Mpandafarasi
Member
- Dec 7, 2008
- 57
- 11
MOJA kati ya habari zilizopewa uzito Juma hili ni ile inayoigusa bohari ya madawa (MSD) kusababisha hasara ya dawa zenye thamani ya sh bilioni 5.2 ambazo ziliharibika baada ya kuhifadhiwa kwa muda mrefu.
Hayo yalibainika katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), baada ya makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Deo Filikunjombe, kumbana kaimu mwenyekiti wa MSD, Tekla Shangali, na mkurugenzi mkuu, Joseph Mgaya, ambao walishindwa kutoa ufafanuzi mbele ya kamati na kutakiwa kutoka nje ya kikao.
Fikunjombe, alikuwa akirejea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambayo ilibaini hasara hiyo baada ya mamlaka hiyo kuweka dawa katika hifadhi zake bila kuzisambaza na kusababisha kuharibika.
Tanzania Daima tunaamini kuwa hasara hiyo ingeweza kuepukwa kama kungekuwa na ufuatiliaji na uwajibikaji wa viongozi husika kama wangejali ama kufikiri juu ya uhai wa watu walioko katika hospitali mbalimbali nchini ambao baadhi yao wamekuwa wakikosa fedha za kununulia dawa.
Lakini viongozi hao hawakufanya hivyo, hawakutimiza wajibu wao.
Ikumbukwe kuwa kuna maelfu ya Watanzania wanakufa kwa kukosa dawa hospitalini, huku serikali ikishutumiwa kila wakati.
Tunasema hatuwezi kuvumilia hali hii kwa sababu suala la dawa ni suala nyeti linalogusa maisha ya kila Mtanzania hasa wale wenye kipato cha chini wasio na uwezo wa kupata huduma hiyo kwa kuhimili bei.
Ikumbukwe hii si mara ya kwanza kwa MSD kuharibikiwa na dawa na kusababisha hasara kubwa tumeelezwa kuwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita kuna dawa nyingine zenye thamani ya sh bilioni nane ziliharibika kutokana na uzembe wa watendaji wa bohari na hivyo kuisababishia hasara serikali.
Tuna kila sababu ya kutamka kwamba hii ni aibu na fedheha kubwa kwa nchi maskini kama Tanzania ambapo kila wakati tumekuwa tukilia na hata kuwapigia magoti wahisani watusaidie katika suala zima la afya.
Tunatoa wito kwa serikali, kuhakikisha inawachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi viongozi wa MSD ambao wamekuwa wakilegalega katika nafasi zao na hata kuisababishia hasara kila wakati.
Kamwe hatutakubali kudanganywa kwa kuambiwa kwamba kilichotokea ni ajali iliyokosa kinga; la hasha, tunasema kilichotokea ni uzembe wa baadhi ya viongozi ambao mwisho wa siku huisababishia hasara serikali na Watanzania kwa ujumla.
Source: Tanzania Daima, Jumamosi 04,06 2011 Huu ni uzembe wa viongozi MSD
Nawasilisha
Hayo yalibainika katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), baada ya makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Deo Filikunjombe, kumbana kaimu mwenyekiti wa MSD, Tekla Shangali, na mkurugenzi mkuu, Joseph Mgaya, ambao walishindwa kutoa ufafanuzi mbele ya kamati na kutakiwa kutoka nje ya kikao.
Fikunjombe, alikuwa akirejea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambayo ilibaini hasara hiyo baada ya mamlaka hiyo kuweka dawa katika hifadhi zake bila kuzisambaza na kusababisha kuharibika.
Tanzania Daima tunaamini kuwa hasara hiyo ingeweza kuepukwa kama kungekuwa na ufuatiliaji na uwajibikaji wa viongozi husika kama wangejali ama kufikiri juu ya uhai wa watu walioko katika hospitali mbalimbali nchini ambao baadhi yao wamekuwa wakikosa fedha za kununulia dawa.
Lakini viongozi hao hawakufanya hivyo, hawakutimiza wajibu wao.
Ikumbukwe kuwa kuna maelfu ya Watanzania wanakufa kwa kukosa dawa hospitalini, huku serikali ikishutumiwa kila wakati.
Tunasema hatuwezi kuvumilia hali hii kwa sababu suala la dawa ni suala nyeti linalogusa maisha ya kila Mtanzania hasa wale wenye kipato cha chini wasio na uwezo wa kupata huduma hiyo kwa kuhimili bei.
Ikumbukwe hii si mara ya kwanza kwa MSD kuharibikiwa na dawa na kusababisha hasara kubwa tumeelezwa kuwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita kuna dawa nyingine zenye thamani ya sh bilioni nane ziliharibika kutokana na uzembe wa watendaji wa bohari na hivyo kuisababishia hasara serikali.
Tuna kila sababu ya kutamka kwamba hii ni aibu na fedheha kubwa kwa nchi maskini kama Tanzania ambapo kila wakati tumekuwa tukilia na hata kuwapigia magoti wahisani watusaidie katika suala zima la afya.
Tunatoa wito kwa serikali, kuhakikisha inawachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi viongozi wa MSD ambao wamekuwa wakilegalega katika nafasi zao na hata kuisababishia hasara kila wakati.
Kamwe hatutakubali kudanganywa kwa kuambiwa kwamba kilichotokea ni ajali iliyokosa kinga; la hasha, tunasema kilichotokea ni uzembe wa baadhi ya viongozi ambao mwisho wa siku huisababishia hasara serikali na Watanzania kwa ujumla.
Source: Tanzania Daima, Jumamosi 04,06 2011 Huu ni uzembe wa viongozi MSD
Nawasilisha