na utaratibu wa kupuuza utekelezaji wa hukumu zilizotolewa na mahakama zetu kwa baadhi ya taasisi mashirika na halmashauri zetu.

Kitendo hicho kimekuwa kero kubwa kwa walioshinda kesi na kupata usumbufu mkubwa kudai utekelezaji wa hukumu zao mpaka inafikia hatua ya mhusika kukata tamaa licha ya ushindi aliopewa na mahakama.

Taasisi na halmashauri mbalimbali zimekuwa kwa makusudi kabisa hazitaki kutekeleza hukumu za mahakama.

Ushauri: mahakama zetu ziwe na kitengo maalum kitakachokuwa kinafuatilia hukumu zake kwa kupewa taarifa ya utekelezaji na mhusika au taasisi au halmashauri iliyotakiwa kutekeleza hukumu hizo.Kufanya hivyo kutazifanya hizo taasisi na halmashauri kutekeleza kwa wakati hukumu hizo kwa wakati na kuwaondolea wananchi kero na usumbufu waliokuwa wanaupata.

Ikumbukwe kuwa uamuzi wa mahakama ni wa mwisho kama kuna mtu taasisi au halmashauri inaupinga basi ifungue kesi mahakamani badala ya kuwasumbua wananchi kwa kutokutekeleza hukumu.

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Kwa katiba hii ambayo rais hashitakiwi akiwa madarakani au akiwa ametoka, usitegemee kuwa na taasisi imara. Mahakama ni baadhi ya muhumili uliodhoofishwa na madaraka ya rais yaliyo juu ya katiba. Kwa Sasa muhimili wa serekali unatekeleza wajibu wake kulingana na utashi wa rais aliye madarakani. Idara yoyote ya serekali inahisi ni udhaifu kutii amri ya mahakama. Hivyo serekeli inatekeleza amri ya mahakama kwa jinsi inavyotaka.
 
Kwa katiba hii ambayo rais hashitakiwi akiwa madarakani au akiwa ametoka, usitegemee kuwa na taasisi imara. Mahakama ni baadhi ya muhumili uliodhoofishwa na madaraka ya rais yaliyo juu ya katiba. Kwa Sasa muhimili wa serekali unatekeleza wajibu wake kulingana na utashi wa rais aliye madarakani. Idara yoyote ya serekali inahisi ni udhaifu kutii amri ya mahakama. Hivyo serekeli inatekeleza amri ya mahakama kwa jinsi inavyotaka.
Sahivi tunaishi kwa hisani ya Rais asee
 
Back
Top Bottom