HORSE POWER
JF-Expert Member
- Feb 22, 2015
- 2,099
- 1,415
Habari wana JF,
Pengine nimetumia lugha kali kidogo lakini ndio hivyo ilivyo. Kuna hawa wanaoitwa mafisadi ambao kimsingi si mafisadi bali ni majambazi watumiao peni na karatasi kuibia umma. Malalamiko dhidi ya ufisadi ni mengi na kashfa za ufisadi ni nyingi mno. Hili liko wazi.
Hawa watu ni hatari kwa mustakabali wa nchi na kwa lugha nyingine hawa ndio waliotufikisha hapa. Wameiibia hii nchi vibaya sana na mpaka leo bado 'inaatangatanga' nyikani. Hoja yangu ni kwamba kwanini tusiwe na sheria ya kuwanyonga hawa watu.
Hawa mafisadi ni wauaji wakubwa kuliko wauaji wa albino.Kwa ufisadi wao wengi wamekufa kwa kukosa dawa, kwa ufisadi wao miradi mingi imekwama. Tuanze sasa kunyonga hawa 'majizi' kama wafanyavyo baadhi ya nchi vinginevyo wataendelea kuchezea hii nchi. Hebu angalia hii; ekari ya milioni 25 watu wamecheza 'rafu' mpaka milioni 800 kwa ekari, hivi ni kiasi cha pesa kimeangamia? Tumeibiwa sana.
Tumechekeana sana. Tumefanywa mabwege sana. Inatosha sana! Upelekwe muswada wa kunyonga hawa mafisadi. Na hapa nawaomba wale wanaojiita watetezi wa haki za binadamu wawe na subira kidogo ili tunyooshe nchi.
Nawasilisha.
Pengine nimetumia lugha kali kidogo lakini ndio hivyo ilivyo. Kuna hawa wanaoitwa mafisadi ambao kimsingi si mafisadi bali ni majambazi watumiao peni na karatasi kuibia umma. Malalamiko dhidi ya ufisadi ni mengi na kashfa za ufisadi ni nyingi mno. Hili liko wazi.
Hawa watu ni hatari kwa mustakabali wa nchi na kwa lugha nyingine hawa ndio waliotufikisha hapa. Wameiibia hii nchi vibaya sana na mpaka leo bado 'inaatangatanga' nyikani. Hoja yangu ni kwamba kwanini tusiwe na sheria ya kuwanyonga hawa watu.
Hawa mafisadi ni wauaji wakubwa kuliko wauaji wa albino.Kwa ufisadi wao wengi wamekufa kwa kukosa dawa, kwa ufisadi wao miradi mingi imekwama. Tuanze sasa kunyonga hawa 'majizi' kama wafanyavyo baadhi ya nchi vinginevyo wataendelea kuchezea hii nchi. Hebu angalia hii; ekari ya milioni 25 watu wamecheza 'rafu' mpaka milioni 800 kwa ekari, hivi ni kiasi cha pesa kimeangamia? Tumeibiwa sana.
Tumechekeana sana. Tumefanywa mabwege sana. Inatosha sana! Upelekwe muswada wa kunyonga hawa mafisadi. Na hapa nawaomba wale wanaojiita watetezi wa haki za binadamu wawe na subira kidogo ili tunyooshe nchi.
Nawasilisha.