Hivi ni kweli tunasamehe na kusahau?

Kusamehe inawezekana ,, ila vigumu kusahau ,inakuwa s rahis. Mtendewa kusahau ,, na pia inategemea n kesi yenyewe uzito wake
 
Katika kusamehe na kusahau aisee yapo makosa mengine ambayo hayasahauliki! Kwangu mimi kwa hali yangu ya ubinadamu naweza kumsamehe mtu akinikosea kosa lolote lile ila yapo engine ambayo huwa ni vigumu kuyasahau. Cha muhimu huwa namwomba Mungu wangu anisaide niyasahau kabisa yale nilokosewa au hata nikiyakumbuka yasinifanye niumie au nimchukie aliyenitendea huo ubaya.
 
Mie huwa nashindwa kusahau ingawa nasamehe ..na siulizi tena nikisamehe ..ila kumbukumbu haitoki
 
me huwa nasamehe bt % kubwa huwa sisahau bali naignore tu. mf. miaka ileee ya kipindi kileee nliwah kumfumania bf wangu live bt baada ya km wiki 2 kupita nkasahau sahau tukarudiana na mapenz yakanoga kuliko mwanzo simply b-cos alikubali kosa na kuomba msamaha. kiukweli me mtu akikubali kosa na ku-apologise huwa namsamehe na kuyaacha tu kwa kweli huwa hayasahauliki

Kumbeeeeee!
 
Kusamehe inawezekana ,, ila vigumu kusahau ,inakuwa s rahis. Mtendewa kusahau ,, na pia inategemea n kesi yenyewe uzito wake

Hapo kwa red nakubaliana na wewe wahida, so huwa tuna-pretend kusahau?
 
Katika kusamehe na kusahau aisee yapo makosa mengine ambayo hayasahauliki! Kwangu mimi kwa hali yangu ya ubinadamu naweza kumsamehe mtu akinikosea kosa lolote lile ila yapo engine ambayo huwa ni vigumu kuyasahau. Cha muhimu huwa namwomba Mungu wangu anisaide niyasahau kabisa yale nilokosewa au hata nikiyakumbuka yasinifanye niumie au nimchukie aliyenitendea huo ubaya.

WALIMWEUSI nadhani hapo kwa red ndo uhalisia mwenyewe, lakini kusema yupo anayesahau kabisa nadhani ni too hypothetical au?
 
Kusahau si kupoteza kumbukumbu....................Kama uzito wa kile ulichotendewa ni mkubwa (kwako mwenyewe) unaweza kusamehe na kusahau (kwa maana ya kutorejesha moyoni maumivu uliotendewa)

Lakini pia unaweza kusamehe na usisahau kwa maana ya kwamba kumbukumbu mbaya juu ya lile ulilotendewa inakurudia kwa nguvu na kwa sababu inasukumwa emotions unashindwa kuzuia.

Lakini unaweza usisamehe wakati huo na ukasahau baada ya kipindi fulani na usiwe na kinyongo kabisa.

Muhimu kuzingatia: Kusahau si kupoteza kumbukumbu
 
Mie huwa nashindwa kusahau ingawa nasamehe ..na siulizi tena nikisamehe ..ila kumbukumbu haitoki

Exactly FirstLady, same as me! Nadhani huu ndo uhalisia wenyewe, sidhani kama kuna ambaye anaweza kutoa kumbukumbu kabisa
 
Kusahau si kupoteza kumbukumbu....................Kama uzito wa kile ulichotendewa ni mkubwa (kwako mwenyewe) unaweza kusamehe na kusahau (kwa maana ya kutorejesha moyoni maumivu uliotendewa)

Lakini pia unaweza kusamehe na usisahau kwa maana ya kwamba kumbukumbu mbaya juu ya lile ulilotendewa inakurudia kwa nguvu na kwa sababu inasukumwa emotions unashindwa kuzuia.

Lakini unaweza usisamehe wakati huo na ukasahau baada ya kipindi fulani na usiwe na kinyongo kabisa.

Muhimu kuzingatia: Kusahau si kupoteza kumbukumbu

Mkuu nimependa zaidi ulivyofafanua maana ya kusahau hapo kwa red
 
Nakubaliana na wewe Lady N, lakini ni kweli vipo ambayo vinasahaulika au tunajifanya tu kuvisahau?
yap, vipo ambavyo vinasahaulika kama tu mkosaji hatarudia tena, lkn akirudia anakumbusha yale ya nyuma
 
Binadamu hasa waafrika hawasahau.. Mtu unakaa nae miaka 10 lakini siku utasikia anakuambia ' we si ulinitenda kitu flani mwaka 2002 na ndio hivo zamu yako sasa' dah wanawake wa kiafrica hawasahau
 
Back
Top Bottom