Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Gazeti na Jarida la Raia mwema la Jumatano wiki hii lilikuwa na Makala yenye kichwa sawia ikiwa imeandikwa na gwiji la Habari Mabala wa Mabalaa. Makala hiyo iliyoandikwa kwa mtindo wa tenzi au aya za Ayah za Binti Hidaya inazungumzia Utawala huu Awamu ya 5.
Mwandshi kaongea ukweli kwamba Utawala huu umepoteza mwelekeo kwenye swala la Sheria na Katiba ya nchi. Baba wa Taifa aliwahi kusema tunapochagua Rais lazima tumwapishe kwa Katiba ya JMT na lazima aape KUILINDA NA KUITETEA KATIBA YA NCHI kama ni Mkristu ataapa kwa kushika BIBLIA, kama Mwislamu ataapa kwa kushika Quruan na kama ni Mpagani lazima tutatafuta namna ya kumwapisha...!!
Rais Magufuli ni Mkristu na aliapa kuilinda na kuitetea Katiba ya Tanzania, lakini jamaa baada ya kuingia Ikulu anafanya kinyume cha Katiba...! Tumeshuhudia Rais huyu akisigina Katiba yetu kwa jeuri na ubabe unaopitiliza kiasi cha baadhi ya Watanzania kuanza kumwita ni Dikteta uchwara. Tujikumbushe machache ambayo mpaka sasa ameyafanya kwa kuvunja Katiba yetu:
Mwandshi kaongea ukweli kwamba Utawala huu umepoteza mwelekeo kwenye swala la Sheria na Katiba ya nchi. Baba wa Taifa aliwahi kusema tunapochagua Rais lazima tumwapishe kwa Katiba ya JMT na lazima aape KUILINDA NA KUITETEA KATIBA YA NCHI kama ni Mkristu ataapa kwa kushika BIBLIA, kama Mwislamu ataapa kwa kushika Quruan na kama ni Mpagani lazima tutatafuta namna ya kumwapisha...!!
Rais Magufuli ni Mkristu na aliapa kuilinda na kuitetea Katiba ya Tanzania, lakini jamaa baada ya kuingia Ikulu anafanya kinyume cha Katiba...! Tumeshuhudia Rais huyu akisigina Katiba yetu kwa jeuri na ubabe unaopitiliza kiasi cha baadhi ya Watanzania kuanza kumwita ni Dikteta uchwara. Tujikumbushe machache ambayo mpaka sasa ameyafanya kwa kuvunja Katiba yetu:
- Kupiga marufuku mikutano na Maandamano ya vyama vya siasa ambayo iko kikatiba na kisheria.
- Kuwakamata Wabunge na Viongozi wa Upinzani na kuwaweka ndani kwa masaa zaidi ya 48 wengine mpaka wiki na miesi kadhaa pasi na kuwafungulia mashtaka.
- Kuwanyima dhamana Washtakiwa hasa wapinzani kitu ambacho ni Haki yao Kikatiba.
- Kubomoa nyumba za Wananchi hata pale ambapo Mahakama imeweka zuio(Court Injuction).
- Kuvunja Mikataba ya Wawekezaji pasi na kujali au kuheshimu Mikataba ya Kimataifa kati ya Wawekezaji na Serikali ambayo iko kisheria.
- Kuingilia mihimili mingine kama Bunge, Uhuru wa Mahakama na Media kwa kutoa maelekezo ili kulazimisha mambo yawe anavotaka yeye.
- Kubadilisha Matumizi na Bajeti ya Serikali kwa kuelekeza Fedha fulani iende kununua au kujenga kitu au jambo ambalo halikupitishwa kwenye Bajeti ya Bunge.
- Watu na Media kunyimwa Uhuru wa kutoa maoni yao kwa kisingizio cha Uchoghezi ilhali Katiba inaruhusu watu au raia kuwa na Uhuru wa kutoa maoni na mawazo yao....!
- Kufukuza Wafanyakazi waliofanya kazi kwa miongo kadhaa na kuwanyima malipo yao kwa madai ya kutokuwa na vyeti au kughushi vyeti vya F4 na F6 na sasa STD 7 huku wateule wake akiwakingia kifua....!
- +++++!