Hivi tanzania hatuna ajenda??????

Najijua

JF-Expert Member
Nov 5, 2010
1,039
180
Ndg zangu,
Kuna jambo linaendelea kusumbua kichwa changu ndugu zangu na hili ni kujiuliza hivi Tanzania na raia wake huw hatuna ajenda?Ajenda zetu ni kama milipuko ya mabomu au majanga ya moto?

Sasa hivi nchi nzima watu wanazungumzia ajenda ya kwa babu Loliondo na wamesahau harakati zote na ugumu wote wa maisha. Hoja ya katiba mpya imeishia wapi?hoja za TUCTA kupanda bei ya umeme na gharama nyingine zimeishia wapi?hoja za ukali maisha zimeishia wapi?harakati na hoja za kupinga malipo ya DOWANS zimeishia wapi?

Kweli Makamba alisema kweli tukamkebehi pale aliposema "Watanzania ni wasahaulifu"

With all that, i remain
 
usisahau kwamba watu husema kipya kinyemi, na hili jambo la loliondo ni jipya si muda litasahaulika na tutarudi kwenye hizo hoja zako VUMILIA KIDOGO.
 
Kwahiyo watanzania ni watu wa kufuata upepo?hatuwezi ku stick kwenye jambo mmoja likaisha then tuhamie mengine?na kuna habari nimesikia babu kapigwa marufuku mpaka dawa yake itakapofanyiwa uchunguzi na isajiliwe TFDA, Lets be serious jamani
 
Back
Top Bottom