Mtumishi Wetu
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 5,712
- 1,906
Ni muda sasa umepita tangu bunge letu tukufu limalizike kwa kumtaka waziri mkuu ajiudhuru au mawaziri waliotajwa kwenye riporti ya CAG wajiudhuru!!!!
Kwanza jambo la kusikitisha Mheshimiwa Raisi hali akijua kuwa kuna sakata linalomtaka PM ajiudhuru, yeye huyo akaenda majuu Latin America kukagua mashamba ya nyanya!!!!!
Baada ya kurudi moto ukiwa bado unawaka yeye huyo kwenye mazishi ya Merehemu Raisi wa Malawi, kama vile anakwepa kitu fulani vile!!!
Si mnajua tena kama kuna shida nyumbani au watu wanakusubiri kwa jambo fulani na wewe bado hujawa tayari, utapita kwa jirani au mahali ili upitishe muda watu hao waondoke ndio urudi nyumbani kupata taarifa zao kwa mama!!!
Hiyo ni delaying tactic watasubiri mwisho watachoka, hapo ni kwamba nia thabiti ya kufanya jambo muhimu hakuna!!!!!!!!!
Kama ni kweli unataka kumchukulia mtu hatua tena umeambiwa ni mwizi, lazima kwanza umtoe ofisini tena kwa ghafla, hapo utakuwa na uhuru wa kupekua kitu kimoja kimoja mpaka upate ushahidi wa kitu unachotafuta!!!!
Sasa unapompa mkuu kwenye ofisi muda huku kukiwa na vitisho vya kufukuzwa kazi, wewe ukamuacha pale unategemea nini????
Eti kwenye hotuba mkuu anasema ripoti ya CAG iwe wazi hivyo ana maana gani kwani hiyo ripoti CAG ataleta kwenye tume za bunge ripoti isiyokuwa wazi??????
Kama ripoti zimefikishwa bungeni na wabunge wamejihakikishia kuwa ni sawa huo wizi umefanyika bila kujali ilichukua muda gani kufanyika inatakiwa hatua ya haraka kuchukuliwa ili kuokoa maeneo mengine mapya yasifanyiwe wizi!!!
Ni lazima wahusika wa wizi wasimamishwe kazi ili uchunguzi huru ufanyike, uchunguzi utafanyika vipi wakubwa wakiwa bado maofisini????
Nia thabiti ya kuokoa fedha za Watanzania zisiendelee kuibiwa haipo mimi hilo naliona sijui wenzangu mnasemaje kuhusu hili?????
Kwanza jambo la kusikitisha Mheshimiwa Raisi hali akijua kuwa kuna sakata linalomtaka PM ajiudhuru, yeye huyo akaenda majuu Latin America kukagua mashamba ya nyanya!!!!!
Baada ya kurudi moto ukiwa bado unawaka yeye huyo kwenye mazishi ya Merehemu Raisi wa Malawi, kama vile anakwepa kitu fulani vile!!!
Si mnajua tena kama kuna shida nyumbani au watu wanakusubiri kwa jambo fulani na wewe bado hujawa tayari, utapita kwa jirani au mahali ili upitishe muda watu hao waondoke ndio urudi nyumbani kupata taarifa zao kwa mama!!!
Hiyo ni delaying tactic watasubiri mwisho watachoka, hapo ni kwamba nia thabiti ya kufanya jambo muhimu hakuna!!!!!!!!!
Kama ni kweli unataka kumchukulia mtu hatua tena umeambiwa ni mwizi, lazima kwanza umtoe ofisini tena kwa ghafla, hapo utakuwa na uhuru wa kupekua kitu kimoja kimoja mpaka upate ushahidi wa kitu unachotafuta!!!!
Sasa unapompa mkuu kwenye ofisi muda huku kukiwa na vitisho vya kufukuzwa kazi, wewe ukamuacha pale unategemea nini????
Eti kwenye hotuba mkuu anasema ripoti ya CAG iwe wazi hivyo ana maana gani kwani hiyo ripoti CAG ataleta kwenye tume za bunge ripoti isiyokuwa wazi??????
Kama ripoti zimefikishwa bungeni na wabunge wamejihakikishia kuwa ni sawa huo wizi umefanyika bila kujali ilichukua muda gani kufanyika inatakiwa hatua ya haraka kuchukuliwa ili kuokoa maeneo mengine mapya yasifanyiwe wizi!!!
Ni lazima wahusika wa wizi wasimamishwe kazi ili uchunguzi huru ufanyike, uchunguzi utafanyika vipi wakubwa wakiwa bado maofisini????
Nia thabiti ya kuokoa fedha za Watanzania zisiendelee kuibiwa haipo mimi hilo naliona sijui wenzangu mnasemaje kuhusu hili?????