Hivi Michuzi ni Mtumwa wa CCM??

Nimekuwa nikifuatilia kwa kina dhidi ya issamichuzi.blogspot.com na sijawahi kuona hata mara moja ikizungumza lolote juu ya maslahi ya wananchi, wala tashuwishi mbali mbali kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu katika sekta mbali mbali za maendeleo. Hivyo ina maana hayaoni yanayotendeka au analinda ugali wake? Mawazo yangu nimefikiria ikiwa yeye ni blogger wa muda mrefu kama inavyojulikana hivyo kwa nini asichukue fursa hiyo kugombea haki za wananchi? Au anajivunia tu kwamba yeye ni blogger wa muda mrefu ila hajali wananchi wanavyoonewa,wanavyoteseka, wanavyodhulumiwa haki zao na serikali kupotosha taarifa za ukweli kwenye vyombo mbali mbali vya habari? Au anasubiria wengine ndio waandike baadae apite kwenye daraja la jasho la muhanga la waandishi wa habari majasiri? Au wadau nyinyi mnaonaje!!!
 
Alikuwa spy wa Tanzania na hii sio siri lakini sijui kuhusu CCM. Anatumiwa na watu wachache ambao wana mpa deal za hapa na pale mfano viongozi kwenye PR zao
 
Nashukuruni kwa kunijuza, hivi kuna tofauti kubwa sana kiutendaji baina ya CCM na serikali? Au ni kitu kimoja kiutendaji? Na kama tofauti ipo tufahamishane kwa mapana gani kwa maana mimi nashindwa kutofautisha kati ya serikali na CCM naona kama ni kitu kimoja hivi. Na alikuwa spy wa nini hasa? Ni mtaalamu wa upelelezi yeye au alikuwa kiraka tu? Maswali yanatirirka kichwani kwa maana sikumsikia akinung'unika juu ya ukatili aliofanyiwa Dr. Ulimboka na hatimaye Kibanga hapa majuzi na ikiwa ni wenzake katika tasnia ya habari. Hivyo haimuumi au anajionea sawa? Ebu tusaidiane kulichambua hili mwisho wa siku huenda ikasaidia asilimia kubwa ya waandishi wa habari na wahariri kuwa na nguvu juu ya sauti za wananchi na maslahi yao kwa maana media imekuwa ikificha uhalisia wa maovu uliomo nchini kwa miaka mingi sasa
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa kina dhidi ya issamichuzi.blogspot.com na sijawahi kuona hata mara moja ikizungumza lolote juu ya maslahi ya wananchi, wala tashuwishi mbali mbali kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu katika sekta mbali mbali za maendeleo. Hivyo ina maana hayaoni yanayotendeka au analinda ugali wake? Mawazo yangu nimefikiria ikiwa yeye ni blogger wa muda mrefu kama inavyojulikana hivyo kwa nini asichukue fursa hiyo kugombea haki za wananchi? Au anajivunia tu kwamba yeye ni blogger wa muda mrefu ila hajali wananchi wanavyoonewa,wanavyoteseka, wanavyodhulumiwa haki zao na serikali kupotosha taarifa za ukweli kwenye vyombo mbali mbali vya habari? Au anasubiria wengine ndio waandike baadae apite kwenye daraja la jasho la muhanga la waandishi wa habari majasiri? Au wadau nyinyi mnaonaje!!!



Halafu utashangaa anajiita mpiganaji. Huwa nami najiuliza kila kukicha, anapigania nini wakati blog yake imejaa pumba na cold propaganda kwa kulinda ugali wake. He bores me to death!
 
Blog ya michuzi ni ya habari na mipicha picha aka taswira zaidi kuliko makala. Hata kama kutakua na makala basi utakuta siyo yeye aliyeiandika bali kaletewa na mtu apost. Yeye binafsi haandiki makala, hata hivyo nimekua naona kama kuna news au picha kuhusu mtoa mada unachokiongelea huwa anaweka na comment watu wanaandika. Nafikiri hii ndo staili yake na inabidi ukubaliane naye
 
Mkuu Luali wewe ni typical Tanzanian. Ni mtu wa kulalamika tu!

Blog ni ya kwake. Hujui alipopitia hadi ikawa pale ilipo. Leo wewe unahisi yeye ni puppet wa CCM kwasababu haweki vitu unavyovitaka wewe aviweke kwenye blog yake. Hebu jifikirie mara mbili halafu uone kama unamtendea haki.

