Idara ya Usalama wa Taifa yakanusha tuhuma

Status
Not open for further replies.
Times change...wakati wa sasa kazi za kijasusi zinadai watu wenye uwezo na upeo mkubwa sana wa kuzifanya na kuiletea nchi yoyote heshima.

Mkiweka watu wajinga wajinga kila siku mtaishia kupata kashfa tu. Hii idara inaajiri watu wa aina gani siku hizi? kama hawa mapoyoyo tunao waona mitaani ndio wamejaa kila sehemu mbona kazi ipo. Mtaandika haya matangazo mpaka mchanganyikiwe
 
USA kila siku President anakuwa briefed na CIA, je na Bongo ni hivyo? Kama ndio, je sehemu kubwa ya utekelezaji wa TISS ni mwongozo wa Rais?
KWANI RAIS WENU ANA MDA WA KUWA BRIEFED? ye daily kuzurula na bata tuu....mtajicheki wenyewe...Riz maisha safi,Miraj naye bos mtaani....mama anasubir pension ya Ualim....yaan KAMA MAMTONI
 
Nakubaliana na wewe mkuu....Hivi siku hizi watu walio kwenye idara wana uwezo kiasi gani wa kufanya kazi ndani ya idara hiyo? Kila siku kuna jipya Tanzania...wizi wa mali ya umma, utoroshaji wa nyara za serikali, usafirishaji haramu wa binadamu, na hata Iran kutumia bendera ya Tanzania kwenye meli zake si kitu kidogo.Halafu wanafikiri kwa kutoa matangazo kama haya watu watawaamini kuwa ni wakweli....toka lini????
Kitendo cha Ramadhan kujitambulisha kwa Dr Uli kama Abeid huku akiwasilliana na Dr kwa namba ya simu iliyosajiliwa kwa jina lake halisi ni ushahidi tossha kuwa huyu hana sifa wala ujuzi wa kuwa kwenye idara hiyo.
 
Mi wangeniambia kama yule jamaa aliyetajwa na Mwanahalis, yule anayeitwa Rama kama sio mfanyakazi wao ningewaelewa, lakini hizi taarifa za jumla jumla, aaah ni rahisi kuwapuuza wao na sio Mwanahalisi, hata ukataaji wenyewe, ile taarifa ya Mwanahalisi ni nzito sana, kama ingekuwa ni uongo, sahizi tungekuwa tunasema lugha nyingine, may be wangekuwa hata mahakamani sahizi, kimya chao kinatufanya tuwaone Mwanahalisi ni wakweli 100% also also reputations yao Mwanahalisi inawabeba!
 
Sijakuelewa hapa mkuu, ina maana TISS wanatuhumiwa kwa vile hawajasema nani kahusika? Kwa uelewa wangu najua mwenye Mamlaka ya kutoa tamko nani kahusika ni Jeshi la Polisi.

Jeshi la polisi na hao TISS ni watoto wa Baba Mmoja kama wangekuwa makini wangeshapeleka taarifa za watekaji hao...lakini wao na KOVA wote ni dhaifu
 
HEBU TOENI HUU UCHAFU...HII SIO FORUM YA WATOTO WADOGO....elezeni yakwenu ili tukipima na ya kwenye vyombo vya habari tuamini uzushi....

Nakuunga mkono Mkuu, ingekuwa vizuri kama Idara hii ingekuwa inasema imefikia wapi katika kumtafuta aliyehusika katika kuhatarisha usalama wa Taifa kwa kumteka Daktari huyo kwa lengo la kuchochea hasira za wananchi dhidi ya Serikali yao.
 
...wanajishuku nini kama wanahisi hawahusiki? pumba tu!
Yakanusha kuwa haikupanga kumuua Dr. Ulimboka na kwamba kinachotangazwa na vyombo vya habari ni vipande vya taarifa visivyo na ukweli wowote na wananchi wapuuze.
 
Mimi kama mwananchi mtanzania ambaye nilifaulu darasa la saba nikiwa najua kusoma na kuandika. Kukanusha kwao hakubadilishi ukweli ulioandikwa na mwanahalisi kwani ndiyo UKWELI wenyewe na unaendana na tukio.

Lakini uchunguzi wao kipolisi uliomkamata mkenya, unajitenga mbali sana na tukio lilivyokuwa na mtirirko wake. Itakuwa ngumu sana kwangu kukubali utetezi wao ambao hata hawamanishi chochote kwetu wananchi ila wanajikosha kwa kuona aibu kwani hawajajua kuchunguza, wanachunguza amabacho hakihusiani na Ulimboka kwani uchunguzi wao wanaacha kuanza na mawasiliano ya mwisho na ulimboka kwenye simu ila wameamua kuhamia kenya, na kuwaacha watanzania walohusika na ndo maana naamini kwamba ni usalama wa taifa waliohusika na hii ni kwa sababu mnajua mlichokifanya kwa hiyo manjiogopa kujichunguza, na nashangaa kwani hamkujua mtajulikana mlivyokwenda pupa pupa, mnafikiri wananchi wote tulifaulu darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika?

Jipangeni upya tena hapo mmechemsha na lazima mlinywe.
 
TISS na POLICE ni kichaka cha uovu wa ccm na serikali.zinatakiwa zifumuliwe zote na zianze upya.
 
Hawakupanga kumuua bali kumtesa ili awatajie aliye nyuma ya mgomo!


Naamini walichotaka kufanya kilikuwa kuleta hofu na kupunguza kujiamini kwa wanaharakati. Wangetaka kumuua Ulimboka wangemuua tu. Na kwa mtizamo fulani lengo limefanikiwa. Kinachofanyika sasa kwa hili tamko ni damage control.
 
Tangu lini hawa wamekuwa wakifanya kazi kwa weledi? Wangekuwa wanafanya kazi kwa weledi basi wangemshukia Pinda pale alipotoa kauli kwamba "Wezi wa EPA ni matajiri wakubwa nchini kama wakikamatwa basi nchi itawaka moto." pia wangekuwa makini kuhakikisha ndege ya kigeni haingii nchini usiku usiku kuiba wanyama katika mbuga za Taifa tena bila ya kibali cha kutua nchini...Hawana hata sifa moja ya kustahili kuitwa usalama wa Taifa.

Ni wa kuwapuuza, hawana maana kama TAKUKURU ! wamebakia majina tuu !
 
Upuuzi mtupu huu, yaani hamjui hata jinsi ya kujisafisha! Kama mmeweza kutumia taaluma yenu ya uchunguzi mkachunguza na kugundua kwamba tuhuma hizo si za kweli kwa haraka namna hiyo, mnashindwaje kuchunguza kwa speed hiyohiyo na kuwataja walohusika. Au mnakanusha bila kutafiti nini? Hamna mahali pa kutokea. Mmetajwa kuhusika kwa kuwekewa vielelezo vilivyo wazi kabisa. kukanusha mnatakiwa kutolea maelezo kielelezo kimoja baada ya kingine na sio majibu ya jumla namna hiyo
 
sayansi na teknologia imewaumbua yaani imewaulimbuka. wangekua wa janja wangeipiga mawe minara yote ya mitandao baada ya tukio.
 
daima cwezi acha kuamini usalama wa taifa hawahusiki mwanahalisi endelea kutujuza zaidi maovu ya hawa wauwaji
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom