Huu mpango wa Serikali ni hatari sana kwa sababu unakwenda kuua ubora wa elimu yetu

May 22, 2016
63
59
Haya ni maoni yangu binafsi kuhusu mpango mpya wa serikali wa kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu wa sayansi uliotangazwa na Suleiman Jaffo Naibu Waziri wa TAMISEMI.

Kwanza ninaomba watu waelewe ya kwamba Ualimu ni taaluma kama zilivyo taaluma zingine, hivyo basi ninawaomba sana wanasiasa kuheshimu taaluma hii. Kitendo cha serikali kutangaza kuchukua wahitimu wa shahada ya sayansi ambao hawana taaluma ya ualimu nakuwapa shortcourses kuhusu ualimu kwa lengo la kuwaajiri kuwa walimu wa masomo ya sayansi, kwa mtizamo wangu naona hii ni dharau kubwa ya wanasiasa katika kada ya ualimu.

Hatuwezi kuboresha elimu yetu kwa kuajiri watu ambao sio qualified teachers.Kama tunataka kuboresha elimu yetu ni lazima serikali iwekeze ziada katika elimu yetu nasio vinginevyo. Kitu kinachonishangaza ni kuona Walimu wa sayansi wapo mitaani tu, wengine wamehitimu mwaka jana na wengine mwaka huu lakini serikali haitaki kuwapatia ajira,

Halafu bungeni Mheshimiwa Naibu Waziri wa ofisi ya rais TAMISEMI Suleiman Jaffo anatoa tamko kwamba serikali imeandaa mpango wa kuwaajiri wahitimu wa shahada ya sayansi ambao hawajasomea taaluma ya ualimu kufundisha masomo ya sayansi,najiuliza ni kwanini hii inafanyika katika kada ya ualimu tu mbona hata katika sekta ya afya kunaupungufu wa wahudumu wa afya kwani nini serikali isiseme na huko iwachukue wahitimu wa shahada ya sayansi nakuwapatia shortcourses ili wakawe wahudumu wa afya katika zahanati, vituo vya afya na hospitali?.

Binafsi nilipoisikia kauli hii ya serikali kuhusu jambo hili la kutatua uhaba wa walimu wa sayansi nimeshindwa kupata picha au mwelekeo wa serikali yetu kuhusu suala la elimu kwani majuzijuzi tena waziri wa elimu Prof Joyce Ndalichako alitoa tamko lingine na kudai kwa kuanzia sasa masomo ya sayansi kwa sekondari ni ya lazima

Wakati anatoa tamko hilo anajua kabsa kunashule za sekondari zingine hazina kabsa maabara za masomo ya sayansi, lakini pia walimu wa masomo ya sayansi hawatoshi kabsa.Unapomlazimisha mwanafunzi kusoma masomo ya sayansi wakati walimu hawapo wakumfundisha, maabara na nyenzo za kufundishia sayansi hazipo hapo ni kumuonea tu mwanafunzi huyo.

Kama serikali inataka kupunguza au kuondoa kabsa tatizo la uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi na hisabati.Inatakiwa kufanya mambo yafuatayo kwa sasa.

1.Kuboresha maslahi ya walimu wa sayansi waliopo, kwani haingii akilini mwalimu wa Sayansi ambaye anaingia darasani kufundisha halafu huyohuyo ndiye anaingia maabara kuandaa practical na kufundisha pia, halafu maslahi yake yakawa sawa na mwalimu wa sanaa.Kiuharisia kama mshahara wa daktari na muuguzi ni tofauti kwa maana daktari anapokea mshahara mkubwa ukilinganisha na nurse.

Kwanini Mwalimu wa Sayansi mshahara wake ulingane sawa na mwalimu wa art wakati Walimu wa Sayansi wamekuwa wanafanya kazi mara mbili ya kufundisha halafu kama lab technician katika mashule ya sekondari lakini pamoja na yote mishahara wanapewa sawa na walimu wa arts.

Walimu wa sayansi wanafanya kazi nzito sana huwezi kulinganisha na walimu wa arts. Kama kweli serikali inadhamira ya kutatua tatizo la walimu wa masomo ya sayansi hainabudi kuongeza mishahara pamoja na kuwapatia posho maalum walimu wa masomo ya sayansi.

