Hizi familia hizi zina mengi mazito.

Khs salama ya dogo bs niseme nilikosea hayo mengne unayoisema ni kwasababu hayajakukuta Tu Mzee kweli tena kuna watu ni pasua kichwa.
Kuhusu ulalamishi Kwa taarifa yako sinaga muda wa kulalamikia mtu hata SKU moja mi nilishaamua kufanya maisha yangu sina chuki na mtu aisee.
Umeleta ishu yako huku ili upate ushauri, Sasa acha kubishana , wewe chukua chenye kukufaa kisichofaa Baki nacho kumtima.
Kwa namna yako ngumu sana kujitambua.
 
Ndugu yangu ndugu yangu ndugu yangu.
Kama ni kufa hata wao wanaweza tangulia nikalea watoto wao.
Kama marafiki ninao ndani ya ukoo tena wengne ni haohao adui zangu wananikubali na ushahidi ninao kwamba wananikubali hata lilitokea tukio la wanaukoo lazma waniulzie kama nipo au sjafka pale haijalishi wengne nao hawajafka.

We jidanganye tu.

Nakazia "Kiburi si maungwana. "
 
Pole sana jamaa, fanya hivi tafuta namna uwe unawatumia hela kidogo ya matumizi. Kila ukipata tuma. Maana mamdogo wako alihisi wewe unamaliza chakula cha home. Chuki nyingi katika familia huanzia kwenye pesa.
 
Mkoa siwezi sema mkuu si unajua. Ila nipo kanda ya ziwa.
Kutonikubali kwao ilikuwa kimaslahi Tu maana Mzee alikuwa njema kiuchumi kuliko ndugu zake wote na walikuwa wanamtegemea Sana sa alipoanza hamishia nguvu kwangu na Mimi nilivyokuwa najaribu kuangalia sn maslahi ya familia Kwanza kuliko wengne ikaanza kuwapa shida ndugu WA Mzee ukizngatia hao akina aunt ndo wakimpindua mama na kufanya house awe mama mwny nyumba.
Kuhusu ma mdogo nadhan hofu yake ilikuwa endapo taendelea kushika hatamu Kwa Mzee uwenda swala la Maza kupinduliwa ningeliibua ikampa shida sn pale kwenye mji wake ikabd awe upande WA WiFi zake wanipindue kama walivyompindua maza
mkuu tafuta pesa,, ka wamekuona hufai na ww waone hivyo hivyo!!kwanza kaa mbali nao na wasijuwe ulipo wala mawasiliano yyte yale futa, kama kweli huna kosa kama ulieleza hapa sion haja ya kuomba msamaha mtu kwa kosa usilolijua,, tafuta pesa omba Mungu wako hakika utafanikiwa ipo sikj watakutafta wenyewe ila usisite kuleta mrejesho,,,
 
tayari NPO mkoa mwngn kbs na hawajui nipo mkoa upi kikazi na namba zangu hawana Ila kuna dogo mmoja upande WA ma mdogo ni WA kike ananikubali kinyama yaani hata nikipotea vp atapambana mpk anipate uzuri Naye hamkubali Mzee wala shangaz zake. Na anajua fika sina shida na mama ake Ila wabaya ni kina shangazi huyu ndo huwa kidogo tunawasiliana Sana pia yupo dogo WA aunt yng ndiye kufa na kuzkana maana misimamo yetu inaendana kuhusu ndugu.
tatu Nina marafiki zangu wawili hao ni zaidi ya ndugu kbs nilisoma nao advance na chuo mmoja ni pastor mwngn ni advocate sjawahi pata shida hata kidogo wasje aisee.
"Kikulacho kinguoni mwako"
"Umdhanie ndie kumbe sie"
 
Mimi kwa mzee nimetoka Kikwete akigombea awamu ya kwanza. Nilipatembelea tena mwaka 2011 na sijarudi tena. Leo hii sipakumbuki, naweza kwenda endapo tu mke wake atakuwa safari ya mbali. Mambo ya kuhatarisha usalama wangu sitaki
mm nakushaul wala usiende kabisa delete them..utakufa mkuu siku s zako
 
