Hoja ya Moto: Hakuna dharau mbaya kama ya kudharauliwa akili

Tumedanganywa mengi. Kwanza walikuja na Tanzania yenye neema kwa kila mmoja inawezekana. Wakatupigisha wimbo wa maisha bora kwa kila mtanzania! Wakatudanganya kuhusu EPA, DOWANS NA RICHMOND! Mpaka leo tunadanganywa kuhusu meremeta! Naam, wakatudanganya kiwira. Wakatudanganya kuwa matatizo ya nchi yetu yanasababishwa na kuyumba kwa uchumi wa dunia. Mara ni kupanda kwa bei ya mafuta. Tena mkulu akatudanganya kuwa hajui kwanini sisi ni maskini. Akatudanganya na kilimo kwanza. Akatudanganya kwa mbwembwe za mpango wa miaka mitano. Loh, mengi kweli! Hata kigoma kuwa Dubai ya Afrika tumedanganywa! Na sasa hii sinema ya Kova na Joshua wake! Loh! Kweli dhaifu! Sasa tatizo si la wadanganyaji bali wadanganywaji! Hata lini itakuwa hivi? Chukua hatua, liwalo na liwe!
 
Ni nani sasa wakutuondoa kwenye hii fear? Nani atupe Ujasiri? Je ni sera? Sheria? Au Katiba mpya? Tumechoka Na hii fear, tunahitaji kutoka Na kuokolewa. Hata maandiko matakatifu yanasema waoga wote hawatauona ufalme wa Mbingu.

ni jitihada za taasisi tofauti kuanzia katika ngazi ya familia ,mifumo ya elimu na imani zetu itujenge tuwe wa kuthubutu na kuhoji na kupigania haki.
mifumo yetu ya sasa imetulea kuogopa utawala si kuuliza au kutaka kitu fulani kifanyike.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom