MKWECHE
JF-Expert Member
- Apr 8, 2011
- 299
- 64
Sawa ripoti ya Mkaguzi inasema hivyo ila alichambua kiini cha tatizo? Wenyewe MSD wanasema hizo zilizoharibika ni zile zilizotolewa msaada na wafadhili zikaja changanywa na stock za kwao walizokwisha nunua unategemea nini? Ilitakiwa serikali kuwasiliana na MSD kuitaarifu jamani kuna msaada na mbaya zaidi unakuta mara nyingi zinakuwa zinazokaribia kwa matumizi yas binadamu labda bado miezi minne mpaka sita unategemea nini? Sio nawatetea MSD ila mfumo wenyewe ungetakiwa kurekebishwa na huyo CAG angetakiwa ashauri both to Serikali na MSD ukiangalia kwa undani siku hizi ni kutafutana tu, hivi mbona hatusikii Budget ya Idara ya Bunge wametumiaje? Na wamepangiwa kiasi gani kwa Mwaka,hata hizo Tume za Bunge kwa maoin zina misuse Govt fund, what is their role kama walishapitisha budget then wanakwenda kukagua? Na CAG? Je wao wanakaguliwa na nani?
Lakini Mh Sakane Kwa Ukubwa wa Tatizo la Dawa za Binadamu hapa TZ!Ni aibu kutoa Kisingizio cha Kusema stock ya wafadhili ndio ilisababisha Madawa yakawa mengi hadi Kuharibikia Store!Kuna Thinker Mmoja Kasema hata Hospitali za Za Dar Yalipo Makao ya MSD hakuna Madawa!Na hata siku moja haikusikika dawa zimejaa Hospitali za Dar!Licha ya Huku Igangidungu kwa kina Mimi Mkweche wa Mkangafu!
Mie naona MSD ni Donda ndugu halina Tiba!Hata kama dawa ni za Muda Mfupi wangezisambaza kwa vituo vya Kanda ya Mashariki au Kugawa Bure kwenye vituo vyovyote vilivyosajiliwa na waka-State!Kosa la Kuharibu dawa ni sawa na Kuharibu chakula wakati wengine wafa kwa njaa!
MSD ni Madawa Sina Daima!