Khs salama ya dogo bs niseme nilikosea hayo mengne unayoisema ni kwasababu hayajakukuta Tu Mzee kweli tena kuna watu ni pasua kichwa.
Kuhusu ulalamishi Kwa taarifa yako sinaga muda wa kulalamikia mtu hata SKU moja mi nilishaamua kufanya maisha yangu sina chuki na mtu aisee.
Ww endelea na maisha yako ,,,mtoa laana ni Mungu ,,kama kweli hujawahi mkosea Mzee ,,,Alishakuzaa kaz yake kamaliza ,,,Ndg ni Masnitch sana,,,
 
Hiki ulichokisema kwamba madogo ni mzgo wangu wewe si WA Kwanza kusema aisee.
Pili khs Mzee kuja kunitafutia pia si WA Kwanza kusema hata wale adui zangu nao huwa napata taarifa zao kwamba huwa wanasema Mzee atanitafutaga Tu.
Nimeishi na mdogo wangu (mtoto wa mjombawangu)toka mwaka 2007 akiwa kafukuzwa kwao kisa kasababisha shot ya umeme na kuharibu vifaa vingi vya umeme ndani. Dada ake (mama angu)akajaribu kumuombea msamaha akakataa. 2008 wakakaa kikao cha familia uncle akamsamehe dogo lakini kwa kuwa tayari mjomba ana negative attitude juu dogo ikawa kila dogo akifanya mistakes ndogo ndogo uncle anazikuza na kuwa story kila kona. Hivyo dogo akakosa amani na akawa ana muda mchache wakujisomea so hata performance yake school ikapungua. Siku moja nikampitia dogo tukapige basketball mana dogo alikuwa mkali sana kwenye Basket japo alikua mfupi na tulivyoenda akakiwasha kinoma. Sasa kurudi home uncle akamzingua sana viboko vingi na akafunga mlango dogo alale nje. Dogo akajiongeza akapanda boda hadi home (kule kwenye basket alitunzwa vipesa na mashabiki ) akanigongea nikamfungulia akanisimulia ikabidi alale home. Kuamka asbuhi ikiwa nongwa uncle akawasha moto hadi home na akamfukuza dogo kwake eti aishi hukohuko alikolala ndo kwao. Mzee zilikuwa haziungi na uncle na kitendo cha mjomba kuja kufoka pale home akakitofsiri kama dharau hivyo nayeye akamfukuza dogo pale home. Iliniuma sana na ukizingatia me nimehusika kumshawishi dogo twende kwenye game na bahati mbaya mother ashafariki ambae ndo angekuwa mtetezi. Basi nikamuomba sana mzee amkubari dogo mzee akagoma, nikamuita shangazi yangu mmoja (huwa anamuweza father) tukamlilia sana mzee lakini wapi . Mzee akasema kuliko amruhusu dogo kuja pale bora akaishi kwenye moja kati ya nyumba zake alizokuwa anapangisha (mzee alikuwa jumla ana nyumba 6 mbili za urithi) . Basi me nikaona ngoja nihame home nikaishi na dogo kule kwenye nyumba ya mzee ambayo haipo mbali sana na home( ili msosi niwe nachukuwa home tunakula wote). Kiufupi tuliishi na dogo toka 2008 akiwa form2 me nikiwa form 4 hadi me nikamaliza nikaanza saka life kabda ya matokeo kwa kupiga biashara za hapa na pale huku tukiwa hatuelewani na uncle. Dogo akamaliza 2010 akaingia advance pale tabora boys (dogo alikua na akili mno) 20013 akamaliza 6 kwenye application za mkopo mzee wake akagoma ku sign form ya mzazi hivyo dogo akaomba aende veta(japo sikumuelewa) aunt akamlipia na badae akamuunganisha na mzee mmoja tanesco dogo akaanza kama service man badae akala shavu na mpaka sasa ashaenda chuo kamaliza engineering yake na ni kitengo tanesco na mzee wake akaanza kurudisha majeshi (kwanza alianza kujilalamikisha kwa watu eti dogo amemtenga hajui kama ye ndo baba au ana baba mwingine? Badae akaanza kuwasukuma wanae wadogo(wadogo zake dogo wakimuomba pesa anasema wakamuombe kaka yao) uzalendo ukamshinda akiwa ashchoka kimaisha akamuita dogo akasema alikuwa amerogwa (kumchukia) dogo akataka kumkazia but father akamkataza na dogo anamsikiliza sana mzee wangu. Ko mpaka sasa wapo pamoja. Ko story yako me nime experience kupitia binam yangu.
 
Mkuu tatizo ninaloliona kwako labda wewe ni muoga kiasi fulani hivi, watu huwa wanapenda sana kusema neno 'jishushe', hivi ujishushe ili nini au kitokee nini? sijui kwanini wanalipenda hilo neno. Kuna muda naamini hil neno ni kwa ajili ya watu waoga. Na wewe pengine ulishalitumia kipindi fulani au kwenye hicho kikao cha familia.

Jambo lingine Mkuu amini nakwambia hakuna mwanaume unaweza mshauri au kumweleza jambo akakuelewa iwapo kuna mwanamke ambaye ni mpenzi/mke wake nyuma. Kifupi ni kwamba mzee wako hawezi kukuelewa kabisa Mkuu.

Muhimu Mkuu wewe fanya maisha yako, wakikuita kikao kama familia/ukoo nenda alafu uka 'speak your mind', uzuri umesoma unayo elimuwakati una speak your mind tumia reasoning kuwaeleza msimamo wako, achana na habari za kujishusha huo ni uoga na unafiki muhimu usiwafokee au kuwadharau. Jielezee kama mtu mzima sio mtoto anayeogopa kuchapwa.

Wapo watakao kuelewa kama ukitumia reasoning pia wao watakao kuheshimu kutokana na msimamo wako including your father au huyo mama mdogo, hatakuchukulia poa poa tena. Ila kwa vyovyote usirudi kuishi hapo nyumbani, utakuja kuambiwa unamtongoza ma mdogo au ulitaka mbaka kabisa yeye au mdogo wake.
 
Ukishazaliwa kituo kinachofuata ni kupambana na hali yako mkuu. .huna kosa, wala huna hatika komaa na maisha, hao mashangazi achana nao, huyo mamdogo wako mdwanzi tu, wagumu kamaa sisi huwa tunawap3lekea moto maana sisi wengine hatuna miiko wala mipaka, ungepeleka moto kuanzia kwa mamdogo mpaka mdogonwake kabla ya kusepa, n a hao mashangazi pia kama ingewezekana ungewakojolea tu. Man mm mpaka dakika hii nimebaki na ndugu wawili tu hapa duniani, sio kwamba sina ndugu ( ndugu jina ) nnao wengi tu, lakini nimejenga undugu na nature! Kila mwanaadam kama hana ungese ungese ni nduguyangu, na nna furaha kinyama kuliko kipinfi nayumbishwa na hizo mazafanta ndugu...

We pambana ndugu watakuja tu hata kama si original.
 
Unachokosa hapa ni kushindwa kujishusha mara kwa mara hasa kwa hao dnugu zako wasio enda shule.

Wewe ni mtu wa Kupenda haki sana na hupe di kuonewa, ukiwa na ndugu jaribu kujishusha.

Mjeuri inaweza semwa kwa sababu ukiambiwa jambo unalifanya lakini kwa njia tofauti tena kwa maamuzi yako binafsi, unapaswa kujadiliana na mtu anaekupa Amari iwapo unataka kutumia njia nyingine kutatua hiyo changamoto.

Mwisho. rudi nyumbani ukweke mambo swa kama hujaharibu kizazi chako kijacho.
akijichanganya akarudi tu atapewa kesi ya kumchungulia ma mdogo wakati anaoga au kumtongoza ama ma mdogo au mdogo wake kabisa
 
Ndugu yangu tafuta pesa watakuja wenyewe.
Kama anaamini ushirikina point yako ni muhimu keshalishwa tunda na Eva.
 
