Hizi sio ndoto za kawaida

Habari,ni Mara ya kwanza kukuona nimefurahi kwakuwa ktk watu wanaoongoza kwa kuota nahisi naongoza duniani:Nina maswali Mengi ambayo sijawahi kupata ufumbuzi:kwa Leo naomba nisaodie kutafsiri hii ndoto:kuna siku niliota nipo shule ya msingi ambayo nilisoma miaka mingi sana,nipo kwenye uwanja Fulani hv sasa ghafla nikamuona Simba dume nikaogopa sana,nikajitengenezea fensi zile za seng'enge haraka nikawa ndani ya fensi Simba nje,ghafla àkaja Mdogo wangu wa kiume ameshikilia bahasha ya kaki mkononi akaruka fensi akaingia ndani,nikashangaa amepitaje huko nje wkt kuna Simba?
Wkt nashangaa Mara nikamuona yule Simba nae kaingia ndani ya fensi bila kujua kapitia wapi,basi akaanza kutukimbiza tulikimbia sana huku namwambia Mdogo wangu akazane ni heri Simba anile Mimi lkn asimle yeye.nikashtuka ghafla.kuangalia saa ilikuwa SAA 8 usiku.je maana Yake nini hyo ndoto?

Mkuu Mshana Jr Heshima yako chief.

Nimeota usiku wa kuamkia majuzi (wiki hii hii),..Ni Mara ya tatu kama sio ya pili.
Nilianza kwenda na jamaa mahali (sura simfahamu) tukaelekea poroni kama vile kuna kitu tunaenda kukufuata tulikua na piki piki.Gafla likatokea basi Moja ivi likasimamishwa na wanajeshi wakasema Luna jambazi humo mpo chini ya linzi Mimi nilikua Katibu na basi hilo nikajitupia kwenye mitaro hii ya pembeni ya Barbara",.. Mmoja wa wale wanajeshi wakiwa wanatangisha basi akaniona akaanza kunilenga kwa risasi,.. nikainua mkono kuashiria sins kosa ila alizidi kunimiminia risasi hizo (nilikua sijeruhiki) hakuna aliyenitetea hata kwa kusikitika huku nafsi ikijawa na hofu na maumivu,..

Nikaona nisimame akanilenga za kichwa (bado nilikua sijeruhiki) Punde baada ya risasi hizo likatokea gari Moja likanibeba kunipeleka mbali (walionibeba hata siwafahamu) tukaenda mbali gafla wakatokea wengine wakimsaka mtu wao ila wakiniona mm wananitaka, kutokana na wale watu wakawa wananiacha,.. ivo ivo kwenye barrier zingine adi nikavuka nikaenda sehemu salama nikashuka nikiwa na furaha kwa kiasi chake.
Sijui itakua INA maana yoyote maana nimeota Mara ya tatu hivo hivo bila kubadilika kitu.
Hizi ndoto zenu wote zinaashiria kitu kimoja! Mapambano ya kiroho katika ulimwengu wa giza
Hiyo ya shule ya msingi ni dalili kwamba mapambano hayo ni ya siku nyingi
Na hii ya ugenini ni kwamba tayari kuna kitu kibaya kilikuwa kinakuandama ndio maana hata mfanyakazi mwenzako akaota umekufa
Ndoto mara nyingi huwezi kupata tafsiri yake halisi bali ni kwa ujumla wake tu kutokana na viashiria vya ndoto husika
Hizi ndoto za kujirudia rudia ndio hizi tunazoita ndoto maono au taarifa, ni ufahamu wako unajaribu kukupa warning fulani...unaota unagongwa na gari lakini huumii ukifika kesho yake kazini unanusurika kuanguka kwenye ngazi nk
Ndoto za mapambano halafu huku unaibuka mshindi, ni mapambano na vita vya nguvu za giza lakini Zikiwa zinakushindwa hasa kama zikiendelea kujirudia kwamba mapambano hayo bado yanaendelea
Ni vema na ni muhimu ukiota ndoto za kujirudia rudia siku inayofuata ujaribu kuwa makini kwa kinachokutokea kisha linganisha na ndoto husika utagundua mengi ya kushangaza sana
 
Naweza kuwa na majibu yasoyikidhi maswali ya wengi au hata kuwa na makosa madogo madogo kwenye kujibu! Kwa msaada zaidi na kwa wale watakaopenda kujifunza siri na tafsiri ya ndoto kwa undani kitabu hiki hapa
1477104800208.jpg
Kwa mfano baada ya kupitia links nyingine tofauti tofauti hasa kuhusiana na ndoto za nyoka ni kwamba ndoto hizo huashiria maisha marefu ya muotaji, lakini ni tofauti na kuumwa na nyoka, hizo ni ndoto za kufukuzwa kuzungukwa ama kukutana na nyoka
 
Kuna siku niliota tuko maeneo kama ya shuleni hivi
Niko na jamaa wawili ninaowafahamu kabisa mmoja wao alikuwa anapika nyama za watu na akawa anatupa tunakula
Ilikuwa inamaanisha nini?
 
Na ndoto ya kuota uko darasani unasoma tena uko sekondari wakati ulishapita muda mrefu hiyo level inamaana gani nayo?
 