Serikali itakapoboresha maslahi ya walimu wa sayansi zaidi automatically hii field itakuwa ni kimbilio la watu wengi sana lakini walimu watafundisha kwa kujituma zaidi nakupelekea ufaulu wa wanafunzi kuwa mkubwa.Endapo serikali ikitekeleza jambo hili, Haitahitajika serikali kuanza kufikiria kuajiri walimu wa sayansi magumashi/mwendokasi ili kumaliza tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi.

2.Serikali itoe ajira kwa walimu wote wa Sayansi waliohitimu mwaka jana na mwaka huu.Serikali itoe ajira kwa wakati kwani ucheleweshaji wa makusudi wa ajira za ualimu hususan wa masomo ya sayansi ni hasara kubwa kwa wanafunzi ambao wengi wao ni watoto wa maskini.Shule za serikali ndio zinazokabiliwa na upungufu huu na waathirika wakubwa katika jambo hili ni watoto wa maskini . Viongozi wakubwa wengi wao watoto wao wanasoma katika shule za binafsi ambazo kimsingi hakuna uhaba wa walimu ndio maana jambo wamekuwa wakiliona kama sio kipaumbele cha serikali.

Kitendo cha serikali kuzuia ajira kwa walimu wa sayansi waliohitimu vyuoni na kutangaza mpango wa kuajiri watu ambao kimsingi hawajasomea ualimu lakini kwa sababu wamesomea shahada ya sayansi tu tafsiri yake ni kama serikali imekusudia kuua ubora wa elimu ya watoto wetu.

Huu mpango wa serikali ukifikiria juujuu unaweza ukaona kama ni mwarobaini wa tatizo la walimu wa masomo ya sayansi lakini ndivyo sivyo kabsa.Naishauri serikali huu mpango iweke pembeni kwanza ifanye research upya kuhusu Negative impacts za mpango huu kabla ya kufanya implementation.

Wako,
Abel Magembe Lugimba.
Kada wa CCM, Kalambo-Rukwa.
 
ndugu yangu kada wa chama,
hoja yako haijapimwa kisayansi. Watu wote wenye shahada za sayansi iwe ni ufundi, kilimo, mifugo, wamesoma na kufaulu vizuru masomo ya sayansi kidato cha sita. Hivyo wanazo sifa za msingi za kuwa walimu wa sayansi. aidha, wameongeza ufahamu wao katika masomo hayo ya sayansi katika kiwango cha shahada japokuwa wamefanya specialization, lakini maarifa yamekuzwa.

Chuo cha ualimu hufundisha namna ya kufundisha (pedagogy) na hawa watu wenye sifa za msingui wanachokosa elimu ya ufundishaji hivyo wanahitaji kupewa elimu hii ili wafundishe. hivyo wakipewa elimu hii wanakuwa ni walimu kamili.

kwa taarifa yako hawa wana sifa ni wazuri kuliko hata crush program ya UDOM.
 
Wewe sio kada wa ccm, kama kweli ni kada basi jiandae kutumbuliwa kwa kuisema serikali tukufu ya mkuruuuu
ukomavu ni kukosoa cham chako na serikali yako,amefanya vyema na ndio utaratibu wa CCM hakuna usultani..suala la msingi nilitaka nimuambie kwenye dharura ni bora wahitimu wa masomo ya sayansi wakafundishe masomo hayo.Mfano wahitimu wa engineering wanaweza kuwa walimu wazuri wa Hisabati,fizikia,kemia...wale biology wataweza kufundisha biologia...so ni sawa tu,japo baada ya muda watapelekwa training ya PGD Education mwaka mmoja. Hii sio mara ya kwanza miaka ya 1999-2002 wanasayansi wengi kutoka SUA,UDSM walipelekwa kuwa walimu na hadi sasa ni walimu bora sana.Pili kama vijana wa sasa wa A-Level wanafundishwa twisheni na ''form sic leavers''...hana tabu.Abel kaleta hoja ya kisomi na inapaswa kujadiliwa kisomi ili na yeye apate mwanga.
 
ndugu yangu kada wa chama,
hoja yako haijapimwa kisayansi. Watu wanacnye shahada za sayansi iwe ni ufundi, kilimo, mifugo, wamesoma na kufaulu vizuru masomo ya sayansi kidato cha sita. Hivyo wanazo sifa za msingi za kuwa walimu wa sayansi. aidha, wameongeza ufahamu wao katika masomo hayo ya sayansi katika kiwango cha shahada japokuwa wamefanya specialization, lakini maarifa yamekuzwa.

