Kwanza nianze kwa kumwelezea waziri ni nani? Kwa kadri ninavyofahamu mimi waziri ni Mwanasiasa. Waziri ni Kada wa chama chake. Waziri ni shabiki wa chama chake. Waziri ni MNAZI wa chama chake. Waziri ni mshauri wa kisiasa wa Rais. Waziri ni msimamizi wa SERA na AHADI za chama chake katika wizara husika. Kazi kuu ya waziri katika wizara ni kufuatilia manifesto ya chama chake, iliyowapa ushindi katika uchaguzi. Naomba hata hivyo nikiri kuwa mimi si 'mwanasiasa' [ingawa nashawishika kuamini kuwa kila mtu ni mwanasiasa] lakini pia si mtaalamu wa mambo ya Utawala bali mimi ni Social Worker kitaaluma.
Najua katika kila wizara kuna Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu pengine Manaibu Makatibu Wakuu wawili ama zaidi, lakini kuna Wakurugenzi kwa kila idara, Manaibu Wakurugenzi, Maafisa waandamizi na Maafisa wengine mbalimbali ambao ndio wataalamu na watendaji mahususi. Sasa Waziri anafanya nini tangu asubuhi saa 1.30 [kwa wengine watakao sifa] hadi saa 3 usiku. Napenda tuangalie kwa makini hapa; hivi tunamuhitaji kweli kweli waziri mtendaji? Kama pana waziri mtendaji wizarani, hawa Makatibu, Makamisna, Wakurugenzi na Maafisa mbalimbali wanafanya nini ambacho waziri anaweza kufanya lakini wao wanashindwa kufanya? Imetokea mara nyingi utaona Waziri akitaka kumfukuza mtumishi kazi, anamwambia [siyo kuamuru] Katibu Mkuu amfukuze mtumishi husika, kwa nini?
Kazi azifanyazo waziri si hizo hizo anazotakiwa kufanya Katibu Mkuu? Kwa kitendo cha waziri kufanya kazi za Katibu Mkuu na za Maafisa wengine si kumfanya Katibu Mkuu awe 'redundant?' Kwa utaratibu huu si tunamlipa Katibu Mkuu ambaye hafanyi kazi yote anayotakiwa kufanya? Kwa tabia hii ya Mawaziri kufanya kila kitu si anauza tu sura kwa watu 'kampeni' ili chama chake kionekane kinafanya kazi? Kwa nini kunakuwa na watu wawili wanaotakiwa kufanya kazi ile ile na bado wanalipwa mishahara na marupurupu kibao? Hayo si matumizi mabaya ya rasilimali za nchi?
Kwa mapendekezo yangu, waziri abakie kuwa mwanasiasa, mshauri wa Rais, kada wa chama, shabiki, n.k. ila aruhusiwe kwenda wizarani kufuatilia manifesto ya chama chake kama inatekelezwa kama walivyowaahidi wapiga kura. Sasa, kufanya kazi hiyo hahitaji magari wawili, mshahara mkuuuubwa na marupurupu kibaaaao! Namna nzuri ya waziri kufuatilia [siyo kusimamia] ahadi za chama chake ni kuwa na vikao vichahe, kwa mfano vikao vinne [quarterly] kwa mwaka vinatosha ili awape wataalamu nafasi ya kufanya kazi kwa uhuru naye apate taarifa ya quarter. Kama patakuwa na mapungufu atasawazisha. Kama Katibu mkuu hawezi kazi atamshauri Rais amfute kazi, basi. Waziri [wakati mwingine si mtaalamu] anawatisha tu watumishi wizarani [kwa uwepo wake] hivyo wizara zingine wanamwachia waziri afanye kila kitu! Makatibu wakuu wengi kwa kweli wanabembea tu kwenye vitu vyao ofisini.
Napenda nieleweke hata hivyo kuwa kuna mawaziri wanaochapa kazi vizuri tu lakini wanaweza kufanya hivyo kwa kuwa na vikao vya robo mwaka na kufuatilia kile walichokubaliana robo iliyopita. Ufuatiliaji kama huu unatosha kabisa kuona kuwa manifesto inatekelezeka kikamilifu. Maana kama kuwa wizarani masaa kumi na nne [14] ndiko kunakotoa tija, basi inabidi waziri awepo pia katika mamlaka zilizo chini ya wizara yake. Kwa mfano waziri Magufuri agawe muda kila siku awepo Wizarani, TANROADS, TAMESA, n.k. Waziri afanye kazi kama afanyavyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya. Inatosha kabisa hiyo na itapunguza matumizi, kisha waziri asiwe jikoni kabisa ili afuatilie sawasawa. Hivyo afanyavyo yeye anakuwa sehemu ya utekelezaji. Kwa mtindo huu ni makosa Mwakyembe kulaumu Bandari wanapoharibu. Ni makosa Magufuli kulaumu TANROADS, kwa sababu yeye naye ni sehemu ya utendaji!