Na ndoto ya kuota uko darasani unasoma tena uko sekondari wakati ulishapita muda mrefu hiyo level inamaana gani nayo?
Hizi ni ndoto kumbukizi tu zilizobaki kwenye ufahamu zinajirudia
 
Kuna siku niliota tuko maeneo kama ya shuleni hivi
Niko na jamaa wawili ninaowafahamu kabisa mmoja wao alikuwa anapika nyama za watu na akawa anatupa tunakula
Ilikuwa inamaanisha nini?
Hili la kula ama kulishwa Maranyingi huhusiana na nguvu za giza na mambo ya kishirikina na huyo uliyemuona kama ni rafiki yako ni mtu tu kaamua kuvaa sura yake
 
Asee mkuu Mimi kila usiku lazima niote moments za shule ya msingi wakati mwaka wa pili huu sijakamata daftari ila usiku ndotoni nipo zangu primary afu walimu kila siku wanabadilika Mara walionifundisha O'level au A'level . hii sijui nini maana yake
Hali ikoje kwenye career yako mkuu?
 
Hizi ndoto zenu wote zinaashiria kitu kimoja! Mapambano ya kiroho katika ulimwengu wa giza
Hiyo ya shule ya msingi ni dalili kwamba mapambano hayo ni ya siku nyingi
Na hii ya ugenini ni kwamba tayari kuna kitu kibaya kilikuwa kinakuandama ndio maana hata mfanyakazi mwenzako akaota umekufa
Ndoto mara nyingi huwezi kupata tafsiri yake halisi bali ni kwa ujumla wake tu kutokana na viashiria vya ndoto husika
Hizi ndoto za kujirudia rudia ndio hizi tunazoita ndoto maono au taarifa, ni ufahamu wako unajaribu kukupa warning fulani...unaota unagongwa na gari lakini huumii ukifika kesho yake kazini unanusurika kuanguka kwenye ngazi nk
Ndoto za mapambano halafu huku unaibuka mshindi, ni mapambano na vita vya nguvu za giza lakini Zikiwa zinakushindwa hasa kama zikiendelea kujirudia kwamba mapambano hayo bado yanaendelea
Ni vema na ni muhimu ukiota ndoto za kujirudia rudia siku inayofuata ujaribu kuwa makini kwa kinachokutokea kisha linganisha na ndoto husika utagundua mengi ya kushangaza sana
Asante sana
 
Anguko gani mkuu
Career ya kielimu au ipi?
Nipo na biashara tu ila msomi
Nimeuliza hvyo mana wengi wanao ota hzo ndoto kama ndo ametoka chuo kupata kazi ni shida sana hata aliye kazini mara nyingi mambo huwa hayaendi kuna mtu aliwahi nambia ukiota hvyo ujue tayari watu (ulimwengu wa giza) washafanya yao kwenye Career yako
 
Nimeuliza hvyo mana wengi wanao ota hzo ndoto kama ndo ametoka chuo kupata kazi ni shida sana hata aliye kazini mara nyingi mambo huwa hayaendi kuna mtu aliwahi nambia ukiota hvyo ujue tayari watu (ulimwengu wa giza) washafanya yao kwenye Career yako
Mkuu labda hii inawezekana
Maana biashara imekuwa ngumu
 
View attachment 421080Ni usiku mwingine tena tunapojiandaa kupumzika vitandani mwetu ( hata kama ni ugenini gesti house au barabarani kuna dakika chache utalala kidogo na kuota)
Ndoto njozi na kuota ni hitaji la kawaida la mwanadamu, shida ipo ni je unaona ndoto za aina gani?

-unaota ndoto za kawaida kutokana na harakati za kawaida za kimaisha kutokana na fikra mawazo matendo na maono?

-Ama la unaota ndoto taarifa au ndoto ujumbe au ndoto maono? Ndoto zenye ujumbe maalum?

- Au je unaota zile ndoto zile ambazo si ndoto bali ni matendo ya giza? Ndoto za
Kuota umelazwa kwenye jeneza
Kuota unazama/unazamishwa baharini
Kuota unakula/unalishwa nyama

Kuota unang'atwa na mdudu na unapata maumivu mpaka asubuhi
Kuota unakimbizwa au kufukuzwa
Kuota umefungiwa kwenye kiota chupa nk
Ndoto zote hizi huwa live mpaka asubuhi au unapostuka na unakumbuka kila kitu saa nyingine hata uchovu maumivu na Ladha....!

Ndoto za namna hii si ndoto za kawaida na huambatana na mambo yako mengi kuharibika! Hizi ni ndoto za kufanyiwa mambo mabaya na watu wabaya
Ukiweza jitahidi kuchunguza ndoto zako leo na siku zijazo utagundua kitu View attachment 421088
Kuna siku tena nimeota shule hiyohiyo ya msingi nlosoma miaka mingi sana,mmoja wa aliekuwaga mwl mkuu kipindi hichoo.eti ananikimbiaza vibaya sana huku akiwa amevaa suti, nilikmbia sana kuizunguka shule na yeye yupo nyuma ananikimbiza sana.nilipokaribia upande wa pili wa shule nilimkamata nilimbamiza ukutani kikasikika kishindo kama mtu kagongwa na gari lililokuwa speed.alibiringita karibia Mara Tatu kwa kile kishindo nikajua nimeua.half nkaamka.nayo maana Yake nini?
 
Kuna siku tena nimeota shule hiyohiyo ya msingi nlosoma miaka mingi sana,mmoja wa aliekuwaga mwl mkuu kipindi hichoo.eti ananikimbiaza vibaya sana huku akiwa amevaa suti, nilikmbia sana kuizunguka shule na yeye yupo nyuma ananikimbiza sana.nilipokaribia upande wa pili wa shule nilimkamata nilimbamiza ukutani kikasikika kishindo kama mtu kagongwa na gari lililokuwa speed.alibiringita karibia Mara Tatu kwa kile kishindo nikajua nimeua.half nkaamka.nayo maana Yake nini?
Mmh hii ni mkusanyiko wa kumbukumbu tu za maisha ya shule mawazo yanagongana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom