DOKEZO IGP Wambura tunaomba ingilia Kati hili linaloendelea kwenye hiki Kituo cha Polisi Tabata Relini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Rushwa na Polisi ni jambo la kawaida sana hasa Trafik wapo tayari kwa lolote mradi wachukue Rushwa. Juzi nilikamatwa pale Salenda na Trafik mmoja mwanamama kala mkorogo wa haja, nikaongea nae vizuri sana gari halikuwa na tatizo kbs lakini cha ajabu akalazimisha kosa. IGP Wambura ni lazima atengeneze mfumo wa kukamata hawa Trafik wala rushwa. Kimara stopova ukipita tu taa wapo mtu unajiuliza wanafanya nini? Hawa wa hapa Ova ni walarushwa hatari.
Yye mwenyewe ni mchafu unafikili atawakamata wachafu wenzake? Hawezi na hatoweza
 
Tuma timu yako kwa namna inayofaa leo tarehe 01.10.2023 wakajiridhishe namna Trafic wanavyokomoa Madereva hasa wa Bajaji katika eneo hilo.

Leo nimepita Mandela Road Dar es Salaam nimeona operesheni kali madereva wa Gari wanakamatwa na wengine watu wazima wanafokewa na kujibiwa vibaya kwa kiburi, Dharau na udhalilishaji kama watoto wadogo katika kituo cha Polisi Tabata Relini, usimamizi wa sheria umegeuka Vita pale.

Makosa yenyewe nimeyaangalia mengi yanahitaji Elimu tu lakini watu wanakomolewa wanaandikiwa tu notification kama watu wametumwa kufikia Target flani ya Makusanyo bila kuangalia chochote.

Upokeaji wa Rushwa eneo lile ni wa kiwango cha kutisha,Trafic anaongea waziwazi kwa Dereva kwamba chini ya Elfu 10 hapokei hata kabla Dereva hajamwambia habari za Rushwa hii ni hatari.

Kuna Trafic mmoja mwanamke namba zake zina 88 mbili mkononi kavaa Smart Watch na Bracelet ni hatari kwa Rushwa,kukomoa na Majibu ya hovyo kwa Madereva, anafanya kazi kwa vitisho na vurugu kama mtu ambaye ameshatumia kilevi au kisaikolojia ana matatizo makubwa.

Naona huyu Dada anatumia sana Sticker ya Nenda kwa Usalama kama kosa kubwa sana,kwanini Polisi wasiweke Sheria vizuri kama hilo ni kosa kubwa kiasi hicho zikapatikana palepale kituoni gari ikakaguliwa hapohapo mtu akalipia akapewa badala ya kutumia Rungu la Faini tu kwa kila kitu,rungu la Elimu na Uhamasishaji liko wapi?

Ieleweke hali ya Maisha ni ngumu kumlipisha Dereva wa Bajaji Faini makosa mawili au matatu kwa pamoja asubuhiasubuhi ambayo ukiyaangalia ni makosa ambayo yanahitaji tu Elimu, tukumbuke kumfanyia hivyo umefanya siku nzima afanye kazi bure umemuumiza yeye umeumiza hadi Familia yake ,hii siyo nzuri inazidisha sana Chuki ya Raia kwa Jeshi la Polisi.

Kwa nia njema IGP liangalie hili.
Sasa Faini ya Bajaji ni Elfu kumi, halafu uombwe tena rushwa ya elfu kumi.Wewe sema wamekuandikia tu hao.
Madereva waende Driving School,ili wasijifiche kwenye kichaka cha kupewa elimu. Kama mtu umekosea pigwa Faini au uende Mahakamani tu.

Njooni Shambani tulime huku hakuna traffic kusimamisha jembe wala shamba lako
 
Naona huyu Dada anatumia sana Sticker ya Nenda kwa Usalama kama kosa kubwa sana,kwanini Polisi wasiweke Sheria vizuri kama hilo ni kosa kubwa kiasi hicho zikapatikana palepale kituoni gari ikakaguliwa hapohapo mtu akalipia akapewa badala ya kutumia Rungu la Faini tu kwa kila kitu,rungu la Elimu na Uhamasishaji liko wapi?
Habari ya stika ni kero sana hivi sasa, stika zinafichwa ili ziuzwe kwa bei juu na wahuni
 
Sasa Faini ya Bajaji ni Elfu kumi, halafu uombwe tena rushwa ya elfu kumi.Wewe sema wamekuandikia tu hao.
Madereva waende Driving School,ili wasijifiche kwenye kichaka cha kupewa elimu. Kama mtu umekosea pigwa Faini au uende Mahakamani tu.

Njooni Shambani tulime huku hakuna traffic kusimamisha jembe wala shamba lako
Wapi nimesema Faini alipiga Bajaji pekee,Wewe Ziwa Jipe ni mmojawao au mfanya hayo mambo sehemu nyingine ndiyo maana unakuja mbio kuropoka kwa akili za tumbo bila kusoma mada kwa makini na kuelewa.
 
Tuma timu yako kwa namna inayofaa leo tarehe 01.10.2023 wakajiridhishe namna Trafic wanavyokomoa Madereva hasa wa Bajaji katika eneo hilo.

Leo nimepita Mandela Road Dar es Salaam nimeona operesheni kali madereva wa Gari wanakamatwa na wengine watu wazima wanafokewa na kujibiwa vibaya kwa kiburi, Dharau na udhalilishaji kama watoto wadogo katika kituo cha Polisi Tabata Relini, usimamizi wa sheria umegeuka Vita pale.

Makosa yenyewe nimeyaangalia mengi yanahitaji Elimu tu lakini watu wanakomolewa wanaandikiwa tu notification kama watu wametumwa kufikia Target flani ya Makusanyo bila kuangalia chochote.

Upokeaji wa Rushwa eneo lile ni wa kiwango cha kutisha,Trafic anaongea waziwazi kwa Dereva kwamba chini ya Elfu 10 hapokei hata kabla Dereva hajamwambia habari za Rushwa hii ni hatari.

Kuna Trafic mmoja mwanamke namba zake zina 88 mbili mkononi kavaa Smart Watch na Bracelet ni hatari kwa Rushwa,kukomoa na Majibu ya hovyo kwa Madereva, anafanya kazi kwa vitisho na vurugu kama mtu ambaye ameshatumia kilevi au kisaikolojia ana matatizo makubwa.

Naona huyu Dada anatumia sana Sticker ya Nenda kwa Usalama kama kosa kubwa sana,kwanini Polisi wasiweke Sheria vizuri kama hilo ni kosa kubwa kiasi hicho zikapatikana palepale kituoni gari ikakaguliwa hapohapo mtu akalipia akapewa badala ya kutumia Rungu la Faini tu kwa kila kitu,rungu la Elimu na Uhamasishaji liko wapi?

Ieleweke hali ya Maisha ni ngumu kumlipisha Dereva wa Bajaji Faini makosa mawili au matatu kwa pamoja asubuhiasubuhi ambayo ukiyaangalia ni makosa ambayo yanahitaji tu Elimu, tukumbuke kumfanyia hivyo umefanya siku nzima afanye kazi bure umemuumiza yeye umeumiza hadi Familia yake ,hii siyo nzuri inazidisha sana Chuki ya Raia kwa Jeshi la Polisi.

Kwa nia njema IGP liangalie hili.
Kwa trafiki mbona ndo tabia yao.kila mkoa hali iko hivyo.Ni mwamba JPM tu ndiye aliyewapunguza makali lkn kwa sasa mambo yamerudi kule kule.trafiki alisimamisha gari yoyote dereva anasimama mbali kidogo na hawa jamaa halafu anateremka kuwafuata na kuwapa kitu kidogo na safari inaendelea.siku moja nilimwuliza dereva kwa nini unasimamisha gari mbali halafu unawafuata na kwa nn asije yeye hapa? akacheka na kusema nchi hii ni ngumu sana.
 
Tuma timu yako kwa namna inayofaa leo tarehe 01.10.2023 wakajiridhishe namna Trafic wanavyokomoa Madereva hasa wa Bajaji katika eneo hilo.

Leo nimepita Mandela Road Dar es Salaam nimeona operesheni kali madereva wa Gari wanakamatwa na wengine watu wazima wanafokewa na kujibiwa vibaya kwa kiburi, Dharau na udhalilishaji kama watoto wadogo katika kituo cha Polisi Tabata Relini, usimamizi wa sheria umegeuka Vita pale.

Makosa yenyewe nimeyaangalia mengi yanahitaji Elimu tu lakini watu wanakomolewa wanaandikiwa tu notification kama watu wametumwa kufikia Target flani ya Makusanyo bila kuangalia chochote.

Upokeaji wa Rushwa eneo lile ni wa kiwango cha kutisha,Trafic anaongea waziwazi kwa Dereva kwamba chini ya Elfu 10 hapokei hata kabla Dereva hajamwambia habari za Rushwa hii ni hatari.

Kuna Trafic mmoja mwanamke namba zake zina 88 mbili mkononi kavaa Smart Watch na Bracelet ni hatari kwa Rushwa,kukomoa na Majibu ya hovyo kwa Madereva, anafanya kazi kwa vitisho na vurugu kama mtu ambaye ameshatumia kilevi au kisaikolojia ana matatizo makubwa.

Naona huyu Dada anatumia sana Sticker ya Nenda kwa Usalama kama kosa kubwa sana,kwanini Polisi wasiweke Sheria vizuri kama hilo ni kosa kubwa kiasi hicho zikapatikana palepale kituoni gari ikakaguliwa hapohapo mtu akalipia akapewa badala ya kutumia Rungu la Faini tu kwa kila kitu,rungu la Elimu na Uhamasishaji liko wapi?

Ieleweke hali ya Maisha ni ngumu kumlipisha Dereva wa Bajaji Faini makosa mawili au matatu kwa pamoja asubuhiasubuhi ambayo ukiyaangalia ni makosa ambayo yanahitaji tu Elimu, tukumbuke kumfanyia hivyo umefanya siku nzima afanye kazi bure umemuumiza yeye umeumiza hadi Familia yake ,hii siyo nzuri inazidisha sana Chuki ya Raia kwa Jeshi la Polisi.

Kwa nia njema IGP liangalie hili.
Polisi ni majambazi waliovaa sare za serikali ni aibu sana tena sana wandugu police wetu wana njaa mno mno
 
Back
Top Bottom