Huduma za Matibabu Hospitalini

O-man

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
323
65
Nimepata tetesi kwamba Hospitali ya Temeke kuna kijipu uchungu kinahitaji tiba ya haraka kabla hakijageuka kuwa tambazi. Ipo wadi moja (Wadi namba 4) ambayo mgonjwa wako akilazwa humo basi anza kufanya mipango ya mazishi. Nikahoji, kulikoni na kuambiwa kwamba mgonjwa akiingizwa humo hapati aina yoyote ya tiba na wala hakuna uangalizi wa daktari wala wahudumu. Mwenye taarifa zaidi hebu tujuze.
 
Kweli inachekesha? Sidhani. Ipo habari pia (wiki iliyopita) ya mtu aliyepata bahati mbaya ya kulazwa humo na kukuta wagonjwa wengine sita au saba na siku iliyofuata akabaki yeye tu! Aliomba ndugu zake wamrudishe nyumbani akaugulie huko. Sijadhibitisha lakini naliafanyia kazi. Nitawajuza soon.
 
Back
Top Bottom