Chuo cha ualimu hufundisha namna ya kufundisha (pedagogy) na hawa watu wenye sifa za msingui wanachokosa elimu ya ufundishaji hivyo wanahitaji kupewa elimu hii ili wafundishe. hivyo wakipewa elimu hii wanakuwa ni walimu kamili.

kwa taarifa yako hawa wana sifa ni wazuri kuliko hata crush program ya UDOM.
Uko sawa kabisakabisa swala la kufundisha halina skills nyingi kama utabibu ,
 
Wewe sio kada wa ccm, kama kweli ni kada basi jiandae kutumbuliwa kwa kuisema serikali tukufu ya mkuruuuu

Unaleta uchochezi
Umeambiwa jadili maada ww unaingiza vitu vinavyokuwasha akili mwako why?

Mwenyekiti CCM JF
 
MPANGO WA SERIKALI KUAJIRI WAHITIMU WA SHAHADA YA SAYANSI AMBAO SIO WALIMU UNAKWENDA KUUA UBORA WA ELIMU YETU.

Haya ni maoni yangu binafsi kuhusu mpango mpya wa serikali wa kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu wa sayansi uliotangazwa na Suleiman Jaffo Naibu Waziri wa Tamisemi.

Kwanza ninaomba watu waelewe ya kwamba Ualimu ni taaluma kama zilivyo taaluma zingine, hivyo basi ninawaomba sana wanasiasa kuheshimu taaluma hii. Kitendo cha serikali kutangaza kuchukua wahitimu wa shahada ya sayansi ambao hawana taaluma ya ualimu nakuwapa shortcourses kuhusu ualimu kwa lengo la kuwaajiri kuwa walimu wa masomo ya sayansi, kwa mtizamo wangu naona hii ni dharau kubwa ya wanasiasa katika kada ya ualimu.Hatuwezi kuboresha elimu yetu kwa kuajiri watu ambao sio qualified teachers.Kama tunataka kuboresha elimu yetu ni lazima serikali iwekeze ziada katika elimu yetu nasio vinginevyo. Kitu kinachonishangaza ni kuona Walimu wa sayansi wapo mitaani tu, wengine wamehitimu mwaka jana na wengine mwaka huu lakini serikali haitaki kuwapatia ajira, halafu bungeni Mheshimiwa Naibu Waziri wa ofisi ya rais Tamisemi Suleiman Jaffo anatoa tamko kwamba serikali imeandaa mpango wa kuwaajiri wahitimu wa shahada ya sayansi ambao hawajasomea taaluma ya ualimu kufundisha masomo ya sayansi,najiuliza ni kwanini hii inafanyika katika kada ya ualimu tu mbona hata katika sekta ya afya kunaupungufu wa wahudumu wa afya kwani nini serikali isiseme na huko iwachukue wahitimu wa shahada ya sayansi nakuwapatia shortcourses ili wakawe wahudumu wa afya katika zahanati, vituo vya afya na hospitali?.Binafsi nilipoisikia kauli hii ya serikali kuhusu jambo hili la kutatua uhaba wa walimu wa sayansi nimeshindwa kupata picha au mwelekeo wa serikali yetu kuhusu suala la elimu kwani majuzijuzi tena waziri wa elimu Prof Joyce Ndalichako alitoa tamko lingine na kudai kwa kuanzia sasa masomo ya sayansi kwa sekondari ni ya lazima, wakati anatoa tamko hilo anajua kabsa kunashule za sekondari zingine hazina kabsa maabara za masomo ya sayansi, lakini pia walimu wa masomo ya sayansi hawatoshi kabsa.Unapomlazimisha mwanafunzi kusoma masomo ya sayansi wakati walimu hawapo wakumfundisha, maabara na nyenzo za kufundishia sayansi hazipo hapo ni kumuonea tu mwanafunzi huyo.

