Hujuma Ubalozi wa Tanzania Sweden

Kichakoro

JF-Expert Member
Sep 10, 2008
3,065
5,393
Ndugu wanabodi,

Tanzania sasa tunahujumiwa hata na balozi zetu, hii sasa inatisha kisa chenyewe kiko hivi.

Mimi ni Mtanzania ninaishi Denmark ingawa sio mwanachama rasmi wa umoja wa watanzania hapa Denmark (TANDEN). TANDEN ilifanya summer party 30.08.2008 lakini kawaida ya party zao huwa zinatanguliwa na mada za kuitangaza Tanzania na hasa utaliii kwani siku hiyo huwa inawaleta watu wa mataifa mbali mbali hivyo TANDEN hutumia wasaa huo kuitangaza nchi yetu of which is very good.

Aliyetoa mada kuhusu Tanzania kwa kweli alinigusa na alielezea kwa ufasaha vivutio vya Tanzania na hata girl friend wangu amehamasika kwenda Tanzania. Tulipomuomba mtoa mada kuhusu vipeperushi ambavyo mtu akitaka kusoma zaidi ndipo nilipogundua hujuma yenyewe. Maelezo yake ni kama ifuatavyo:

Ubalozi wa Tanzania Sweden kwanza uliombwa kuleta bronchure za kuitangaza Tanzania (Tanzania the Land of Kilimanjaro, Seringeti and Zanzibar) ambazo serikali imetumia gharama nyingi kuzichapisha na kisha kuzisambaza kwenye balozi zake zote.

Cha kushangaza kila waaandaji walipojaribu kuwasiliana na ubalozi waliambiwa zitakuja wasiwe na wasi wasi. Cha kusikitisha Zaidi baadae zikaja taarifa oooh ni gharama kuzisafirisha. wakati wanasema ni gharama balozi alikuja Denmark 25.08.2008 kwa ajili ya seminar ya kuwavutia wawekezaji wa kidanish kwenda kuwekeza Tanzania, Hakuleta hakutaka hata kuonana na watanzania waishio Denmark.

Ila alikuwa na nafasi ya kuonana na wanaCCM mimi nikiwa ni mmojawapo mike, Mzee msimbazi na wengine tuliokutana shame uponi you balozi. swali mtauliza hujuma iko wapi????

Moja serilkali imetumia gharama kuchapisha vipeperushi ili viwafikie watu na sio vikae kwenye maboksi kwenye ofisi za balozi hivyo hela za walipa kodi hazikutumika kama ilivyotarajiwa je balozi hajahujumu uchumi?????

Pili kama aliweza kuja hapa Denmark na delegation yake walishindwa hata kuja na vipeperushi ishirini ambavyo havifiki kilo moja wakati ni hela za walala hoi zimetumika kuwgharamia safari yao, sio hujumaa hiii????????

Kuna tetesi kwamba anaondoka ama anabadilishwa kituo, ila habari za uhakika nilizozipata ni kwamba anastaafishwa kwa manufaa ya UMMA, lakimi je kustaafishwa ama kuhama kituo kunakufanya mtu asitimize wajibu wake???? Je ndio aliamua kufanya retaliation kwa njia hiyo??????

Tunao mabalozi wengi wa aina Dr. Ben Moses sehemu nyingi ni muda wa kusema HATUWATAKI.

OMBI kwa ndugu Mh. Kikwete sasa umefika wakati wa balozi zifanye kazi kwa manufaa ya watanzania wote waishio nje na wale waliopo nchini. HIVYO MTU UTKAYEMLETA KAMA BALOZI SWEDEN HAKIKISHA NI MCHAPA KAZI, MZALENDO, MPENDA MAENDELEO, ANAYEPENDA KUTUMIKIA KULIKO KUTUMIKIWA, na ZAIDI YA YOTEASIWE FISADI

Ndugu zangu Watanzania popote mlipo tuchukue jukumu la kuitangaza Tanzania kama wenzetu wa TANDEN wanavyofanya, Tuwaumbue mabalozi wazembe bila woga wala kumuonea.

