Mbase1970
JF-Expert Member
- Jun 11, 2015
- 6,053
- 4,595
WanaJF,
Wanasema waswahili kuwa hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Huu msemo umejidhihirisha kwa Lowassa ambae amekuwa akitajwa kuwa ni moja ya watu matajiri Tanzania.
Utajiri huo wa Lowassa ambao wengi wanaamini ni wa magendo na dili za kuibia wananchi wa Tanzania, umeanza kupata mabalaa na kuhofiwa kupotea kabisa kabla ya sherehe za pasaka!
Wengi mnafahamu kuwa kampuni ya Alpha Dry Cleaners inamilikiwa na Lowassa na moja ya ofisi zao ipo PPF Tower kwenye basement. Kampuni hii ndio imekuwa chanzo kikuu cha mapato kwa Lowassa tangu atimuliwe kwenye nafasi ya uwaziri mkuu kwa kashfa ya ufisadi wa RICHMOND.
Taarifa zinasema kampuni hiyo ambayo sasa ndio uti wa mgongo wa Lowassa, imeanza kushindwa kujiendesha; Kwanza wafanyakazi wake hawajapata mshahara kwa miezi miwili hadi sasa na pili, kodi ya pango ambayo ilikwisha mwezi novemba, hadi leo haijalipwa kinyume kabisa na mkataba wa upangishaji. Hali hii imepelekea kampuni hiyo kupewa notisi ya siku 30 kufunga virago na kutoka kwenye jengo la PPF.
Aidha, taarifa zinasema kuwa mtikisiko huo wa biashara hiyo ya Lowassa, pamoja na mambo mengine, umetokana na kuchotwa kwa pesa nyingi ya kampuni hiyo na kutumika kwenye kugharamia uchaguzi wa urais...Maamuzi ambayo wafanyakazi wa kampuni na wadau wengine wanaamini yamehatarisha uhai wa kampuni hiyo kongwe inayojihusisha na ufuaji hapa nchini.
My take,
Kwanza nianze kwa kumpa pole mzee Lowassa kwa matatizo, lakini pia niseme: Huu ndio wakati wa kupima urafiki wa Mbowe na Lowassa. Natarajia kuona Mbowe anatumia sehemu ya lile fungu alilotorosha Uswizi na China (Pesa ya kuuza chama) kumsaidia Lowassa kulipa kodi ya pango na malimbikizo yote kwa maana notisi imetolea ya siku 30 tu.
Mtoa mada nakuonea huruma huyo uliyemgusa kuanzia mwaka jana ni Mungu mtu hivyo jiandae kutukanwa. Ukitaka kuupamba huu ukurasa msifie Lowasa kashifu JPM ama wa Msoga utapata like nyingi. Watu hawajadili mada wanatukana ili mradi anayejadiliwa si wa upande anaoupenda. MUNGU IBARIKI TANZANIA MAANA HATA TULIOWAJUA KUWA MA GREAT THINKERS WAMEKUWA NYUMBU SABABU YA MAPENZI YA KICHAMA SIYO TENA MAMA TANZANIA. LUCK DUBE ALISEMA "There is no truth in the world. Lies become true and truth becomes lies.