Hivi ndivyo ccm inavyohujumiwa

Mghaka

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
320
127
Wahenga wanatwambia kama unaishi kwenye nyumba ya vioo usiwatupie maadui zako mawe. Ninapata shida sana kufuatilia hoja za wabunge wa ccm bungeni, kama kuna kitu wanafanikiwa ni kuwakejeli wabunge wa upinzani. Bahati mbaya kejeli hizi ni mafanikio kwa wapinzani.

Bajeti inayojadiliwa bungeni ni ile ya serikali ambayo wapinzani wanaipinga kwa hoja ambazo zimewasilishwa kupitia waziri kivuli na michango mingine ya wabunge inayoendelea bungeni sasa. Wabunge wa ccm kuivalia njuga hoja ya waziri kivuli ni kufirisika kimawazo. Hoja ya waziri kivuli ni mchango na mawazo ya upinzani. Utashanga ccm wameacha agenda na kuunda agenda yao. Mwisho wa siku ccm wote hawatakuwa wamemtendea haki waziri wa fedha maana hakuna cha maana anachopata kutoka kwao.

Wamepoteza wasikilizaji nje ya bunge wakiona wa ccm anasimama wanasema ni wale wale wa yaleyale.
Hakuna kitu kibaya katika siasa kama kupoteza mvuto na maana yake ni kukosa fursa ya kusikilizwa. Ukisifiwa na mke wako, watoto na ndugu zako wewe si kitu, maana unatekeleza yale wanayotegemea kutoka kwako. Ni vema ukafanya vizuri na kuvutia watu wengine nje ya wale ambao wanakuhusu.


Kwa hiyo kama watu wanadhani wabunge wetu wa ccm wanakijenga chama kwa kuwakejeli wa upinzani hii ni bahati mbaya sana tena sana kwani matokeo yake ni kinyume. Ccm inabomolewa na wabunge wake bungeni. Ccm inabomolewa na makada wake serikalini na ccm inabomolewa na wanasiasa wake uchwara majukwaani. Kama ingekuwa siasa ni mchezo wa pointi kama ngumi sasa hivi refa wa mpambano wa wapinzani na ccm alipaswa kusimamisha mpambano kwani ccm inatoka damu kila sehemu ya uso na majeraha yamekuwa makubwa mno.

Bondia wa namna hii anaweza kupandwa hasira na kushika silaha ya aina yoyote akaishia kuua nataahadharisha washabiki na bondia anayepambana nae kuchukua tahadhali mapema.
 
Wahenga wanatwambia kama unaishi kwenye nyumba ya vioo usiwatupie maadui zako mawe. Ninapata shida sana kufuatilia hoja za wabunge wa ccm bungeni, kama kuna kitu wanafanikiwa ni kuwakejeli wabunge wa upinzani. Bahati mbaya kejeli hizi ni mafanikio kwa wapinzani.

Bajeti inayojadiliwa bungeni ni ile ya serikali ambayo wapinzani wanaipinga kwa hoja ambazo zimewasilishwa kupitia waziri kivuli na michango mingine ya wabunge inayoendelea bungeni sasa. Wabunge wa ccm kuivalia njunga hoja ya waziri kivuli ni kufirisika kimawazo. Hoja ya waziri kivuli ni mchango na mawazo ya upinzani. Utashanga ccm wameacha agenda na kuunda agenda yao. Mwisho wa siku ccm wote hawatakuwa wamemtendea haki waziri wa fedha maana hakuna cha maana anachopata kutoka kwao.

Wamepoteza wasikilizaji nje ya bunge wakiona wa ccm anasimama wanasema ni wale wale wa yaleyale.
Hakuna kitu kibaya katika siasa kama kupoteza mvuto na maana yake ni kukosa fursa ya kusikilizwa. Ukisifiwa na mke wako, watoto na ndugu zako wewe si kitu, maana unatekeleza yale wanayotegemea kutoka kwako. Ni vema ukafanya vizuri na kuvutia watu wengine nje ya wale ambao wanakuhusu.


Kwa hiyo kama watu wanadhani wabunge wetu wa ccm wanakijenga chama kwa kuwakejeli wa upinzani hii ni bahati mbaya sana tena sana kwani matokeo yake ni kinyume. Ccm inabomolewa na wabunge wake bungeni. Ccm inabomolewa na makada wake serikalini na ccm inabomolewa na wanasiasa wake uchwara majukwaani. Kama ingekuwa siasa ni mchezo wa pointi kama ngumi sasa hivi refa wa mpambano wa wapinzani na ccm alipaswa kusimamisha mpambano kwani ccm inatoka damu kila sehemu ya uso na majeraha yamekuwa makubwa mno.

Bondia wa namna hii anaweza kupandwa hasira na kushika silaha ya aina yoyote akaishia kuua nataahadharisha washabiki na bondia anayepambana nae kuchukua tahadhali mapema.


Wanajua kabisa kwamba hata wakichangia hajuna kitakacho badilika kwenye bajeti yao. Baadhi yao walijaribu kuipinga wakapigwa mkwara waka fyata mkia. Kwa hiyo wameona wapoteze muda ambao wangeutumia kuijadili na kuchangia kuwaponda wapinzani. Mwisho wa siku bunge la bajeti litakwisha na wao wanabeba posho zao.

Tunawasubiri tu uraiani 2015 ni kikomo. Na wakijaribu kuchakachua haki ya nani tutabeba silaha..bora tuishe wote kuliko kuishi kwenye shida wakati mali tunazo.
 
Ulichokiongea kinamsaada mkubwa kwa watu walio tayari kusaidika,lkn kwa vile wapewao ushauri ni sawa na sikio la kufa, bado litaenelea kutoa usaha tu kuelekea kuzimu hata ufanyeje.Na nina kutahadhalisha ukae mbali kwani kwa jinsi lilivyo kwisha halibika nakusihi ukae mbali kwani unaweza kutumbukiwa na pindi litokeapo hilo stashangaa kwani ni kawaida ya mgonjwa huyu pale aonekanapo kusaidiwa kumgeuka msaidizi wake kwa matusi na kejeri kibao na kisha kujigamba kuwa yeye ni doctor tena daraja 1 ktk hospitali ya rufaa ilihali haonyeshi mawazo ama mchanganuo wowote wa kitabibu unao weza kuleta ufanisi.Sijui ni DR gani huyu hata mganga wa kienyeji hawezi kuwa hivyo.Ama kweli kama asemavyo Andanenga,"Usione mgongo kutuna ukadhani umeshiba,macho kuona,ukadhani yatizama,kila uonacho,usione ukadhani"
 
........Ninapata shida sana kufuatilia hoja za wabunge wa ccm bungeni, kama kuna kitu wanafanikiwa ni kuwakejeli wabunge wa upinzani. Bahati mbaya kejeli hizi ni mafanikio kwa wapinzani. Kwa hiyo kama watu wanadhani wabunge wetu wa ccm wanakijenga chama kwa kuwakejeli wa upinzani hii ni bahati mbaya sana tena sana kwani matokeo yake ni kinyume.

Majibu haya hapa:

Tuliona la Dr. Slaa na EPA Bungeni mwaka 2007, CDM wakashinda kesi Mahakama ya Wananchi na bado wanazidi kuvuna riba ya makosa yalitokana na udhaifu wa Bunge la wakati ule. Ikaja mwaka 2008 Zitto akafukuzwa Ubunge, wimbi la ushindi wa kuungwa mkono na wananchi likaendelea kusimama upande cha CDM. Bunge jipya 2011 tumewabeza CDM na Katiba, leo hii tunafakamia matapishi yetu tukiwa chooni kwa wapinzani. Juzi juzi tu Jaji wa Mahakama katika kesi ya Uchaguzi wa Arusha, kwa kufikiri amefanya kazi ya kusifiwa na chama, kaleta balaa uraiani kwa kumuacha Godbless Lema alande lande nchi nzima. Sasa badala ya watu wa Arusha wavue magamba, nchi nzima hata watoto wanavaa magwanda. Bado tu hatujajifunza wala kuwafunza au kuwaeleza watoa maamuzi kwamba; chonde chonde kujipendekeza kwenu kwa nia ya kukinusuru Chama Tawala, serikali na Taasisi zake (Bunge, Uraisi, Mahakama) havisaidii bali ndo vinamwaga petrol kwenye tanuru la kuni kavu za zinazoiteketeza serikali! Wananchi wa Tanzania ya leo, si wa Tanganyika ya Mwaka 1947! Wana maamuzi rohoni mwao tayari kwa kiama cha serikali yao hapo mwaka 2015.
Mghaka Unasema....!

Ccm inabomolewa na wabunge wake bungeni. Ccm inabomolewa na makada wake serikalini na ccm inabomolewa na wanasiasa wake uchwara majukwaani.

Nami nimeyasema jana haya unayoyasema leo!


Bado najiuliza kwa nini "washika mipini" (Spika, Majaji, Mwanasheria Mkuu, Mawaziri, n.k) kwa maksudi wanachukua maamuzi ya kusiliba kaburi la ccm? Hakuna hata mmoja anajifunza kutokana na makosa yake ya awali au ya mtangulizi wake!

Mghaka hii Point yako....

Kama ingekuwa siasa ni mchezo wa pointi kama ngumi sasa hivi refa wa mpambano wa wapinzani na ccm alipaswa kusimamisha mpambano kwani ccm inatoka damu kila sehemu ya uso na majeraha yamekuwa makubwa mno

Mie nili iyona kwa mtazamo huu:


...Ukiyatazama haya yote huwezi kuja na uamamuzi kama wa leo juu ya JJ Mnyika. Watoa maamuzi wa serikali yetu ya ccm lazima wajue kuwa hawa CDM ......Upya uko wapi mpaka huyo Spika anampa Mnyika kupiga penalti kwenye goli lisilo na golikipa?!
 
Last edited by a moderator:
Na hakika CCM watamwaga damu tu, hilo ndilo litakua azimio la mwisho.Naionea huruma nchi yangu kwa yatakayoikumba siku za usoni
 
Waache waendelee na nidhamu ya woga lakini mwisho wao ni hukumu ya 2015. Tunaoiombea mema nchi hii tuhakikishe tunapiga kura 2015 na kuilinda!
 
Back
Top Bottom