Kilimanjaro ni yetu, Kiswahili lugha yetu na Tanzania nchi yangu,

asante
 
Ndugu yangu Kichakoro, poleni sana...! Hivyo ndio hali halisi ya Balozi zote za Tanzania, yaani zinakera...! Mabalozi wetu wapo kwenye ubalozi kwa ajili ya kusubiri kuhudhuria dhifa na sherehe tu...! Tena, nimejaribu kufuatilia, watu wengi wanaoteuliwa kuwa mabalozi huwa ni baadhi ya maafisa wa serikali walioshindikana sasa sehemu ya kuwatupia inakua ni huko ubalozini...! Hawana taaluma yoyote kuhusu foreign policy, tourism and sovereign advertisment...!

Wengi wa mabalozi na Foreign Service officers (FSO) wanapewa nafasi hizo kwa kujuana zaidii kuliko ufanisi....! Wengi wanafurahia kwenda huko nje wa ajili ya kutembea tu na sio kwenda kufanya kazi....!

Balozi nyingi huko nje hazina msaada wowote tena unapopata shida ukienda ubalozini unonekana kama ni mhalifu tena unadharauliwa....!

Pole sana kaka....!
 
Ndugu yangu Kichakoro, poleni sana...! Hivyo ndio hali halisi ya Balozi zote za Tanzania, yaani zinakera...!

Nami pia nampa pole zangu ndugu yetu Kichakoro.

Lakini ndugu yangu Mhafidhina, sio kwamba balozi zote za Tanzania zina matatizo hayo.

Mfano Balozi wa Tanzania katika nchi za BeNeLux (Kingdom of Belgium, the Kingdom of the Netherlands, and the Grand Duchy of Luxembourg) huwa anashirikiana vizuri na WaTanzania waliopo katika nchi hizo. Hata mfano ulio hai alituma vipeperushi, video za kuitangaza Tanzania na maliasili yake na hata kushiriki yeye mwenyewe sherehe za usiku wa mwafrika zilizofanyika chuoni UNESCO-IHE kilichopo jijini Delft, tarehe 15 mwezi wa 8 mwaka huu.
 
Majungu.....

Masatu Si udaku

Mimi ni mdau hapa Denmak kwanza namshukuru mdau aliyeweka hiyo post.
Aliyo sema ni kweli na nimewasiliana na viongozi wa TANDEN wamenihakikishia ni kweli aliyoandika huyo bwana ni kweli na kuna zaidi ya hilo ila kwa sababu si msemaji wa TANDEN na sio mwanachama nachelea kusema mengi zaidi.

Ni kweli Balozi alikuja hapa Copenhagen kwa mwaliko wa serikali ya hapa aje kuelezea vivutio vya uwekezaji Tanzania. kwa habari zaidi soma www.um.dk/da/menu/Udviklingspolitik...legationTilTanzaniaAfholdtDen13Og26August.htm
sorry maana ipo kwenye lugha ya kigeni hii kudhirisha kweli balozi alikuepo

Pia kuna dada niliongea naye siku ya part huyo dada anaorganise safari kwa wanaotaka kwenda kutalii nyumbani na yeye anatoa same complain.
kwa ujumla ubazo wetu sweden ni Kero hivyo kama kweli anaondoka basi akapumzike kwa amani.
 
Ndugu wanabodi,

Tanzania sasa tunahujumiwa hata na balozi zetu, hii sasa inatisha kisa chenyewe kiko hivi.

Mimi ni Mtanzania ninaishi Denmark ingawa sio mwanachama rasmi wa umoja wa watanzania hapa Denmark (TANDEN). TANDEN ilifanya summer party 30.08.2008 lakini kawaida ya party zao huwa zinatanguliwa na mada za kuitangaza Tanzania na hasa utaliii kwani siku hiyo huwa inawaleta watu wa mataifa mbali mbali hivyo TANDEN hutumia wasaa huo kuitangaza nchi yetu of which is very good.

Aliyetoa mada kuhusu Tanzania kwa kweli alinigusa na alielezea kwa ufasaha vivutio vya Tanzania na hata girl friend wangu amehamasika kwenda Tanzania. Tulipomuomba mtoa mada kuhusu vipeperushi ambavyo mtu akitaka kusoma zaidi ndipo nilipogundua hujuma yenyewe. Maelezo yake ni kama ifuatavyo:

Ubalozi wa Tanzania Sweden kwanza uliombwa kuleta bronchure za kuitangaza Tanzania (Tanzania the Land of Kilimanjaro, Seringeti and Zanzibar) ambazo serikali imetumia gharama nyingi kuzichapisha na kisha kuzisambaza kwenye balozi zake zote.

Cha kushangaza kila waaandaji walipojaribu kuwasiliana na ubalozi waliambiwa zitakuja wasiwe na wasi wasi. Cha kusikitisha Zaidi baadae zikaja taarifa oooh ni gharama kuzisafirisha. wakati wanasema ni gharama balozi alikuja Denmark 25.08.2008 kwa ajili ya seminar ya kuwavutia wawekezaji wa kidanish kwenda kuwekeza Tanzania, Hakuleta hakutaka hata kuonana na watanzania waishio Denmark.

Ila alikuwa na nafasi ya kuonana na wanaCCM mimi nikiwa ni mmojawapo mike, Mzee msimbazi na wengine tuliokutana shame uponi you balozi. swali mtauliza hujuma iko wapi????

Moja serilkali imetumia gharama kuchapisha vipeperushi ili viwafikie watu na sio vikae kwenye maboksi kwenye ofisi za balozi hivyo hela za walipa kodi hazikutumika kama ilivyotarajiwa je balozi hajahujumu uchumi?????

Pili kama aliweza kuja hapa Denmark na delegation yake walishindwa hata kuja na vipeperushi ishirini ambavyo havifiki kilo moja wakati ni hela za walala hoi zimetumika kuwgharamia safari yao, sio hujumaa hiii????????

Kuna tetesi kwamba anaondoka ama anabadilishwa kituo, ila habari za uhakika nilizozipata ni kwamba anastaafishwa kwa manufaa ya UMMA, lakimi je kustaafishwa ama kuhama kituo kunakufanya mtu asitimize wajibu wake???? Je ndio aliamua kufanya retaliation kwa njia hiyo??????

Tunao mabalozi wengi wa aina Dr. Ben Moses sehemu nyingi ni muda wa kusema HATUWATAKI.

OMBI kwa ndugu Mh. Kikwete sasa umefika wakati wa balozi zifanye kazi kwa manufaa ya watanzania wote waishio nje na wale waliopo nchini. HIVYO MTU UTKAYEMLETA KAMA BALOZI SWEDEN HAKIKISHA NI MCHAPA KAZI, MZALENDO, MPENDA MAENDELEO, ANAYEPENDA KUTUMIKIA KULIKO KUTUMIKIWA, na ZAIDI YA YOTEASIWE FISADI

Ndugu zangu Watanzania popote mlipo tuchukue jukumu la kuitangaza Tanzania kama wenzetu wa TANDEN wanavyofanya, Tuwaumbue mabalozi wazembe bila woga wala kumuonea.

Kilimanjaro ni yetu, Kiswahili lugha yetu na Tanzania nchi yangu,

asante

Alipewa na nafasi hiyo na si mwingine bali fisadi Mkapa akiwa amebakisha miezi mitatu kumaliza awamu yake. Kisa 'wameoa nyumba moja' juhudi kama hizi za kuwapinga mabalozi wazembe na mafisadi labda zinaweza kuzaa matunda na hatimaye kuteuliwa mabalozi wenye uwezo tu, lakini hii serikali dhaifu iliyo madarakani sidhani kama inaweza kufanya lolote kwa sababu JMK anaogopa sana kuwagusa wote walioteuliwa na fisadi Mkapa sijui sababu kubwa ya hili ni kitu gani au ndiyo udhaifu na woga ja JMK.
 
Lakini suala la kujiuliza ni kuwa wanapoteuliwa wanapewa terms of reference zikiwa na majukumu gani?.....kuna evaluation yoyote inafanyika kila baada ya mwaka kujua balozi ametekelezaje majukumu yake?...manake tunaweza kuwalaumu wao kumbe hata mamlaka zinazowateua hazijui katika uchumi wa kisasa wa dunia mabalozi wanatakiwa wafanye nini.
 
deny_all,

umeuliza swali la msingi sana......Dr Ben Moses ni kati ya ma-PS wachache waliojijengea sifa sana katika uchapaji kazi.............sijui imekuwaje
 
deny_all,

umeuliza swali la msingi sana......Dr Ben Moses ni kati ya ma-PS wachache waliojijengea sifa sana katika uchapaji kazi.............sijui imekuwaje

Ogah

Sina uhakika na usemalo lakini jiulize ni kitu gani huyu bwana amekifanya kwenye huu ubalozi wa Sweden (scandivia and Baltic region). Kama ni kuorganise sisi wanaccm kwa kweli amefanya kazi maana tuko intouch nae kila mara kwa kila jambo na tunapata ushirikiano wa kutosha. Lakini je yupo kwa ajilia ya chama ama watanzania?????