Yaani Mimi huwezi nitenganisha na damu yangu yaani nitengane na damu yangu kisa mke wa kambo.Nimejifunza Sana ukiwa na mke wa kambo ukaletewa mashtaka kuhusu damu yako yafaa kuwa na akili mbili ya kulia na ya kushoto zitumie kwa pamoja maaana wengi wamewapoteza damu zao wakaja jutia uzeeni wakishafika saa 12 jioni na msaada umegota waliyemdharau au kumtesa akiwa juu.
All in all everything happens for reasons.
Diamond angelelewa vyema asingekuwa star labda angekuwa ni muajiriwa fulani msotaji kama wewe tu.
 
Unamchukia mama yako. Hupatani na Baba yako. Shangazi zako wanakusema vibaya. Una bifu na mama yako mdogo.

Sihitaji kua mtaalamu wa sayansi ya anga za mbali kufahamu kwamba wewe ni tatizo!
 
Huyo mama mdogo wako uliyemzaba kibao fanya bidii pita nae heshima irudi maana ye ndo chanzo.
 
Ukiona umri umeenda, na upo home 'unadekezwa' tarajia zengwe kubwa.
Tafuta watu wa heshima ktk ukoo uende kwa mzee muyamalize.
Sijui wewe ni wa kabila gani, kwa sisi wa kando ya ule mlima mrefu Africa, mzee akikuvimbia, na wewe ukavimba, HUTOTOBOA KTK MAISHA, hata kama umezungukwa na fursa kama matone ya mvua.
 
Tatzo Mzee wangu Tyr alishatekwa na ma mdogo ambaye alimpindua max akishirikiana na Dada zake na Mzee
Pili Mzee ametawaliwa na Dada zake.
Tatu nilishakaa Naye kujua tatzo nn bt hakunielewa ukizngatia kuna taarifa za kuchezewa Kwa ndumba na wapinzani wangu.
Nne hata SKU ya mwisho nilipokanyaga home nilimuomba msamaha Kwa yote Kwa mara nyngn ndo akaleta masharti niliyosema hapo juu na hayo masharti Kwa Imani yangu spo Tyr kusujudia kaburi wala kusujudia wanadamu Kwa kitu ambacho si cha kweli.
Pole sana, Mi najua nguvu ya mahusiano ya kifamilia hasa linapofika suala la ndugu waliozaliwa pamoja, Mara nyingi sana Madada wanapenda sana kuingilia mahusiano ya kaka zao lakini pia hupenda sana kuwalalamikia mawifi zao(waikoolewa) kwa mahusiano yao na waume zao na hasa kama Kwa kaka kuna maslahi mapana.
Tafuta nafasi mtembelee mzee wako na mmalize tofauti zenu bila wewe kwenda kuomba msamaha kwenye makaburi ya wafu, mwambie vile unavyokereka na tabia yake patana naye akiwa mzima kuna siku na wewe utakuwa na watoto wasije wakakufanyia kama wewe na baba yako.
Tengeneza kungali asubuhi.
 
Mkuu wewe ni JEURI kama mzee wako. Damu yake inakimbizana kwenye mishipa yako pia so wote wale wale. Kuja kulia lia hapa haitakusaidia

Kama huna chuki na mtu ule uzi wa kwanza ulitosha kabisa,sasa ulipoona wananzengo wanakuunga mkono ukaja na uzi wa pili. Wa kwanza umemsimanga mama yako,wa pili unamsimanga baba yako,wa tatu utakuja kumsimanga mdogo wako aliyeolewa.

KAMA UNAONA HAWANA UMUHIMU KWENYE MAISHA YAKO SI UPOTEZEE TU YA NINI KUWACHORESHA HAPA
Khs salama ya dogo bs niseme nilikosea hayo mengne unayoisema ni kwasababu hayajakukuta Tu Mzee kweli tena kuna watu ni pasua kichwa.
Kuhusu ulalamishi Kwa taarifa yako sinaga muda wa kulalamikia mtu hata SKU moja mi nilishaamua kufanya maisha yangu sina chuki na mtu aisee.
 
Back
Top Bottom