TUKANA UONE
JF-Expert Member
- Jan 3, 2018
- 1,816
- 5,151
Ukihitaji salamu njoo unikatie mauno kwanza kama Yondo, tofauti na hapo utaambulia chuya!
Huu utaratibu ulianza kama mzaha lakini kadiri siku zinavyozidi ndivyo hali inakuwa mbaya,kitu kibaya zaidi hadi wanaume watu wazima utawakuta nao wamejifunga kibwebwe wanakata mauno bila aibu wala soni!.
Viongozi wetu wakienda nchi za watu walioendelea huwezi kuona huu uwendawazimu wa kina mama na kina baba wa huko kukata mauno kama wendawazimu!.
Zamani viongozi walipokuwa wakija hapa nchini kulikuwa na vikundi vya ngoma za asili vilivyocheza kwa staha,madoido na mbwembwe bila kukata mauno ovyo!, Sijajua siku hizi hivi vikundi vimepatwa na nini maana siyo kwa miuno hiyo inayokatwa!.
Kuna mtu nilikuwa najadiliana nae akaniambia kwamba huo ndiyo utamaduni wetu na wageni wanapokuja wanapaswa wakatiwe viuno ili wafurahie utamaduni wa mtanzania!.
Kama ndivyo aisee hii ni hatari sana!.
Nimeshangaa sana kuona mijibaba yenye ndevu ikiwa inakata mauno mbele ya Rais wa Germany!,Rais kazi yake ilikuwa ni kupiga makofi tu na kushangaa!, bila shaka nadhani akirudi Germany ataenda kuwasimulia wenzie, hivyo tutegemee ugeni mzito kutoka Germany kuja kushangaa wakata miuno pale JKNIA!
Huu utaratibu ulianza kama mzaha lakini kadiri siku zinavyozidi ndivyo hali inakuwa mbaya,kitu kibaya zaidi hadi wanaume watu wazima utawakuta nao wamejifunga kibwebwe wanakata mauno bila aibu wala soni!.
Viongozi wetu wakienda nchi za watu walioendelea huwezi kuona huu uwendawazimu wa kina mama na kina baba wa huko kukata mauno kama wendawazimu!.
Zamani viongozi walipokuwa wakija hapa nchini kulikuwa na vikundi vya ngoma za asili vilivyocheza kwa staha,madoido na mbwembwe bila kukata mauno ovyo!, Sijajua siku hizi hivi vikundi vimepatwa na nini maana siyo kwa miuno hiyo inayokatwa!.
Kuna mtu nilikuwa najadiliana nae akaniambia kwamba huo ndiyo utamaduni wetu na wageni wanapokuja wanapaswa wakatiwe viuno ili wafurahie utamaduni wa mtanzania!.
Kama ndivyo aisee hii ni hatari sana!.
Nimeshangaa sana kuona mijibaba yenye ndevu ikiwa inakata mauno mbele ya Rais wa Germany!,Rais kazi yake ilikuwa ni kupiga makofi tu na kushangaa!, bila shaka nadhani akirudi Germany ataenda kuwasimulia wenzie, hivyo tutegemee ugeni mzito kutoka Germany kuja kushangaa wakata miuno pale JKNIA!