Weekend hii nilijaribu kudodosa kwa msiri wake mmoja hapa DK, nilichogundua ni kwamba yeye hakuna ties kubwa na mheshimiwa, so alikua anajaribu kujikita mizizi kwenye chama ili profile yake iweze kupata support kutoka kwenye chama. Pili kama mnavyojua Katibu wake ni Mtoto wa makamu mwenyekiti Msekwa, amekuwa akimtumia pia kufikisha nia yake hiyo lakini inaonekana kugonga mwamba ndio maana amekuwa akifanya anayoyafanya.

Msiri huyo anasema tatizo lake jingine ni kukaa nje muda mrefu na kusahau hali halisi ya nyumbani na hata kuamini kwamba watanzania wa leo ni sawa na wale wa miaka ya 90s wa ndio mzee kila kitu.

kingine ni muoga ama mgumu wa kudelegate power kwa watu kufanya kazi hivyo kutaka kufanya kila kitu yeye mwenye mwishowe kushindwa kutekeleza ama kuchelewa kutekeleza. Katika yote ameshindwa kuwa karibu na watanzania waliopo kwenye nchi anazozisimamia, badala yake amekuwa akijihusha na makundi fulani fulani ambayo nayo yanachochea mgawanyiko wa watanzania waliopo katika nchi hizo.

Swali: Je ni jambo gani Dr. amelifanyia taifa ama watanzania waliopo Scandinavia na Baltic region watamkumbuka nalo??????

Jibu: Kwa sisi wa Denamrk ni hii hujuma sijui wa nchi nyingine watsema lipi.
 
Masatu Si udaku

Mimi ni mdau hapa Denmak kwanza namshukuru mdau aliyeweka hiyo post.
Aliyo sema ni kweli na nimewasiliana na viongozi wa TANDEN wamenihakikishia ni kweli aliyoandika huyo bwana ni kweli na kuna zaidi ya hilo ila kwa sababu si msemaji wa TANDEN na sio mwanachama nachelea kusema mengi zaidi.

Ni kweli Balozi alikuja hapa Copenhagen kwa mwaliko wa serikali ya hapa aje kuelezea vivutio vya uwekezaji Tanzania. kwa habari zaidi soma www.um.dk/da/menu/Udviklingspolitik...legationTilTanzaniaAfholdtDen13Og26August.htm
sorry maana ipo kwenye lugha ya kigeni hii kudhirisha kweli balozi alikuepo

Pia kuna dada niliongea naye siku ya part huyo dada anaorganise safari kwa wanaotaka kwenda kutalii nyumbani na yeye anatoa same complain.
kwa ujumla ubazo wetu sweden ni Kero hivyo kama kweli anaondoka basi akapumzike kwa amani.

bowbow
nashukuru kwa kufuatilia na soma ujumbe niliokutumia kwenye PM yako
 
Ogah

Sina uhakika na usemalo lakini jiulize ni kitu gani huyu bwana amekifanya kwenye huu ubalozi wa Sweden (scandivia and Baltic region). Kama ni kuorganise sisi wanaccm kwa kweli amefanya kazi maana tuko intouch nae kila mara kwa kila jambo na tunapata ushirikiano wa kutosha. Lakini je yupo kwa ajilia ya chama ama watanzania?????

Weekend hii nilijaribu kudodosa kwa msiri wake mmoja hapa DK, nilichogundua ni kwamba yeye hakuna ties kubwa na mheshimiwa, so alikua anajaribu kujikita mizizi kwenye chama ili profile yake iweze kupata support kutoka kwenye chama. Pili kama mnavyojua Katibu wake ni Mtoto wa makamu mwenyekiti Msekwa, amekuwa akimtumia pia kufikisha nia yake hiyo lakini inaonekana kugonga mwamba ndio maana amekuwa akifanya anayoyafanya.

