Prince Chapee
Senior Member
- Jul 31, 2017
- 179
- 126
Hospitali hii imekuwa ya ndugu wa madaktari, manesi na washkaji zao..
Tangu afe Magufuli huduma za hospitali Rufaa Mkoa wa Ruvuma zinatolewa kwa kujuana sana, ndugu wa watoa huduma hospitalini madaktari na manesi pamoja na washkaji zao wao kwa wao wanaingia na kutoka sisi wengine tumekaa tu kwenye mabenchi tukisubiri wamalize kuhudumiana.
Kama huna ndugu anayefanya kazi hospitali hii utasubiri sana kupata huduma.
Ukiwa na mkono mfupi bila kuwapa buku tano tano manesi fomu zako ziteleze bila vikwazo vya maskini wenzako waliopo kwenye foleni utasubiri sana.
Nimeandika kwa jazba tu, mimi siyo mwandishi wa habari.
Ofisi za malalamiko na zenyewe ni "malalamiko" hazina msaada wowote unaweza ukafa ukisubiri kuhudumiwa.
Ushauri wangu, nendeni na pesa hospitalini ili mpate angalau nafasi ya pili.
=============
UPDATES...
MAJIBU YA HOSPITALI
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Ruvuma, Dkt. Charles Hinju anafafanua:
Kwa kawaida katika Taasisi yetu kuna maelekezo ya kutoa maoni kuuhusu Hospitalini hao, Wananchi wapo huru kwa kuwa ni Taasisi ya Umma, upande mwingine kuna Kamati inayosimamia ubora wa huduma zinazotolewa.
Hospitali ina vitengo vingi, labda huyo Mdau angefafanua ni sehemu gani alipokutana na changamoto hiyo ili iwe rahisi kutolea ufafanuzi.
Pamoja na hivyo kuna watu wanaosema vibaya kuhusu Hospitali ya Mkoa lakini wakati huohuo wengine wanatuma ujumbe wa kushuruku kwa kupata huduma nzuri.
Ningependa kuwaona watu wanaolalamika kuhusu huduma zetu, wakipata nafasi waje watueleza kwa kuwa uongozi wetu umekuwa ukisisitiza utoaji wa huduma bora.
Pamoja na hivyo, napokea maoni hayo, nitayafikisha kwenye uongozi ili tujipime tuone iwapo wapo kuna upungufu wowote na tuweze kuufanyia kazi.
Tangu afe Magufuli huduma za hospitali Rufaa Mkoa wa Ruvuma zinatolewa kwa kujuana sana, ndugu wa watoa huduma hospitalini madaktari na manesi pamoja na washkaji zao wao kwa wao wanaingia na kutoka sisi wengine tumekaa tu kwenye mabenchi tukisubiri wamalize kuhudumiana.
Kama huna ndugu anayefanya kazi hospitali hii utasubiri sana kupata huduma.
Ukiwa na mkono mfupi bila kuwapa buku tano tano manesi fomu zako ziteleze bila vikwazo vya maskini wenzako waliopo kwenye foleni utasubiri sana.
Nimeandika kwa jazba tu, mimi siyo mwandishi wa habari.
Ofisi za malalamiko na zenyewe ni "malalamiko" hazina msaada wowote unaweza ukafa ukisubiri kuhudumiwa.
Ushauri wangu, nendeni na pesa hospitalini ili mpate angalau nafasi ya pili.
=============
UPDATES...
MAJIBU YA HOSPITALI
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Ruvuma, Dkt. Charles Hinju anafafanua:
Kwa kawaida katika Taasisi yetu kuna maelekezo ya kutoa maoni kuuhusu Hospitalini hao, Wananchi wapo huru kwa kuwa ni Taasisi ya Umma, upande mwingine kuna Kamati inayosimamia ubora wa huduma zinazotolewa.
Hospitali ina vitengo vingi, labda huyo Mdau angefafanua ni sehemu gani alipokutana na changamoto hiyo ili iwe rahisi kutolea ufafanuzi.
Pamoja na hivyo kuna watu wanaosema vibaya kuhusu Hospitali ya Mkoa lakini wakati huohuo wengine wanatuma ujumbe wa kushuruku kwa kupata huduma nzuri.
Ningependa kuwaona watu wanaolalamika kuhusu huduma zetu, wakipata nafasi waje watueleza kwa kuwa uongozi wetu umekuwa ukisisitiza utoaji wa huduma bora.
Pamoja na hivyo, napokea maoni hayo, nitayafikisha kwenye uongozi ili tujipime tuone iwapo wapo kuna upungufu wowote na tuweze kuufanyia kazi.