Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,794
Ndoto njozi na kuota ni hitaji la kawaida la mwanadamu, shida ipo ni je unaona ndoto za aina gani?
- unaota ndoto za kawaida kutokana na harakati za kawaida za kimaisha kutokana na fikra mawazo matendo na maono?
- Ama la unaota ndoto taarifa au ndoto ujumbe au ndoto maono? Ndoto zenye ujumbe maalum?
- Au je unaota zile ndoto zile ambazo si ndoto bali ni matendo ya giza? Ndoto za
Kuota umelazwa kwenye jeneza
Kuota unazama/unazamishwa baharini
Kuota unakula/unalishwa nyama
Kuota unang'atwa na mdudu na unapata maumivu mpaka asubuhi
Kuota unakimbizwa au kufukuzwa
Kuota umefungiwa kwenye kiota chupa nk
Ndoto zote hizi huwa live mpaka asubuhi au unapostuka na unakumbuka kila kitu saa nyingine hata uchovu maumivu na Ladha....!
Ndoto za namna hii si ndoto za kawaida na huambatana na mambo yako mengi kuharibika! Hizi ni ndoto za kufanyiwa mambo mabaya na watu wabaya
Ukiweza jitahidi kuchunguza ndoto zako leo na siku zijazo utagundua kitu