Msiri huyo anasema tatizo lake jingine ni kukaa nje muda mrefu na kusahau hali halisi ya nyumbani na hata kuamini kwamba watanzania wa leo ni sawa na wale wa miaka ya 90s wa ndio mzee kila kitu.

kingine ni muoga ama mgumu wa kudelegate power kwa watu kufanya kazi hivyo kutaka kufanya kila kitu yeye mwenye mwishowe kushindwa kutekeleza ama kuchelewa kutekeleza. Katika yote ameshindwa kuwa karibu na watanzania waliopo kwenye nchi anazozisimamia, badala yake amekuwa akijihusha na makundi fulani fulani ambayo nayo yanachochea mgawanyiko wa watanzania waliopo katika nchi hizo.

Swali: Je ni jambo gani Dr. amelifanyia taifa ama watanzania waliopo Scandinavia na Baltic region watamkumbuka nalo??????

Jibu: Kwa sisi wa Denamrk ni hii hujuma sijui wa nchi nyingine watsema lipi.

kichakoro,

.......kwa kweli..............I personally understand your frustrations.....inaudhi sana kwa kweli.........it was very logic kwa Balozi na timu yake kuwaletea hivyo vitu mlivyoomba toka ubalozini..........ndio maana najiuliza hii commonsense........imekuwaje kwa Dk Ben Moses

NOTE: kama alivyosema deny_all hapo juu...............
 
Kuna tetesi nilizozipata hivi punde kuwa Dr. Moses sasa ameshakabidhi rasmi ofisi kwa aliyekuwa msaidizi(Bwana Msekwa) ambaye atakaimu office hadi balzi mpya atakapotangazwa.

Swali kwa Dr. Ben, Je kwa nini usichukue wasaa huu kuwashukuru na kuwaaga watanzania waliopo kwenye nchi za baltic na scandinavia kwa kuwatumikia ama
kuwashukuru kwa ushirikiano ulioupata kutoka kwao??????

Tafsiri yangu ya kushindwa kufanya hivyo ni kuwa labda hukuwa na ushirikiano nao
ama hukuwa unawatumikia wao bali......

Nakutakia kila la kheri kwa kile utakachokuwa unafanya baada ya kuwatunikia watanzania
kwa wakati wote ukiwa hapa Canada na huko scandinavia. Mapumziko mema
 
Ndugu wanabodi,

Tanzania sasa tunahujumiwa hata na balozi zetu, hii sasa inatisha kisa chenyewe kiko hivi.

Mimi ni Mtanzania ninaishi Denmark ingawa sio mwanachama rasmi wa umoja wa watanzania hapa Denmark (TANDEN). TANDEN ilifanya summer party 30.08.2008 lakini kawaida ya party zao huwa zinatanguliwa na mada za kuitangaza Tanzania na hasa utaliii kwani siku hiyo huwa inawaleta watu wa mataifa mbali mbali hivyo TANDEN hutumia wasaa huo kuitangaza nchi yetu of which is very good.

Aliyetoa mada kuhusu Tanzania kwa kweli alinigusa na alielezea kwa ufasaha vivutio vya Tanzania na hata girl friend wangu amehamasika kwenda Tanzania. Tulipomuomba mtoa mada kuhusu vipeperushi ambavyo mtu akitaka kusoma zaidi ndipo nilipogundua hujuma yenyewe. Maelezo yake ni kama ifuatavyo:

Ubalozi wa Tanzania Sweden kwanza uliombwa kuleta bronchure za kuitangaza Tanzania (Tanzania the Land of Kilimanjaro, Seringeti and Zanzibar) ambazo serikali imetumia gharama nyingi kuzichapisha na kisha kuzisambaza kwenye balozi zake zote.

Cha kushangaza kila waaandaji walipojaribu kuwasiliana na ubalozi waliambiwa zitakuja wasiwe na wasi wasi. Cha kusikitisha Zaidi baadae zikaja taarifa oooh ni gharama kuzisafirisha. wakati wanasema ni gharama balozi alikuja Denmark 25.08.2008 kwa ajili ya seminar ya kuwavutia wawekezaji wa kidanish kwenda kuwekeza Tanzania, Hakuleta hakutaka hata kuonana na watanzania waishio Denmark.

Ila alikuwa na nafasi ya kuonana na wanaCCM mimi nikiwa ni mmojawapo mike, Mzee msimbazi na wengine tuliokutana shame uponi you balozi. swali mtauliza hujuma iko wapi????