Kama serikali inataka kupunguza au kuondoa kabsa tatizo la uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi na hisabati.Inatakiwa kufanya mambo yafuatayo kwa sasa.

1.Kuboresha maslahi ya walimu wa sayansi waliopo, kwani haingii akilini mwalimu wa Sayansi ambaye anaingia darasani kufundisha halafu huyohuyo ndiye anaingia maabara kuandaa practical na kufundisha pia, halafu maslahi yake yakawa sawa na mwalimu wa sanaa.Kiuharisia kama mshahara wa daktari na muuguzi ni tofauti kwa maana daktari anapokea mshahara mkubwa ukilinganisha na nurse. Kwanini Mwalimu wa Sayansi mshahara wake ulingane sawa na mwalimu wa art wakati Walimu wa Sayansi wamekuwa wanafanya kazi mara mbili ya kufundisha halafu kama lab technician katika mashule ya sekondari lakini pamoja na yote mishahara wanapewa sawa na walimu wa arts. Walimu wa sayansi wanafanya kazi nzito sana huwezi kulinganisha na walimu wa arts. Kama kweli serikali inadhamira ya kutatua tatizo la walimu wa masomo ya sayansi hainabudi kuongeza mishahara pamoja na kuwapatia posho maalum walimu wa masomo ya sayansi.Serikali itakapoboresha maslahi ya walimu wa sayansi zaidi automatically hii field itakuwa ni kimbilio la watu wengi sana lakini walimu watafundisha kwa kujituma zaidi nakupelekea ufaulu wa wanafunzi kuwa mkubwa.Endapo serikali ikitekeleza jambo hili, Haitahitajika serikali kuanza kufikiria kuajiri walimu wa sayansi magumashi/mwendokasi ili kumaliza tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi.

2.Serikali itoe ajira kwa walimu wote wa Sayansi waliohitimu mwaka jana na mwaka huu.Serikali itoe ajira kwa wakati kwani ucheleweshaji wa makusudi wa ajira za ualimu hususan wa masomo ya sayansi ni hasara kubwa kwa wanafunzi ambao wengi wao ni watoto wa maskini.Shule za serikali ndio zinazokabiliwa na upungufu huu na waathirika wakubwa katika jambo hili ni watoto wa maskini . Viongozi wakubwa wengi wao watoto wao wanasoma katika shule za binafsi ambazo kimsingi hakuna uhaba wa walimu ndio maana jambo wamekuwa wakiliona kama sio kipaumbele cha serikali.Kitendo cha serikali kuzuia ajira kwa walimu wa sayansi waliohitimu vyuoni na kutangaza mpango wa kuajiri watu ambao kimsingi hawajasomea ualimu lakini kwa sababu wamesomea shahada ya sayansi tu tafsiri yake ni kama serikali imekusudia kuua ubora wa elimu ya watoto wetu. Huu mpango wa serikali ukifikiria juujuu unaweza ukaona kama ni mwarobaini wa tatizo la walimu wa masomo ya sayansi lakini ndivyo sivyo kabsa.Naishauri serikali huu mpango iweke pembeni kwanza ifanye research upya kuhusu Negative impacts za mpango huu kabla ya kufanya implementation.

Wako,
Abel Magembe Lugimba.
Kada wa CCM, Kalambo-Rukwa.

Hivi unajua maana ya kuwa mwalimu ni nini? Ualimu kwa asilimia 90% ni content na asilimia zilizobaki 10% ni ethics ambazo ndo serikali imesema itaenda kuwafundisha hawa watu, mtu ambae kahitimu shahada ya sayansi chuo kikuu maana yake amesoma PCM, PCB, CBG, PGM advance, maana nyingine ni kwamba alifaulu vizuri O level masomo hayo na akafaulu vizuri A level na akafaulu vizuri Chuo kikuu. Sasa kutokana na ugumu wa ajira mtaani, serikali inachukuwa hawa watu na kuwapa course ya kuwawszesha kutumia maarifa yao kusaidia vijana wetu, Ni nini unapinga hapo?
 
