Huu utaratibu unaopigiwa debe wa kujitolea kwanza ili upewe kipaumbele kwenye kuajiriwa ni unyanyasaji

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,664
18,038
Ukiweka sharti la kujitolea ili mtu apewe ajira maana yake ni kwamba kila mwajiriwa mtarajiwa atataka kujitolea! SWALI: Je waajiriwa wote wanaweza kupata fursa ya kujitolea? Jibu la dhati ni HAPANA. Sasa hivi kuna vijana takriban 600,000 wanasaka ajira. Je tuna uwezo wa kuwapa wote hawa fursa ya kujitolea? Jibu ni hapana. SWALI: Kwa nini umbague mtu kwenye ajira wakati hukuwa na uwezo wa kumpa fursa ya kujitolea? Yawezekana huyu ambaye hakupata fursa ya kujitolea ndio ana uwezo zaidi.

Haya mambo ya kujitolea yatafungua mlango wa upendeleo na rushwa!! Kiongozi wa taasisi fulani atakuwa na uwezo wa kuwapa ndugu zake fursa ya kujitolea na hivyo kuwaandalia mazingira ya kuajiriwa!! Huu utaratibu wa sasa umewabana sana wakubwa, hata kama kuna wanaopenyeza lakini si kama zamani!

Anayejitolea mwache ajitolee lakini atapambanishwa kwenye usaili na wale ambao nao wangependa kujitolea lakini hawakupata fursa hiyo. Uwanja wa kupambania ajira tunaomba ubaki sawa kwa wote. Msiturudishe kwenye "testimonial" ambazo nyingi ni za mchongo!! Unategemea kijana anayetoka kijijini apate fursa ya kufanya kazi BOT kama yataingizwa mambo ya kujitolea? Nani atakayempa mtu nafasi ya kujitolea BOT?

Mameneja wa BOT wataleta watu wao, Wahasibu wa BOT wataleta watu wao, na vimemo vya wakubwa vitapigana kikumbo kupenyeza watu wao, na wote hawa watataka waajiriwe kwa kuwa waqmejitolea hata kama uwezo wao ni mdogo!! HAPANA!! Wakubwa wanapigania mlango wa nyuma wa kupenyezea watu wao!! Si vizuri kuweka kigezo ambacho kuna watu watalazimika kukikosa kwa sababu mazingira yao hayawaruhusu!!

Kuna mwingine japo hana ajira rasmi lakini ana mzigo wa kulea familia! Hufanya vibarua ili wadogo zake wasome!! Sasa huyu ukimtaka ajitolee hataweza. Ila watoto wa matajiri wana uwezo wa kujitolea maana wataendelea kuhudumiwa bila shida. Lakini mtoto wa mlala hoi kwa vyovyote vile hawezi kumudu kujitolea maana kila siku analazimika kutafuta riziki ya kutwa!!
 
Watoto wa matajiri ndio watakaomudu kujitolea maana bado wanatunzwa na wazazi wao!! Watoto wa walalahoi watakuwa wamebaguliwa sana maana hawawezi kumudu kujitolea! Wana mzigo wa kujitegemea na kulea wadogo zao!!
 
Mbunge ndiye ameuliza swali akiitaka serikali ione umuhimu wa kuajiri waliojitolea kwanza!! Bila shaka wote tutakubliana kuwa MTOTO WA MBUNGE huyu anaweza kujitolea bila stress!! Analala bure, anakula bure, anavalishwa bure na anaweza kujitolea hata miaka 5 na baba yake akaendelea kumhudumia.

Lakini je mtoto wa mlala hoi ambaye alikuwa analazimika hata kutumia boom lake kuchangia kusomesha wadogo zake atawezaje kujitolea huku kuna watu wanamtegemea!! Kila siku anafanya biashara ndogondogo ili ajikimu na wadogo zake halafu leo unamtaka ili aajiriwe ajitolee kwanza!! HAPANA!! Uwanja wa kupambania ajira hautakuwa sawa!!
 
Serikali iwe makini sana na jambo hili!! Vinginevyo nafasi za kujitolea zishindaniwe kwa usaili kama ajira zinavyoshindaniwa!! Na sekretarieti ya ajira iwe inatangaza nafasi za kujitolea watu wapigwe written na oral interview!! Watu wote wagombanie!! Ikiwa hivyo sawa!!
 
Watoto wa wakubwa serikalini na watoto wa matajiri ndiyo wenye uwezo wa kujitolea kwa sababu bado watahudumiwa na wazazi wao kama watoto na watajitolea sehemu nono kwa uhakika wa kuajiriwa baadaye. Watajitolea TRA. BOT, NSSF, nk. Watoto wa walala hoi hawawezoi kujitolea maana hulazimika kutafuta riziki ili wajikimu. Hawawezi kujitolea bure! Halafu kuna wabunge wamelivalia njuga suala la kipaumbele kwa wanaojitolea maana wanajua itakuwarahisi kuwapenyeza watoto wao kwenye malisho mazuri!!
 
Utaratibu wa sasa ndio ulio bora, umeweka uwanja sawa kwa wotw. Kama ni ugumu basi huo ugumu ni kwa wote!!! Watanzania tupingane na hili kwa nguvu zote!! Kuna watu wanaweza kupata nyaraka za kujitolea huku hawakuwahi kujitolea!!
 
Halafu watoto wa wakubwa wanapojitolea usifikiri kuwa wanajitolea bure kabisa!! Hupewa "posho". Wewe mwenzangu na mimi ukiwaiga utapelekwa ukajitolee kiukweli na hakuna cha posho wala nini!! Huu utaratibu unaotaka kupachikwa TUUKATAE!!
 
Baadhi ya taasisi zinatoa pesa wanaita ya usafiri ila ni pesa ambayo mtu anaweza kuishi kwa mfano kuna taasisi wanapewa 350k na kuna chai nzito daily sema mchana mnapambania ...

wanachukua kwa mkataba wa mda kama miezi 3 then kuna kuextend taratibu wapo madogo town wanaishi kwa kujitolea huku wakisikilizia kwingind.

Ishu ambayo sijui labda wale wanakuwa na connection au ?
 
Halafu watoto wao si kwamba ni kweli wanajitolea, bali hupewa mikataba mifupi mifupi na posho kibao!! Wewe unataka mwenzako ajitolee, atakula nini wakati anajitolea!!
Watoto wengi wa mawaziri au watu wa serikalini vilaza, kuna waziri mwanawe kapewa cheti wakati shule kafeli tena vibaya tu. Ajira hapa mchongo tu
 
Ukiweka sharti la kujitolea ili mtu apewe ajira maana yake ni kwamba kila mwajiriwa mtarajiwa atataka kujitolea! SWALI: Je waajiriwa wote wanaweza kupata fursa ya lkujitolea? Jibu la dhati ni HAPANA. Sasa hivi kuna vijana takriban 600,000 wanasaka ajira. Je tuna uwezo wa kuwapa wote hawa fuesa ya kujitolea? Jibu ni hapana. SWALI: Kwa nini umbague mtu kwenye ajira wakati hukuwa na uwezo wa kumpa fursa ya kujitolea? Yawezekana huyu ambaye hakupata fursa ya kujitolea ndio ana uwezo zaidi.

Haya mambo ya kujitolea yatafungua mlango wa upendeleo na rushwa!! Kiongozi wa taasisi fulani atakuwa na uwezo wa kuwapa ndugu zake fursa ya kujitolea na hivyo kuwaandalia mazingira ya kuajiriwa!! Huu utaratibu wa sasa umewabana sana wakubwa, hata kama kuna wanaopenyeza lakini si kama zamani!

Anayejitolea mwache ajitolee lakini atapambanishwa kwenye usaili na wale ambao nao wangependa kujitolea lakini hawakupata fursa hiyo. Uwanja wa kupambania ajira tunaomba ubaki sawa kwa wote. Msiturudishe kwenye "testimonial" ambazo nyingi ni za mchongo!! Unategemea kijana anayetoka kijijini apate fursa ya kufanya kazi BOT kama yataingizwa mambo ya kujitolea? Nani atakayempa mtu nafasi ya kujitolea BOT?