Moja serilkali imetumia gharama kuchapisha vipeperushi ili viwafikie watu na sio vikae kwenye maboksi kwenye ofisi za balozi hivyo hela za walipa kodi hazikutumika kama ilivyotarajiwa je balozi hajahujumu uchumi?????

Pili kama aliweza kuja hapa Denmark na delegation yake walishindwa hata kuja na vipeperushi ishirini ambavyo havifiki kilo moja wakati ni hela za walala hoi zimetumika kuwgharamia safari yao, sio hujumaa hiii????????

Kuna tetesi kwamba anaondoka ama anabadilishwa kituo, ila habari za uhakika nilizozipata ni kwamba anastaafishwa kwa manufaa ya UMMA, lakimi je kustaafishwa ama kuhama kituo kunakufanya mtu asitimize wajibu wake???? Je ndio aliamua kufanya retaliation kwa njia hiyo??????

Tunao mabalozi wengi wa aina Dr. Ben Moses sehemu nyingi ni muda wa kusema HATUWATAKI.

OMBI kwa ndugu Mh. Kikwete sasa umefika wakati wa balozi zifanye kazi kwa manufaa ya watanzania wote waishio nje na wale waliopo nchini. HIVYO MTU UTKAYEMLETA KAMA BALOZI SWEDEN HAKIKISHA NI MCHAPA KAZI, MZALENDO, MPENDA MAENDELEO, ANAYEPENDA KUTUMIKIA KULIKO KUTUMIKIWA, na ZAIDI YA YOTEASIWE FISADI

Ndugu zangu Watanzania popote mlipo tuchukue jukumu la kuitangaza Tanzania kama wenzetu wa TANDEN wanavyofanya, Tuwaumbue mabalozi wazembe bila woga wala kumuonea.

Kilimanjaro ni yetu, Kiswahili lugha yetu na Tanzania nchi yangu,

Mkuu Kichakoro,

Kwanza heshima mbele sana, hii kitu nilikuwa sijaiona kwa kweli inasikitisha sana, I promise kwamba hii post yako nitaifikisha kwa waziri Membe by Jumatatu.

Ahsante Mkuu.
 
Tafsiri yangu ya kushindwa kufanya hivyo ni kuwa labda hukuwa na ushirikiano nao ama hukuwa unawatumikia wao bali......

Nakutakia kila la kheri kwa kile utakachokuwa unafanya baada ya kuwatunikia watanzania kwa wakati wote ukiwa hapa Canada na huko scandinavia. Mapumziko mema

Kwa nini unauma na kupuliza ? Hivi Tanzania kwa nini tuna hii tabia ya kusujudia viongozi hata wanapovurunda ?

Wewe ukikutana njiani na huyo Balozi sijui utamchekea chekea na kumpongeza au utamkazia uso ? Wabongo tuache huku kujinyenyekeza kwa Wabukwa wasiotujali.

Huyu Balozi wa Sweden ana distinction ya kutajwa Bungeni na Waziri Kawambwa wa Miundombinu kwamba arudishe nyumba mbili za Serikali alizojinunulisha kinyume na utaratibu! Hana sifa nzuri huyu. Sasa huku "kumtakia mapumziko mema baada ya kututumikia" wakati ushasema inawezekana hakuwa anatutumikia sisi mimi sikubaliani nako.
 
kichakoro,

.......kwa kweli..............I personally understand your frustrations.....inaudhi sana kwa kweli.........it was very logic kwa Balozi na timu yake kuwaletea hivyo vitu mlivyoomba toka ubalozini..........ndio maana najiuliza hii commonsense........imekuwaje kwa Dk Ben Moses

NOTE: kama alivyosema deny_all hapo juu...............

common sense is very uncommon!
 
Hapa Tanzania ukijikomba kwa rahisi(I mean rais) unapewa ubalozi siku hiyo hiyo. Believe me.
 
Masatu Si udaku

Mimi ni mdau hapa Denmak kwanza namshukuru mdau aliyeweka hiyo post.
Aliyo sema ni kweli na nimewasiliana na viongozi wa TANDEN wamenihakikishia ni kweli aliyoandika huyo bwana ni kweli na kuna zaidi ya hilo ila kwa sababu si msemaji wa TANDEN na sio mwanachama nachelea kusema mengi zaidi.

