Hivi ulitongozaje siku ile ulipo tongoza kwa mara ya kwanza.

hii imenkumbusha kisa cha jamaa wa movie ya the gods must be crazy,part one kama sikose,
jamaa alijipanga kweli kweli ila alipofika akishia kuharib mwishoe akamtell mdada ni an interesting psychological phenomena..............mdada alikufa mbavu kwa kwa jinc jamaa alivyokuwa anahangaika ila alimwelewa akampiga bonge la kiss.............mambo yakawa mwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
Aya yaya yayayaya!.
 
hahahahahahaaaaaa,
aya ya yayayaya, [
naipenda kwa kweli..QUOTE=Kyaiyembe;4386351]Aya yaya yayayaya!.[/QUOTE]
 
kuna jamaa alikuwa bingwa wa kuandika barua za mapenzi nilimtumia huyo kwa ofa sigara mbili za Nyota, barua aliyonitungia huyo staa nilimpa mdogo wangu wa kike aipeleke kwa demu wangu mtarajiwa. Ilinichukua mieze miwili kupata majibu, hata hivyo nilikubaliwa na sasa tuna watoto wanne,first born anasubiri jina lake litoke TCU!

Umetisha mzazi..
 
Wanaume kumbe wanakazi kutongoza,wakishapata ndio ooooooooooh marijali wao...
 
nilimwambie nampenda akaniambia nikaandke barua tena ya kiingereza.
 
nilimnunulia blackberry na Vitz.. baada ya hapo hakukuwa na haja ya saund!
 
mim nikikumbuka kwa mara ya kwanza kulikuwa na msichana 1 tunasoma nae alikuwa mlokole nilimwandikia barua kwanza nilitembea nayo kama wiki hivi nikiogopa kumpa siku hiyo mwalim wa kiswahili alikuja na kutuunganisha kwenye makundi akagawa vitabu tukawa tunasoma mim nikaomba daftari yake ya kiswahili nikaiweka ile barua nakumrudishia baati mbaya mda si mrefu mwalim akatoa kazi ya kufanya alipofungua tu daftari akaikuta alistuka sana mpaka madawati ya karibu yakastuka akaitupa chini watu wakaanza kumcheka yeye akaanza kulia kwa sauti mpaka mwalim akasikia na kuuliza kunani ikachukuliwa ile barua na mwalim na kusomwa mbele ya darasa ilikuwa soo sana.mzee mzima nililowa sana najasho
 
Dah, Ingekua mimi nisingerudi tena shule!
mim nikikumbuka kwa mara ya kwanza kulikuwa na msichana 1 tunasoma nae alikuwa mlokole nilimwandikia barua kwanza nilitembea nayo kama wiki hivi nikiogopa kumpa siku hiyo mwalim wa kiswahili alikuja na kutuunganisha kwenye makundi akagawa vitabu tukawa tunasoma mim nikaomba daftari yake ya kiswahili nikaiweka ile barua nakumrudishia baati mbaya mda si mrefu mwalim akatoa kazi ya kufanya alipofungua tu daftari akaikuta alistuka sana mpaka madawati ya karibu yakastuka akaitupa chini watu wakaanza kumcheka yeye akaanza kulia kwa sauti mpaka mwalim akasikia na kuuliza kunani ikachukuliwa ile barua na mwalim na kusomwa mbele ya darasa ilikuwa soo sana.mzee mzima nililowa sana najasho
 
Kipindi hicho nilikuwa darasa la sita, japo nilikuwa na mwandiko mbaya lakini nilijitahidi sana kuilembesha sana barua yangu.
Safari ilianza kuelekea kwa kademu kangu katarajiwa, baada ya dakika chache nikakaona kadogo kake so nkaamua kukakabidhi
ile barua.Fasta fasta mtoto akamkabidhi mbele ya mama yake kwani aliwakuta jikoni wanapika.
Ilikuwa yapata saa moja moja ,mguu kwa mguu mama na mwanae nyumban kwetu. nilipowaona nilizama chumban na kuingia
uvunguni. muda si muda ukumu ikatolea na mnyamwezi nikatiwa hatiani mbele ya jaji(mother). Nilitandikwa viboko sita na nkawaaidi
kutorudia tabia hiyo ambayo waliita kuwa ni chafu.
 
mtoa mada hongera yako.mi nilikuwa mwoga sana, ila bro wangu aka set mambo mpaka sasa najua kujitafutia.
 
Mi nlimuandikia kaujumbe kwenye daftari la jografia, akasau kuchana hiyo karatasi, akakusanya daftari. Hiyo kesi ilikuwa kubwa mpk kwa mwalimu mkuu. Huyo dem sasa hv ni hakimu kanda ya ziwa huko.

we nawe hadi leo unafatilia matapishi ya zamani waachie wenye kumiliki vyao mshika mawili 1 humponyoka, kuna jirani yangu ana tabia kama yako hadi leo hajitambui ni kurudi rudi nyuma anaonyesha jinsi gani hajui hata anataka nini cha kushangaza madai antongozwa je kuchunwa kwake pia ni moja ya kutongozwa au
 
we nawe hadi leo unafatilia matapishi ya zamani waachie wenye kumiliki vyao mshika mawili 1 humponyoka, kuna jirani yangu ana tabia kama yako hadi leo hajitambui ni kurudi rudi nyuma anaonyesha jinsi gani hajui hata anataka nini cha kushangaza madai antongozwa je kuchunwa kwake pia ni moja ya kutongozwa au

Kuchunwa suna, mwanaume anasifiwa matumizi
 
Kuchunwa suna, mwanaume anasifiwa matumizi

unaweza ukawa kibarua na ukawa unaonekana una matumizi kumbe kibega unafanya vya wanaume walio tairiwa

kutairiwa: maana mwanaume mwenye familia na mwenye kuleta manukato.

manukato: maana harufu nzuri kwa familia yake like upendo,amani,ushirikiani,maendeleo,afya,kwa kifupi kufata maadili ya dini kujua mke na watoto kwa kuwatii na kuwapa haki zao za msingi au hata kujieshimu.

kujieshimu:kunafatana na matendo mema.

matendo mema:kufatiliwa na baraka za mwenyezi mungu.

acha kupoteza watu hapa hivi ndo umemaliza IV au u dnt sound kama wewe ni mmiliki wa familia
 
Ila sredi hii ina ubaguzi,
ina mana sisi wanawake hatuwezi kutongoza?
Wengine tuna vipaji kama wanaume.
 
Back
Top Bottom