Mpango ni mzuri ila wasiwasi wangu ni kwa serikali kama itamudu kulipa mishara ya hao graduate. Pia hawa ni wazuri ukilinganisha na form four failure wanaopelekwa kusomea ualimu halafu tunategemea ufaulu mzuri kwa watoto wetu.
 
Watawapata wapi, yaani graduate wa Agriculture general kutoka SUA anayeweza kupata salary ya 1M +aende akafundishe wakati salary yenyewe kichele 570, na mazingira ya kutisha ya kazi. Labda wawaajiri wale waliokosea kozi wakasoma Pure Chemistry, Physics, Biology, Mathematics etc ambao ni wachache sana. Otherwise, wawaajiri wastaafu.
 
Hakuna tatizo kwanza ifaamike kuwa waliospecialize kwenye hayo masomo ya sayansi wanauwezo mkubwa sana mfano mtu kasoma Bsc in mathematics unataka kuseme huyu ana uwezo na uelewa wa maths nabado wataongezewa mafunzo so ninachojua hawa watakuwa na uwezo mkubwa sana katika hayo masomo ya sayansi. Achakupotoshaa mleta mada
 
Mpango ni mzuri ila wasiwasi wangu ni kwa serikali kama itamudu kulipa mishara ya hao graduate. Pia hawa ni wazuri ukilinganisha na form four failure wanaopelekwa kusomea ualimu halafu tunategemea ufaulu mzuri kwa watoto wetu.
Mkuu kwa hapa serikali wala isijisumbue, itangaze mishahara sawa na ile inayowalipa waalimu wa kawaida waliohitimu shahada vyuo vikuu, watakaokuwa tayar waende, watakaoona mshahara mdogo waache.
 
Mkuu, hapo mimi naona umeandika pumba.

Hivi unajua maana ya kuwa mwalimu ni nini? Ualimu kwa asilimia 90% ni content na asilimia zilizobaki 10% ni ethics ambazo ndo serikali imesema itaenda kuwafundisha hawa watu, mtu ambae kahitimu shahada ya sayansi chuo kikuu maana yake amesoma PCM, PCB, CBG, PGM advance, maana nyingine ni kwamba alifaulu vizuri O level masomo hayo na akafaulu vizuri A level na akafaulu vizuri Chuo kikuu. Sasa kutokana na ugumu wa ajira mtaani, serikali inachukuwa hawa watu na kuwapa course ya kuwawszesha kutumia maarifa yao kusaidia vijana wetu, Ni nini unapinga hapo?

Na ww acha kupotosha watu. Ualimu ni teaching skills na psychology. fuatilia course wanazosomea ualimu. mfano diloma ya ualimu course zake ni 1. Teaching skills and methodology, 2. Psychology, 3. Foundation of education 4. Philosophy of education. 5. Research methodology 6. Development studies hizo ni core subject au course. baada ya hapo unachukua masomo mawili ya kufundishia kama ni Physics na chemistry nk. sasa hapo 90% ya content inatoka wapi?
 
kinachonishangaza wale sayansi wa dodoma kwanini wamewapeleka primary wengi wao qakiwa na ufaulu mzur kwanini wasingewaendeleza hawa tukapata walim wa o level na primary???mi naina serikali inaekt
 
Haya ni maoni yangu binafsi kuhusu mpango mpya wa serikali wa kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu wa sayansi uliotangazwa na Suleiman Jaffo Naibu Waziri wa Tamisemi.

Kwanza ninaomba watu waelewe ya kwamba Ualimu ni taaluma kama zilivyo taaluma zingine, hivyo basi ninawaomba sana wanasiasa kuheshimu taaluma hii. Kitendo cha serikali kutangaza kuchukua wahitimu wa shahada ya sayansi ambao hawana taaluma ya ualimu nakuwapa shortcourses kuhusu ualimu kwa lengo la kuwaajiri kuwa walimu wa masomo ya sayansi, kwa mtizamo wangu naona hii ni dharau kubwa ya wanasiasa katika kada ya ualimu.

Hatuwezi kuboresha elimu yetu kwa kuajiri watu ambao sio qualified teachers.Kama tunataka kuboresha elimu yetu ni lazima serikali iwekeze ziada katika elimu yetu nasio vinginevyo. Kitu kinachonishangaza ni kuona Walimu wa sayansi wapo mitaani tu, wengine wamehitimu mwaka jana na wengine mwaka huu lakini serikali haitaki kuwapatia ajira, halafu bungeni Mheshimiwa Naibu Waziri wa ofisi ya rais Tamisemi Suleiman Jaffo anatoa tamko kwamba serikali imeandaa mpango wa kuwaajiri wahitimu wa shahada ya sayansi ambao hawajasomea taaluma ya ualimu kufundisha masomo ya sayansi,najiuliza ni kwanini hii inafanyika katika kada ya ualimu tu mbona hata katika sekta ya afya kunaupungufu wa wahudumu wa afya kwani nini serikali isiseme na huko iwachukue wahitimu wa shahada ya sayansi nakuwapatia shortcourses ili wakawe wahudumu wa afya katika zahanati, vituo vya afya na hospitali?.

Binafsi nilipoisikia kauli hii ya serikali kuhusu jambo hili la kutatua uhaba wa walimu wa sayansi nimeshindwa kupata picha au mwelekeo wa serikali yetu kuhusu suala la elimu kwani majuzijuzi tena waziri wa elimu Prof Joyce Ndalichako alitoa tamko lingine na kudai kwa kuanzia sasa masomo ya sayansi kwa sekondari ni ya lazima, wakati anatoa tamko hilo anajua kabsa kunashule za sekondari zingine hazina kabsa maabara za masomo ya sayansi, lakini pia walimu wa masomo ya sayansi hawatoshi kabsa.Unapomlazimisha mwanafunzi kusoma masomo ya sayansi wakati walimu hawapo wakumfundisha, maabara na nyenzo za kufundishia sayansi hazipo hapo ni kumuonea tu mwanafunzi huyo.

Kama serikali inataka kupunguza au kuondoa kabsa tatizo la uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi na hisabati.Inatakiwa kufanya mambo yafuatayo kwa sasa.

1.Kuboresha maslahi ya walimu wa sayansi waliopo, kwani haingii akilini mwalimu wa Sayansi ambaye anaingia darasani kufundisha halafu huyohuyo ndiye anaingia maabara kuandaa practical na kufundisha pia, halafu maslahi yake yakawa sawa na mwalimu wa sanaa.Kiuharisia kama mshahara wa daktari na muuguzi ni tofauti kwa maana daktari anapokea mshahara mkubwa ukilinganisha na nurse.

Kwanini Mwalimu wa Sayansi mshahara wake ulingane sawa na mwalimu wa art wakati Walimu wa Sayansi wamekuwa wanafanya kazi mara mbili ya kufundisha halafu kama lab technician katika mashule ya sekondari lakini pamoja na yote mishahara wanapewa sawa na walimu wa arts. Walimu wa sayansi wanafanya kazi nzito sana huwezi kulinganisha na walimu wa arts. Kama kweli serikali inadhamira ya kutatua tatizo la walimu wa masomo ya sayansi hainabudi kuongeza mishahara pamoja na kuwapatia posho maalum walimu wa masomo ya sayansi.

Serikali itakapoboresha maslahi ya walimu wa sayansi zaidi automatically hii field itakuwa ni kimbilio la watu wengi sana lakini walimu watafundisha kwa kujituma zaidi nakupelekea ufaulu wa wanafunzi kuwa mkubwa.Endapo serikali ikitekeleza jambo hili, Haitahitajika serikali kuanza kufikiria kuajiri walimu wa sayansi magumashi/mwendokasi ili kumaliza tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi.

2.Serikali itoe ajira kwa walimu wote wa Sayansi waliohitimu mwaka jana na mwaka huu.Serikali itoe ajira kwa wakati kwani ucheleweshaji wa makusudi wa ajira za ualimu hususan wa masomo ya sayansi ni hasara kubwa kwa wanafunzi ambao wengi wao ni watoto wa maskini.Shule za serikali ndio zinazokabiliwa na upungufu huu na waathirika wakubwa katika jambo hili ni watoto wa maskini . Viongozi wakubwa wengi wao watoto wao wanasoma katika shule za binafsi ambazo kimsingi hakuna uhaba wa walimu ndio maana jambo wamekuwa wakiliona kama sio kipaumbele cha serikali.

Kitendo cha serikali kuzuia ajira kwa walimu wa sayansi waliohitimu vyuoni na kutangaza mpango wa kuajiri watu ambao kimsingi hawajasomea ualimu lakini kwa sababu wamesomea shahada ya sayansi tu tafsiri yake ni kama serikali imekusudia kuua ubora wa elimu ya watoto wetu. Huu mpango wa serikali ukifikiria juujuu unaweza ukaona kama ni mwarobaini wa tatizo la walimu wa masomo ya sayansi lakini ndivyo sivyo kabsa.Naishauri serikali huu mpango iweke pembeni kwanza ifanye research upya kuhusu Negative impacts za mpango huu kabla ya kufanya implementation.

Wako,
Abel Magembe Lugimba.
Kada wa CCM, Kalambo-Rukwa.
Kwa upande wangu naona kuwa kwakuwa tunatatizo hili la uhaba wa walimu wa sayans haina shida sana kuwaajiri wahitimu wengine wa sayans wasio waalim hii iwe kama ni hatua ya kwanza tu katka kutatua hili tatizo kwani simba akikosa nyama hula nyasi.

Lakini ili kuilinda Taaluma ya ualimu jambo hili halitakiwi kuwa endelevu kwakuwa ualimu ni Taaluma muhimu sana hivyo haitakiwi kuwa kama jalala.

Njia ya kuboresha maslahi kwa walimu ya sayansi ni bora zaidi ingawa itachelewa kutatua tatizo.
 
Kuna watu waliosoma taaluma za sayansi ni wazuri tu kwa kufundisha mfano Mtu kasoma BSc laboratory science and biotechnology atakuwa mwl mzuri wa masomo ya biology na chemistry both theoretically and practically , walisoma engeneering courses wazuri wa mathematic, physics kozi nyingi wanawezo fit kuwa walimu wazuri kama kilimo walimu wa kilimo, waliosoma informatic wazuri w somo la compter, na mathematcs, walosoma environmetal science waweza kuwa wazuri kwa geography
 
ndugu yangu kada wa chama,
hoja yako haijapimwa kisayansi. Watu wote wenye shahada za sayansi iwe ni ufundi, kilimo, mifugo, wamesoma na kufaulu vizuru masomo ya sayansi kidato cha sita. Hivyo wanazo sifa za msingi za kuwa walimu wa sayansi. aidha, wameongeza ufahamu wao katika masomo hayo ya sayansi katika kiwango cha shahada japokuwa wamefanya specialization, lakini maarifa yamekuzwa.

Chuo cha ualimu hufundisha namna ya kufundisha (pedagogy) na hawa watu wenye sifa za msingui wanachokosa elimu ya ufundishaji hivyo wanahitaji kupewa elimu hii ili wafundishe. hivyo wakipewa elimu hii wanakuwa ni walimu kamili.

kwa taarifa yako hawa wana sifa ni wazuri kuliko hata crush program ya UDOM.
mbona huyo kada kaeleza vizuri .....wawachukue hao wenye shahada mbalimbali za sayansi wakawe wauguzi mana huko pia kuna upungufu
 
Karibuni sana wadau wa JamiiForums kwa mjadala.

Pamoja na ukada wako,umedhihirisha jinsi ulivyo mweupe,unazifahamu sifa zinazomuwezesha mtu kujiunga na kozi ya shahada ya Sayansi?Mtu hachukui kozi hiyo kwa kubahatisha.Ili upate nafasi ya kujiunga na masomo ya kidato cha tano (Sayansi),lazima uwe umefaulu vizuri masomo ya Sayansi kidato cha nne.

Na ili upate fursa ya kujiunga na kozi za "shahada za Sayansi" ni lazima uwe umefanya vizuri katika matokeo ya Mitihani yako ya kidato cha sita,na ili utunukiwe shahada yako ya Sayansi lazima uwe umeasisiwa vizuri katika kozi yako ya shahada ya Sayansi.

Sasa mtu aliyekidhi vigezo na kuwa na sifa zilizomuwezesha kutoka ngazi moja ya kielimu na kuingia ngazi nyingine hadi anafikia kupata shahada yake ya Sayansi atashindwaje kuwa Mwalimu wa Sayansi ikiwa atapatiwa fursa ya kufundishwa mbinu za ufundishaji na ujifunzaji?

Kimsingi kozi ya ualimu kwa kiasi kikubwa si kozi ya kitaaluma,anayechukua kozi ya ualimu anapaswa kuwa na Taaluma ya masomo atakayokwenda kuyafundisha.Katika vyuo vya ualimu,walimu hawafundishwi Hisabati(kwa mfano),hufundishwa namna ya kuyatumia maarifa ya hisabati waliyonayo kuwaongoza wanafunzi wao kulifahamu somo la hisabati.

Hufundishwa mbinu za "kuhawilisha" maarifa waliyonayo kwenda kwa mwanafunzi,hufundishwa mbinu za kumuelewa mwanafunzi wake ili aweze kubaini mbinu bora za kumuwezesha mwanafunzi alielewe somo lake.

Katika vyuo vya ualimu wanafunzi wa kozi ya ualimu hawafundishwi Sayansi kama somo la kitaaluma,hufundishwa misingi ya Elimu,Saikolojia ya Elimu,Mitaala ya Elimu na Ufundishaji,hupewa skills za ualimu tu ili waweze kuwaelewa mwanafunzi wao,hufundishwa matumizi ya zana,njia na mbinu za ufundishaji,hayo ndiyo afundishwayo Mwalimu achukuapo kozi ya ualimu.

Kama Mwalimu hana umahiri na ujuzi wa kutosha wa somo husika,hata akipatiwa mbinu za ufundishaji hawezi kuwa Mwalimu mahiri kwa sababu hana upeo wa kutosha katika Yale atakayoyafundisha.Hivyo Mwalimu bora ni yule aliyepatiwa Elimu bora(aliyefaulu Mitihani yake) na kupatiwa mbinu bora za ufundishaji na ujifunzaji,

Sasa kama wahitimu hao wa Sayansi ni mabingwa wa Sayansi waliosoma vizuri,waliopikwa na kuiva katika nyanja za kisayansi,kuwabadilisha mabingwa hao wa Sayansi na wanaoielewa Sayansi na kuwafanya kuwa walimu wa Sayansi ni jambo dogo sana.Hilo ni jambo jema na ninamuunga mkono waziri katika mkakati huo wenye lengo la kuwapatia watoto wetu wataalamu halisi wa Sayansi.

Pamoja na kwamba Mimi si mwalimu,lakini nikipatiwa skills za ufundishaji na kisha kukabidhiwa darasa,lazima wanafunzi wangu wapagawe!Nilipiga msuli wa kutosha wa PCM(Engineering science,Chemistry na Mathematics),nikapiga 'digit"pale kiungani-TTS,kisha nikapiga msuli wa kutosha advanced nikapasua na kwenda chuo,halafu unifundishe mbinu za ualimu nishindwe kukimbiza?Khaaaa!! Sitaki tu kuwa Mwalimu ila uwezo wa kufundisha masomo ya Sayansi ninao.
 
Kwangu mimi naona kitu kikubwa anacjotakiwa kuwa nacho mwalimu ni 1.uelewa wa anachofundisha na 2.uwezo wa kuhamisha hicho anachokielewa kikaeleweka kwa lugha rahisi kwa mtu mwingine (transfer of knowledge). Mtu mwenye vitu hivi viwili anaweza kufundisha kwa mafanikio popote dunian na wanafunz watampenda na kumfurahia.
 
Back
Top Bottom