Ni kweli Balozi alikuja hapa Copenhagen kwa mwaliko wa serikali ya hapa aje kuelezea vivutio vya uwekezaji Tanzania. kwa habari zaidi soma Informationsmøder om Erhvervsdelegation til Tanzania afholdt den 13. og 26. august - Udenrigsministeriet
sorry maana ipo kwenye lugha ya kigeni hii kudhirisha kweli balozi alikuepo

Pia kuna dada niliongea naye siku ya part huyo dada anaorganise safari kwa wanaotaka kwenda kutalii nyumbani na yeye anatoa same complain.
kwa ujumla ubazo wetu sweden ni Kero hivyo kama kweli anaondoka basi akapumzike kwa amani.

Nyinhyi watu wa Denmark mmezidi sana uswahili. kama kuna balozi anayewajibika katika historia ya ubalozi wetu Sweden basi ni huyu mzee Ben Moses. Kama kuna Mtanzania ambaye hajawahi kumuona huyu mzee akiwajibika, basi huyo Mbongo anakimbia yeye mweneye, huyu mzee ni bingwa wa kutafuta watu wake na kuwasaidia kwa kadiri anavyoweza. Hapa Finland kwa kweli tunajivunia sana kuwa na balozi wa aina yake na tunampa bravoooooooo.
 
Kwa nini unauma na kupuliza ? Hivi Tanzania kwa nini tuna hii tabia ya kusujudia viongozi hata wanapovurunda ?

Wewe ukikutana njiani na huyo Balozi sijui utamchekea chekea na kumpongeza au utamkazia uso ? Wabongo tuache huku kujinyenyekeza kwa Wabukwa wasiotujali.

Huyu Balozi wa Sweden ana distinction ya kutajwa Bungeni na Waziri Kawambwa wa Miundombinu kwamba arudishe nyumba mbili za Serikali alizojinunulisha kinyume na utaratibu! Hana sifa nzuri huyu. Sasa huku "kumtakia mapumziko mema baada ya kututumikia" wakati ushasema inawezekana hakuwa anatutumikia sisi mimi sikubaliani nako.


Acheni unafiki, majina ya waliojiuzia nyumba wametajwa na Ben Moses sio mmojawao, tafuteni jungu lingine.
 
Mkuu Bob,

Huyu balozi aliwahi kuwepo huko kwako mkuu, wewe ninakuaminia sana tuweke sawa hapa kuhusu record ya huyu balozi alipokuwa huko,

maana naona yale yale ya chuki, ukabila na undugu yameshaanza hapa!
 
Acheni unafiki, majina ya waliojiuzia nyumba wametajwa na Ben Moses sio mmojawao, tafuteni jungu lingine.

Hakuna unafiki ni kweli Balozi Ben Boses na Dr Edna Moses "walinunua" nyumba 2 wakati utaratibu ni familia moja nyumba moja kama kiambatanisho hapo chini;

Mwandishi Wetu, Dodoma
Daily News; Saturday,August 30, 2008 @10:38

SERIKALI imeagiza kufutwa kwa mikataba na kurudishwa kwa nyumba kadhaa ilizowauzia maofisa wake waandamizi na watu binafsi, baada ya kubainika kwamba waliuziwa kinyume cha sheria au katika sehemu zisizostahili, ilifahamika bungeni jana.

Imebainika pia kwamba Waziri mmoja mstaafu, Jaji na balozi mmoja waliuziwa nyumba ambazo si za Serikali Kuu na sasa itabidi zijengwe mpya na kufidiwa kwa wamiliki wa awali.

Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa, aliliambia hayo Bunge jana kuhusu utekelezaji wa Maazimio ya Bunge la Uuzaji wa Nyumba za Serikali yaliyotokana na hoja binafsi iliyowasilishwa na Aloyce Kimaro (Vunjo-CCM), Aprili mwaka huu.

Katika maazimio hayo, wabunge walitaka serikali itekeleze agizo la Rais la kurejesha nyumba zilizouzwa kinyume cha utaratibu; itoe orodha ya nyumba zilizouzwa kwa watu ambao si watumishi wa serikali na ambazo hazikupaswa kuuzwa kutokana na unyeti wa wanaostahili kuzitumia.

