Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Salamu kutoka Pemba zinasema kumwambia Huseini Mwinyi waziri wa kupachikwa wa ulinzi hapa Tanzania kuwa ,hawataogopa vifaru wala tembo ,na mabomu yaliofichwa kwenye madalaja mabovu na mengine kulipuka kwenye nyumba wasizoishi watu ni mipango yake akishirikisha vyombo vya ulinzi na usalama.
Habari ambazo zinazidi kutokeza baada ya Waziri mmoja kutamka kuwa atapeleka vikosi vyote kwenda kulinda amani Pemba na upande mwingine Husein Mwinyi akidai kuwa atapeleka majeshi ikiwa ataombwa na vyombo vya serikali ya Zanzibar kufanya hivyo.
Kosa ambalo wamelifanya wapotofu hawa ni kutokufahamiana au kutokufahamishana ni namna gani waanze na watekeleze, katika kuhangaika kwao imetokezea kuwa majeshi na vifaru vimeonekana juzi na jana vikiranda kabla hata hawajatoa kauli zao ,kauli zimefuatilia wakati utekelezaji umeshaanza kwa maana ni mambo yaliopangwa kufanywa.
Hayo yote hayanisikitishi ila pale nionapo CCM inatumia vyombo vya dola kama mali yao na vipo kwa ajili ya kuwaweka wao madarakani. Endeleeni hivyo hivyo mufahamu tu ,wengi wa watawala walikuwa na vyombo na nguvu kuliko mlizo nazo na leo hii hawajulikani hata walipo na wengine wapo kwenye mahakama na wengine wapo jela na wengine wanasubiri hukumu na wengine wanasubiri kukamatwa.
Msidhanie kuwa likitokea la kutokea mtaachiwa tu kama mnavyowaachia mafisadi ,mnaangaliwa kwa jicho linalotegemea kuwa na ushahidi kamili kabisa.
jambo jingine ambalo ni lazima muweke katika akili zenu zilizojaa tamaa kuwa Pemba ni sehemu ndogo sana mnaweza kufanya unyama kwa kadiri mnayoweza na hakuna wa kukuzuieni ila jambo moja Pemba karibu asilimia kubwa au wote ni waIslamu ,Huseini Mwinyi inasemekana ni muislamu halikadhalika na hao wa Unguja nao inasemekana ni Waislamu ,ifahamike tu kuwa hapa hapatafutwi undugu au ujamaa ,la hasha wandugu ,hakuna kul;azimishana katika kuufuata Uislamu ,hilo mulielewe kwa uwazi kabisa ,ninachokihofia ikiwa Waislamu hawa walio wengi hapo Pemba wataona wamevamiwa na kutaka kunyanganywa haki yao basi Dini ya Kiislamu inawaruhusu kufa na mtu ,Huseini analielewa hilo halikadhalika na baba yake nae pia analielewa ,hivyo hayo majeshi ya vifaru na tembo pelekeni kwa wingi sana ,kama wayahudi wanavyowafahamisha kwani vitendo hivyo ni vitendo vinavyotumiwa na wayahudi dhidi ya Wapalestina na hadi leo Wapalestina wapo na msimamo wao haujatetereka.
Kingine ambacho kwa akili yenu potofu mnaona kupeleka majeshi ya vifaru na tembo huko Pemba ni kuzima upinzani na kuua mnasahau kuwa Pemba ni cheche tu moto ukienea basi ni Tanzania nzima na cheche haizuiliki kwa vishindo inataka akili ya mtu anaeelewa maana halisi ya cheche.Vishindo vyenu vitasababisha cheche kuenea na kurukia sehemu zingine hapo ndipo mtakapojua kuwa Pemba ni sehemu ndogo sana ya mambo ambayo mnataka kuyazima.
Habari ambazo zinazidi kutokeza baada ya Waziri mmoja kutamka kuwa atapeleka vikosi vyote kwenda kulinda amani Pemba na upande mwingine Husein Mwinyi akidai kuwa atapeleka majeshi ikiwa ataombwa na vyombo vya serikali ya Zanzibar kufanya hivyo.
Kosa ambalo wamelifanya wapotofu hawa ni kutokufahamiana au kutokufahamishana ni namna gani waanze na watekeleze, katika kuhangaika kwao imetokezea kuwa majeshi na vifaru vimeonekana juzi na jana vikiranda kabla hata hawajatoa kauli zao ,kauli zimefuatilia wakati utekelezaji umeshaanza kwa maana ni mambo yaliopangwa kufanywa.
Hayo yote hayanisikitishi ila pale nionapo CCM inatumia vyombo vya dola kama mali yao na vipo kwa ajili ya kuwaweka wao madarakani. Endeleeni hivyo hivyo mufahamu tu ,wengi wa watawala walikuwa na vyombo na nguvu kuliko mlizo nazo na leo hii hawajulikani hata walipo na wengine wapo kwenye mahakama na wengine wapo jela na wengine wanasubiri hukumu na wengine wanasubiri kukamatwa.
Msidhanie kuwa likitokea la kutokea mtaachiwa tu kama mnavyowaachia mafisadi ,mnaangaliwa kwa jicho linalotegemea kuwa na ushahidi kamili kabisa.
jambo jingine ambalo ni lazima muweke katika akili zenu zilizojaa tamaa kuwa Pemba ni sehemu ndogo sana mnaweza kufanya unyama kwa kadiri mnayoweza na hakuna wa kukuzuieni ila jambo moja Pemba karibu asilimia kubwa au wote ni waIslamu ,Huseini Mwinyi inasemekana ni muislamu halikadhalika na hao wa Unguja nao inasemekana ni Waislamu ,ifahamike tu kuwa hapa hapatafutwi undugu au ujamaa ,la hasha wandugu ,hakuna kul;azimishana katika kuufuata Uislamu ,hilo mulielewe kwa uwazi kabisa ,ninachokihofia ikiwa Waislamu hawa walio wengi hapo Pemba wataona wamevamiwa na kutaka kunyanganywa haki yao basi Dini ya Kiislamu inawaruhusu kufa na mtu ,Huseini analielewa hilo halikadhalika na baba yake nae pia analielewa ,hivyo hayo majeshi ya vifaru na tembo pelekeni kwa wingi sana ,kama wayahudi wanavyowafahamisha kwani vitendo hivyo ni vitendo vinavyotumiwa na wayahudi dhidi ya Wapalestina na hadi leo Wapalestina wapo na msimamo wao haujatetereka.
Kingine ambacho kwa akili yenu potofu mnaona kupeleka majeshi ya vifaru na tembo huko Pemba ni kuzima upinzani na kuua mnasahau kuwa Pemba ni cheche tu moto ukienea basi ni Tanzania nzima na cheche haizuiliki kwa vishindo inataka akili ya mtu anaeelewa maana halisi ya cheche.Vishindo vyenu vitasababisha cheche kuenea na kurukia sehemu zingine hapo ndipo mtakapojua kuwa Pemba ni sehemu ndogo sana ya mambo ambayo mnataka kuyazima.