Nafahamu waziri anaruhusiwa na katiba na sheria kufanya anayofanya, lakini hivi ni lazima Tanzania kufanya kazi kama Uingereza ama India? Napendekeza wataalamu waachwe wafanye kazi kwa uhuru lakini wafuatiliwe. Tujadiri.
Najua katika kila wizara kuna Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu pengine Manaibu Makatibu Wakuu wawili ama zaidi, lakini kuna Wakurugenzi kwa kila idara, Manaibu Wakurugenzi, Maafisa waandamizi na Maafisa wengine mbalimbali ambao ndio wataalamu na watendaji mahususi. Sasa Waziri anafanya nini tangu asubuhi saa 1.30 [kwa wengine watakao sifa] hadi saa 3 usiku. Napenda tuangalie kwa makini hapa; hivi tunamuhitaji kweli kweli waziri mtendaji? Kama pana waziri mtendaji wizarani, hawa Makatibu, Makamisna, Wakurugenzi na Maafisa mbalimbali wanafanya nini ambacho waziri anaweza kufanya lakini wao wanashindwa kufanya? Imetokea mara nyingi utaona Waziri akitaka kumfukuza mtumishi kazi, anamwambia [siyo kuamuru] Katibu Mkuu amfukuze mtumishi husika, kwa nini?
Kazi azifanyazo waziri si hizo hizo anazotakiwa kufanya Katibu Mkuu? Kwa kitendo cha waziri kufanya kazi za Katibu Mkuu na za Maafisa wengine si kumfanya Katibu Mkuu awe 'redundant?' Kwa utaratibu huu si tunamlipa Katibu Mkuu ambaye hafanyi kazi yote anayotakiwa kufanya? Kwa tabia hii ya Mawaziri kufanya kila kitu si anauza tu sura kwa watu 'kampeni' ili chama chake kionekane kinafanya kazi? Kwa nini kunakuwa na watu wawili wanaotakiwa kufanya kazi ile ile na bado wanalipwa mishahara na marupurupu kibao? Hayo si matumizi mabaya ya rasilimali za nchi?
Kwa mapendekezo yangu, waziri abakie kuwa mwanasiasa, mshauri wa Rais, kada wa chama, shabiki, n.k. ila aruhusiwe kwenda wizarani kufuatilia manifesto ya chama chake kama inatekelezwa kama walivyowaahidi wapiga kura. Sasa, kufanya kazi hiyo hahitaji magari wawili, mshahara mkuuuubwa na marupurupu kibaaaao! Namna nzuri ya waziri kufuatilia [siyo kusimamia] ahadi za chama chake ni kuwa na vikao vichahe, kwa mfano vikao vinne [quarterly] kwa mwaka vinatosha ili awape wataalamu nafasi ya kufanya kazi kwa uhuru naye apate taarifa ya quarter. Kama patakuwa na mapungufu atasawazisha. Kama Katibu mkuu hawezi kazi atamshauri Rais amfute kazi, basi. Waziri [wakati mwingine si mtaalamu] anawatisha tu watumishi wizarani [kwa uwepo wake] hivyo wizara zingine wanamwachia waziri afanye kila kitu! Makatibu wakuu wengi kwa kweli wanabembea tu kwenye vitu vyao ofisini.
Napenda nieleweke hata hivyo kuwa kuna mawaziri wanaochapa kazi vizuri tu lakini wanaweza kufanya hivyo kwa kuwa na vikao vya robo mwaka na kufuatilia kile walichokubaliana robo iliyopita. Ufuatiliaji kama huu unatosha kabisa kuona kuwa manifesto inatekelezeka kikamilifu. Maana kama kuwa wizarani masaa kumi na nne [14] ndiko kunakotoa tija, basi inabidi waziri awepo pia katika mamlaka zilizo chini ya wizara yake. Kwa mfano waziri Magufuri agawe muda kila siku awepo Wizarani, TANROADS, TAMESA, n.k. Waziri afanye kazi kama afanyavyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya. Inatosha kabisa hiyo na itapunguza matumizi, kisha waziri asiwe jikoni kabisa ili afuatilie sawasawa. Hivyo afanyavyo yeye anakuwa sehemu ya utekelezaji. Kwa mtindo huu ni makosa Mwakyembe kulaumu Bandari wanapoharibu. Ni makosa Magufuli kulaumu TANROADS, kwa sababu yeye naye ni sehemu ya utendaji!
Nafahamu waziri anaruhusiwa na katiba na sheria kufanya anayofanya, lakini hivi ni lazima Tanzania kufanya kazi kama Uingereza ama India? Napendekeza wataalamu waachwe wafanye kazi kwa uhuru lakini wafuatiliwe. Tujadiri.