Katika kueleza namna serikali ilivyotekeleza maazimio hayo, Waziri Kawambwa aliwaambia wabunge kwamba imebainika kuwa kuna makundi matano ya nyumba za serikali zilizouzwa kinyume cha taratibu ambazo ni zilizoko kwenye makambi; zilizouzwa kwa watu binafsi na nyumba zaidi ya moja zilizouzwa kwa familia moja.

Nyingine ni nyumba za taasisi mbalimbali zilizouzwa kwa watumishi wa Serikali Kuu na ambazo ziko katika maeneo nyeti zilizouzwa kwa watumishi wa umma.

Kwa mujibu wa Kawambwa nyumba 52 ziliuzwa kwa makosa katika makambi, kati yake nane ziko katika makambi wa Polisi, 10 katika makambi ya Magereza na 34 katika maeneo ya hospitali.

Alisema Serikali inakagua na kutathmini maendeleo yaliyofanywa kwa lengo la kupata thamani halisi zitakazokuwa msingi wa kuwafidia wahusika.

Juu ya nyumba za taasisi mbalimbali zilizouzwa, Waziri Kawambwa alisema zilifikia 27, zikiwamo 21 za Serikali za Mitaa, mbili za Shirika la Viwanda Vidogo (Sido), moja ya Mamlaka ya Mapato (TRA) na tatu za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Waziri Kawambwa alisema serikali itajenga nyumba mbadala kufidia nyumba zilizouzwa.

Miongoni wa waliouziwa nyumba hizo kwa mujibu wa kiambatanisho kilichowasilishwa bungeni, ni Waziri mstaafu Bakari Mwapachu, Jaji Stephen Ihema na Balozi Adam Marwa. Hao waliuziwa nyumba za Serikali za Mitaa.

Dk. Kawambwa aliwaambia wabunge kwamba nyumba nne ziliuzwa kwa makosa kwa watu ambao si watumishi wa serikali mjini Dar es Salaam baada ya kutoa taarifa zisizo sahihi. Alisema serikali imefuta mikataba ya mauzo ya nyumba tatu kati ya hizo na moja mhusika amefungua kesi mahakamani.

Kwa mujibu wa viambatanisho vilivyowasilishwa bungeni, miongoni mwa waliouziwa nyumba hizo ni Esther Chilambo katika eneo la Karume; Monica Senga katika eneo la Upanga, Mussa Joseph na Stanley Manongi, wote katika eneo la Ubungo Camp.

Kuhusu familia sita na watumishi wanne waliouziwa nyumba zaidi ya moja, alisema familia tano zimerudisha nyumba tano na kubakiwa na tano wakati watumishi hao wanne wamepewa hadi Septemba 15 kurejesha nyumba ya ziada vinginevyo serikali itafuta mkataba wa nyumba mojawapo.

Kiambatanisho kinaonyesha wahusika walikuwa familia ya Balozi Ben Moses na Dk. Edna Moses (Mambo ya Nje na Afya); Hussein Abdulrahman na Mwanamtama Marandu (Shirika la Reli na Elimu), Emil Kayega na Emerensiana Kayega (Ofisi ya Makamu wa Rais na Ardhi na Makazi), Clement na Esther Mshana (TVT na RTD).


Wengine ni Dk. Mollel Jacob na Theodora Mollel (Mifugo na Ofisi ya Rais Utumishi) na Ngore Kondo na Zainab Kondo (Ofisi ya Rais).

Watumishi waliouziwa nyumba mbili ni Dk. Edna Moses wa Afya, Veronica Mabula wa Bohari Kuu (Mwanza), Sweetbert Bajuza wa DAS (Karagwe) na Agnes Chamshama wa Halmashauri ya Wilaya Lushoto.

Alibainisha zaidi kuwa nyumba 35 zilizouzwa katika maeneo nyeti waliouziwa wameandikiwa barua za kusimamisha mikataba na kuzirejesha serikalini.

Takwimu zilizowasilishwa na Waziri Kawambwa kwa Bunge zinaonyesha kuwa hadi Juni mwaka huu serikali ilikuwa imeuza nyumba 7,159 na ilikuwa imepata Sh bilioni 38.6 kutokana na mauzo hayo kati ya lengo la Sh bilioni 57.

Source: Habari Leo
 
Back
Top Bottom