Mameneja wa BOT wataleta watu wao, Wahasibu wa BOT wataleta watu wao, na vimemo vya wakubwa vitapigana kikumbo kupenyeza watu wao, na wote hawa watataka waajiriwe kwa kuwa waqmejitolea hata kama uwezo wao ni mdogo!! HAPANA!! Wakubwa wanapigania mlango wa nyuma wa kupenyezea watu wao!! Si vizuri kuweka kigezo ambacho kuna watu watalazimika kukikosa kwa sababu mazingira yao hayawaruhusu!!

Kuna mwingine japo hana ajira rasmi lakini ana mzigo wa kulea familia! Hufanya vibarua ili wadogo zake wasome!! Sasa huyu ukimtaka ajitolee hataweza. Ila watoto wa matajiri wana uwezo wa kujitolea maana wataendelea kuhudumiwa bila shida. Lakini mtoto wa mlala hoi kwa vyovyote vile hawezi kumudu kujitolea maana kila siku analazimika kutafuta riziki ya kutwa!!
Naunga mkono hoja yako yote aya ni uhuni wa serikali hii,
 
Chukulia wewe ndio mwajiri

Mwajiriwa anapoanza kazi anafanya makosa kibao.

Inabidi utumie muda wa wafanyakazi wengine wazoefu kuwafundisha kazi na kuwasimamia.

Muda huo unalipa mshahara wa hao wazoefu na wafanyakazi wapya; huku output ikiwa ndogo labda kwa miezi 3-6.

Huyo mfanyakazi mpya akiachwa bado anakuwa na makosa madogo ya hapa na pale; mpaka baada ya mwaka ndio anaanza kukupa production ya kati unayotarajia na kuanza kupata value for money ya mshahara wako unaolipa.

Wakati huo huo kuna kijana anaomba kazi hiyo ambae keshafanya volunteering katika nafasi hiyo sehemu nyingine. Majukumu yake anayaelewa kwa kiasi kikubwa baada ya mwezi tu ya kuzoea mazingira ya kazi mpya output yake iko juu huna hasara ya mwaka mzima na wala upotezi hela nyingi kwenye training.

Wewe ungechagua yupi kati ya hao wawili.

Ni hivi vijana fanyeni volunteering, tena afadhali ata hizo kada zingine, kama ni afya new nurses and MD asilimia kubwa ya ‘medical errors’ zinazo pelekea wagonjwa kupata madhara makubwa au vifo zinasababishwa na mistakes za new recruits.

Inachukua muda sana kuwapa experience medical staff wapya kwa sababu hawa intervention zao ni za kukariri vitabuni bado na little field learning waliyopata kama sehemu ya masomo. Lakini hawana uwezo wa kusoma body language mgonjwa na kuona kama hali imetetereka ghafla wafanye nini.

Sasa unadhani kuna hospitali inaweza mwacha Dr au nurse mwenye experience ya volunteering; ichukue mpya na kuanza kum train wakati production yake ni ndogo.

Watanzania tunapenda kuchukulia vitu rahisi sana, huyo aliefanya work experience kwanza mbele ya mwajiri anaonyesha anaitaka hiyo nafasi na ataitendea haki kuliko wewe ambae huna hiyo experience.

Wengi wetu tunaishi kwenye lala land halafu kupenda kulalamika tu.
 
Kama watala
Chukulia wewe ndio mwajiri

Mwajiriwa anapoanza kazi anafanya makosa kibao.

Inabidi utumie muda wa wafanyakazi wengine wazoefu kuwafundisha kazi na kuwasimamia.

Muda huo unalipa mshahara wa hao wazoefu na wafanyakazi wapya; huku output ikiwa ndogo labda kwa miezi 3-6.

Huyo mfanyakazi mpya akiachwa bado anakuwa na makosa madogo ya hapa na pale; mpaka baada ya mwaka ndio anaanza kukupa production ya kati unayotarajia na kuanza kupata value for money ya mshahara wako unaolipa.

Wakati huo huo kuna kijana anaomba kazi hiyo ambae keshafanya volunteering katika nafasi hiyo sehemu nyingine. Majukumu yake anayaelewa kwa kiasi kikubwa baada ya mwezi tu ya kuzoea mazingira ya kazi mpya output yake iko juu huna hasara ya mwaka mzima na wala upotezi hela nyingi kwenye training.

Wewe ungechagua yupi kati ya hao wawili.

Ni hivi vijana fanyeni volunteering, tena afadhali ata hizo kada zingine, kama ni afya new nurses and MD asilimia kubwa ya ‘medical errors’ zinazo pelekea wagonjwa kupata madhara makubwa au vifo zinasababishwa na mistakes za new recruits.

Inachukua muda sana kuwapa experience medical staff wapya kwa sababu hawa intervention zao ni za kukariri vitabuni bado na little field learning waliyopata kama sehemu ya masomo. Lakini hawana uwezo wa kusoma body language mgonjwa na kuona kama hali imetetereka ghafla wafanye nini.

Sasa unadhani kuna hospitali inaweza mwacha Dr au nurse mwenye experience ya volunteering; ichukue mpya na kuanza kum train wakati production yake ni ndogo.

Watanzania tunapenda kuchukulia vitu rahisi sana, huyo aliefanya work experience kwanza mbele ya mwajiri anaonyesha anaitaka hiyo nafasi na ataitendea haki kuliko wewe ambae huna hiyo experience.

Wengi wetu tunaishi kwenye lala land halafu kupenda kulalamika tu.
Nitakubali tu kama sekretarieti ya ajira inayofanyisha usaili ndio itakayopewa jukumu la kuchagua hao ambao wanataka kujitolea. Nafasi za kujitolea ziwe zinatangazwa kama zinavyotangazwa nafasi za ajira na watu wawe wanaomba na kuzishindania kupitia usaili. Watakaofaulu usaili ndio wapewe nafasi ya kujitolea na majina yao yawe kwenye database wakisubiria ajira!! Lakini kama wakuu wa taasisi na viongozi wengine wataruhusiwa kuchagua watu wa kujitolea hapo ni rushwa na upendeleo hadi basi!!
 
Kama watala

Nitakubali tu kama sekretarieti ya ajira inayofanyisha usaili ndio itakayopewa jukumu la kuchagua hao ambao wanataka kujitolea. Nafasi za kujitolea ziwe zinatangazwa kama zinavyotangazwa nafasi za ajira na watu wawe wanaomba na kuzishindania kupitia usaili. Watakaofaulu usaili ndio wapewe nafasi ya kujitolea na majina yao yawe kwenye database wakisubiria ajira!! Lakini kama wakuu wa taasisi na viongozi wengine wataruhusiwa kuchagua watu wa kujitolea hapo ni rushwa na upendeleo hadi basi!!
Nafasi za kujitolea pia utangazwa rasmi katika website za wizara hasa TAMISEMI na Afya.

Halikadhalika ni jukumu la kijana anaetafuta ajira kupita taasisi mbali kuuliza utaratibu wao wa kuajiri volunteering work, kutuma email HR zao, kwenda kwa work agencies na kutaka kupewa habari kama zikitokea nafasi za volunteering taasisi wanazolenga.

Hii dunia ya kuuza skills zako sio kukaa, kusubiri matangazo ya ajira za serikali wote mkumbilie huko.

Matter of fact vijana pia wanatakiwa wafanye research ya shahada wanazochukua na employability chances zao; vinginevyo bora hiyo miaka 3/4 usipoteze ukasome ufundi baada ya hapo utafute mradi wa kujiajiri.

Dunia ya leo ni ya mikakati, serikali imeshaeleza sana zama za kuajiri wahitimu wote zimepita ni muda wa vijana kuwa wabunifu kwenye route yao ya kupata ajira kwenye soko lenye ushindani mkubwa.

Website za serikali zipo slow kwa sasa halafu inabidi nikimbie sehemu ningekuwekea link za volunteering.

Hao wanaolalamika sio watu wanaojituma kutafuta ajira, wakati wenzao wanachakarika kuongeza nafasi zao za kupata kazi.

👋 got run some errands
 
Back
Top Bottom