- Thread starter
- #21
Sasa kama "inner conscious" yako inakukataza kuwatetea mtu kama Chavda na Chenge, mbona umenikumbusha kuwa kila mtu hana hatia mpaka ithibitishwe vingine? Hicho kitu umekisema ili iweje, umejitamkia tamkia tu?
"Tumepewa wito," tumepewa na nani? "Kiufasaa" maana yake nini, umesikia wapi hicho kitu "kiufasaa," mtaani? Umeweka maneno "nafsi zetu" ndani ya nukuu, ni maneno ya nani hayo, kwa nini yako kwenye nukuu?
Utajivuniaje Legum Magister hata kuwasiliana Kiswahili unapata tabu? Utawakilisha kina nani wewe, Wanyasa? Ndio nyinyi mnategemewa kumudu cha kigeni kujadili mikataba ya kukodisha ardhi ya nchi kwa Wairan, Wasaudi?
Mkuu Dilunga, asante kwa maoni yako mkuu. Kwani kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake kwa jinsi apendavyo. Nakubaliana kutokukubaliana na wewe 'mwalimu wa walimu'.
Mkuu Dilunga, mwisho usinifanye nianze kuamini kwamba: "the only tool you have is a hammer and you tend to see every problem as a nail".
Wakatabahu,
Shadow