masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Tumeona matukio ya kusikitisha tokea mikutano ya CDM ilivyoanza kuanzia Morogoro na hata Iringa
Serikali imetumia nguvu kubwa pasipo ulazima wowote bila kujali kuwa wanao umia ni Watanzania walipa kodi, wawe CHADEMA au vinginevyo.
Amani tuliyozoea kuiimba kila siku haivunjwi na wananchi bali vyombo vya dola-kiashirio ambacho si kizuri kwa mustakabali wa nchi yetu.
Mimi ni mwana CCM lakini kile ninachoona hakinipi faraja yoyote kama kuna utawala bora.Serikali nahisi imeingia kichwa kichwa katika mtego wa CDM na sidhani kama watatoka bila mikono ya baadhi ya viongozi kulowa damu.
Ningependa kumwomba Kamanda IGP kwamba muendelezo wa kutumia maguvu bila akili sana sasa unapitiliza kuliko kiasi.
Ni kwa nia hii hii njema ningemwomba ASITUMIE staili hii huko Mbeya maana vijana wa pale Mwanjelwa hawabipiki.
Ukiwabipu watapiga kweli.
Hatujasahau zile fujo za siku tatu nzima, ambazo zilizimwa na kauli tu ya Mhe Sugu.
Sote tunapenda amani, lakini kwa mtindo huu wa Polisi amani nahisi haitachukua muda mrefu kusambaratika.
Serikali imetumia nguvu kubwa pasipo ulazima wowote bila kujali kuwa wanao umia ni Watanzania walipa kodi, wawe CHADEMA au vinginevyo.
Amani tuliyozoea kuiimba kila siku haivunjwi na wananchi bali vyombo vya dola-kiashirio ambacho si kizuri kwa mustakabali wa nchi yetu.
Mimi ni mwana CCM lakini kile ninachoona hakinipi faraja yoyote kama kuna utawala bora.Serikali nahisi imeingia kichwa kichwa katika mtego wa CDM na sidhani kama watatoka bila mikono ya baadhi ya viongozi kulowa damu.
Ningependa kumwomba Kamanda IGP kwamba muendelezo wa kutumia maguvu bila akili sana sasa unapitiliza kuliko kiasi.
Ni kwa nia hii hii njema ningemwomba ASITUMIE staili hii huko Mbeya maana vijana wa pale Mwanjelwa hawabipiki.
Ukiwabipu watapiga kweli.
Hatujasahau zile fujo za siku tatu nzima, ambazo zilizimwa na kauli tu ya Mhe Sugu.
Sote tunapenda amani, lakini kwa mtindo huu wa Polisi amani nahisi haitachukua muda mrefu kusambaratika.