Ulitaka aweke calendar ya maandamano ya CHADEMA? Kwanini usianzishe blog yako uweke mambo yatakayokufurahisha wewe?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Sikatai kukubaliana nae, ila si wema kulinda tumbo lako ikiwa matumbo ya mamilioni ya watanzania yanaumia na kukandamizwa kama vile wapangaji kwenye nchi yao. Na ndivyo watanzania wanavyoishi yaani kama vile wamepanga kwenye nchi yao na huku wakiwa wanamuogopa mwenye nyumba bila kujua kama nyumba ni ya kwao. Kuna mengi yanajiri nchini na yanashindwa kutatulika kwa sababu watanzania wamekuwa na ubinafsi wa ajabu yaani namaanisha umimi hivyo mtu tumbo lake likishiba huwa hajali mwenye njaa. Wananchi bado hawajajua nguvu ya uhuru wa uandishi wa habari kwa maana huko ndiko kwenye mfumuko wa maendeleo kwa kuwa mengi yatajulikana katika vituo na taasisi mbali mbali za kimataifa na ndio maana maovu yanapoandikwa vituo vya redio na magazeti yamekuwa yakifungiwa hivyo maovu kushindwa kufika kwenye taasisi husika na hata research zinaishia chini ya carpet. Unadhani nini kifanyike ili wananchi wawakomboe wahariri na waandishi wa habari wawe na nguvu katika uandishi wao?
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa kina dhidi ya issamichuzi.blogspot.com na sijawahi kuona hata mara moja ikizungumza lolote juu ya maslahi ya wananchi, wala tashuwishi mbali mbali kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu katika sekta mbali mbali za maendeleo. Hivyo ina maana hayaoni yanayotendeka au analinda ugali wake? Mawazo yangu nimefikiria ikiwa yeye ni blogger wa muda mrefu kama inavyojulikana hivyo kwa nini asichukue fursa hiyo kugombea haki za wananchi? Au anajivunia tu kwamba yeye ni blogger wa muda mrefu ila hajali wananchi wanavyoonewa,wanavyoteseka, wanavyodhulumiwa haki zao na serikali kupotosha taarifa za ukweli kwenye vyombo mbali mbali vya habari? Au anasubiria wengine ndio waandike baadae apite kwenye daraja la jasho la muhanga la waandishi wa habari majasiri? Au wadau nyinyi mnaonaje!!!

Unauliza beberu la mbuzi kunuka?
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni jamani, Michuzi yuko serekalini na ni mtu wa karibu na raisi lakini habagui wala hachagui issues za kurusha kwenye blog yake. Mwenyewe anaiita 'blog ya watu' and you can see why kwasababu habari nyingi na picha analetewa na watu toka pande mbalimbali za dunia na yeye anazirusha tu. Ukitazama utaona kuna picha za matukio na habari si za CCM tu, hata CHADEMA wanarushwa wakiwa na yao. Anaweka mabandiko ya waislamu na wakristu pia, anarusha kero mbalimbali za wananchi, etc. Blog Tanzania ni moja tu, if anything happens back home najua kitakua kwa Michuzi..
 
Muheshimiwa Sumu si kwamba nampangia aandike nini ila tasnia ya uandishi ni nyeti sana na hiyo informational ndio ndimi inayotumika ili kuwafahamisha wananchi juu ya yanayoendelea nchini mwao. Na hapa siongelei U-CCM,U-CUF,U-TLP ama U-CHADEMA bali uananchi na hata hivyo inasikitisha sana mtu kutoa jasho kuhakikisha anabishana kishabiki tu bila kutafakari kwa kina kwamba wananchi wanahitaji maendeleo na mapinduzi makubwa nchini mwao, na miongoni mwa hao wananchi wamo baba zetu, mama zetu, dada zetu, wake zetu, waume zetu na hata watoto wetu hivyo tuondokane na umimi na tuwe kitu kimoja maana nchi ni yetu wote na maendeleo yatakuwa na manufaa kwetu sote. Au wewe unafurahishwa na vitendo vinavyoendelea nchini mzee? Be honest!
 
Ni blog ya burudani na habari za ccm,so kama unahitaji kujua mustakabari wa taifa nakushauri kutembelea blog kama,mnyika.blogspot.com na nyinginezo za namna hyo,lakini co michuzi ile ni blog ya kibaraka!
 
nashukuruni kwa kunijuza, hivi kuna tofauti kubwa sana kiutendaji baina ya ccm na serikali? Au ni kitu kimoja kiutendaji? Na kama tofauti ipo tufahamishane kwa mapana gani kwa maana mimi nashindwa kutofautisha kati ya serikali na ccm naona kama ni kitu kimoja hivi. Na alikuwa spy wa nini hasa? Ni mtaalamu wa upelelezi yeye au alikuwa kiraka tu? Maswali yanatirirka kichwani kwa maana sikumsikia akinung'unika juu ya ukatili aliofanyiwa dr. Ulimboka na hatimaye kibanga hapa majuzi na ikiwa ni wenzake katika tasnia ya habari. Hivyo haimuumi au anajionea sawa? Ebu tusaidiane kulichambua hili mwisho wa siku huenda ikasaidia asilimia kubwa ya waandishi wa habari na wahariri kuwa na nguvu juu ya sauti za wananchi na maslahi yao kwa maana media imekuwa ikificha uhalisia wa maovu uliomo nchini kwa miaka mingi sasa
yupi huyo?
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni jamani, Michuzi yuko serekalini na ni mtu wa karibu na raisi lakini habagui wala hachagui issues za kurusha kwenye blog yake. Mwenyewe anaiita 'blog ya watu' and you can see why kwasababu habari nyingi na picha analetewa na watu toka pande mbalimbali za dunia na yeye anazirusha tu. Ukitazama utaona kuna picha za matukio na habari si za CCM tu, hata CHADEMA wanarushwa wakiwa na yao. Anaweka mabandiko ya waislamu na wakristu pia, anarusha kero mbalimbali za wananchi, etc. Blog Tanzania ni moja tu, if anything happens back home najua kitakua kwa Michuzi..
Kwa mujibu wa maelezo yako it means anabagua baadh ya vyama kama vile NRA,TLP,DP maana huwa hatoi taarifa zake
 
Ni blog ya burudani na habari za ccm,so kama unahitaji kujua mustakabari wa taifa nakushauri kutembelea blog kama,mnyika.blogspot.com na nyinginezo za namna hyo,lakini co michuzi ile ni blog ya kibaraka!

Nashukuru kwa ushauri pia, na ndipo hapo niliuliza hapa kwenye thread iliyopita ya kwamba je anasubiria wenzake wajitoe muhanga ili atumie ujasiri wa waandishi wengine? Nakubaliana na wewe kwamba ni kibaraka na ndio maana akajitoa kutetea haki za wananchi badala yake kuweka mapicha picha tu na kama yeye angebadili mfumo wa blog yake ingekuwa na manufaa kwa wananchi kwa maana wananchi wanahitaji sauti yao ipenye kupitia kila kona ili mwisho wa siku tupate Tanzania isiyo na matabaka, udini wala mgawanyiko wa elimu,kipato, matibabu ama nafasi za kimaendeleo
 
mhhh mada zingine bana, yaani unauliza swali na kujijubu hapo hapo, dah! job true true
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni jamani, Michuzi yuko serekalini na ni mtu wa karibu na raisi lakini habagui wala hachagui issues za kurusha kwenye blog yake. Mwenyewe anaiita 'blog ya watu' and you can see why kwasababu habari nyingi na picha analetewa na watu toka pande mbalimbali za dunia na yeye anazirusha tu. Ukitazama utaona kuna picha za matukio na habari si za CCM tu, hata CHADEMA wanarushwa wakiwa na yao. Anaweka mabandiko ya waislamu na wakristu pia, anarusha kero mbalimbali za wananchi, etc. Blog Tanzania ni moja tu, if anything happens back home najua kitakua kwa Michuzi..

Muheshimiwa naona tafiti zako zina walakini kwa maana hakuna makala kwenye blog ya Michuzi iliyokuwa ikijadili kuhusiana na haki za wananchi, kina mama, watoto na hata walimu, madaktari, wanafunzi,afya, wanawake na ajira na kama zipo tuletee links hapa ili tuende sawa kwa maana majadiliano haya ni manufaa kwetu na ndugu zetu watanzania na si kuzungumza vitu visivyobebwa na tafiti sahihi. Na pia anapoweka hizo picha za Chadema ama CCM kama unavyodai pia inategemeana zina uzito gani juu ya hayo mambo ya msingi dhidi ya wananchi. Sikatai aweke entertainment ila narudia tena sekta ya uandishi na habari ni sekta nyeti sana hivyo inahitaji uwazi na ujasiri na si kuyafumbia macho yale yanayoweza kuyakomboa wananchi
 
Back
Top Bottom