Hivi kwenda bar au club ni uhuni???

Tabai ya kwenda Club na bar ndiyo iliyosababisha mchumba wake wa awali amuache.
Tabia ya kwenda bar au club si uhuni, ila jamii inachukulia ni uhuni kwani mwisho wa starehe huko bar au club ni matendo ya kihuni.
Upande wa pili hii ni tabia tegemezi, ukianzasha tu kwenda club ni vigumu kuacha tabia hii. Hata kama utakosa pesa, utatafuta tu ili weekend uende club.

Kwa sababu hiyo hapo kwa red, ndo maana utakuta wanaume wengi hawaoi wanawake wanaoenda nao club au bar. Watapeana tu kampani huko lakini mwisho wa siku mwanaume anaingia mitini, anatafuta mwanamke mwingine wa kuoa.

Binafsi huwa nawashauri wanawake/wasichana wanaotaka kuolewa waepuke kwenda maeneo hayo, unless umeishakata tamaa ya kuolewa. Otherwise, ni vizuri kwenda na mumeo kama ni obi yako.
 
Kwa sababu hiyo hapo kwa red, ndo maana utakuta wanaume wengi hawaoi wanawake wanaoenda nao club au bar. Watapeana tu kampani huko lakini mwisho wa siku mwanaume anaingia mitini, anatafuta mwanamke mwingine wa kuoa.

Binafsi huwa nawashauri wanawake/wasichana wanaotaka kuolewa waepuke kwenda maeneo hayo, unless umeishakata tamaa ya kuolewa. Otherwise, ni vizuri kwenda na mumeo kama ni obi yako.
Pamoja saana!!!!!!!!!!
 
Kama walivyosema baadhi, uhuni si kuenda bar/club bali ni lile mtu analofanya, iwe ni bar/club, kanisani/msikitini, arusini/msibani n.k.

Ama kuhusu tafsiri ya neno uhuni, ni dhahania, kila mtu anaweza kulifahamu kivyake. Mfano, hata msichana kutembea (kutoka kwa matembezi) na mchumba kwa wengine uhuni wakati wazazi wameliridhia, na kinyume chake.
 
Kwa sababu hiyo hapo kwa red, ndo maana utakuta wanaume wengi hawaoi wanawake wanaoenda nao club au bar. Watapeana tu kampani huko lakini mwisho wa siku mwanaume anaingia mitini, anatafuta mwanamke mwingine wa kuoa.
Hapa nahisi tunarejea kule kule kwa Enzi za Giza - jambo likifanywa na msichana ni uhuni na hilo hilo likifanywa na mvulana, huo ndio udume wenyewe.

Hapo kwenye Italics - Unahisi hao wanaojifungia/fungiwa ndani ni watawa? Ndio maana wengi wanauziwa "mbuzi guniani."
 
Ulaya, America na nchi zolizo juu watu wanaenda Bar kupata kahawa tu saa zingine, hat wakuu wa dini pia, huku ujingani kwenye vichochoro vya dunia ni Ujinga unaotumaliza.
 
Hapa nahisi tunarejea kule kule kwa Enzi za Giza - jambo likifanywa na msichana ni uhuni na hilo hilo likifanywa na mvulana, huo ndio udume wenyewe.

Hapo kwenye Italics - Unahisi hao wanaojifungia/fungiwa ndani ni watawa? Ndio maana wengi wanauziwa "mbuzi guniani."

Uko sahihi kabisa MAMMAMIA, lakini kumbuka kwamba these things are embedded in our culture, and it's always difficult to change the culture, you need time and patience to be able to do that. So you have got to blend yourself into a particular culture. Vinginevyo utaishia kuchukia wanaume wote wakati kumbe wewe mwenyewe ndo unakinzana na utamaduni wa society husika
 
kwangu mimi sioni uhuni mimi na mchumba wangu tumelogwa na club haipiti weekend bila kwenda club ingawa hatukukutana club kwangu hata nikifikisha 50 yrs nitakuwa naenda club siangalii mtasema nini. nakumbuka nilishaenda nchi za wenzetu mara ya kwanza kuingia club nilishangaa sana nilikuwakuta age kuanzia 18 mpka 70 yrs wana have a fun. uhuni inategemea na wewe mwenyewe unaweza kuwa mtu mzuri sana kufundisha bible ila ukawa mzizi sana wa wake za watu. kwa nje watu wanakuona wa maana sana kumbe umeoza na mitabia yako ya kishetani, so do most which make you happy in your life usijibanie kwa kuwaangalia watu au watakusema vip bora usile cha mtu na usifanye vitendo vya kishetani kwa kugongwa gongwa au kugonga gonga wenzako na mengine ambayo unahisi hayafai, vaa unavyotaka kutokana na mahali uhusika iwe club, kanisani, harusini, msibani nk maisha yanaenda jipe raha mkuu acha kabisa kusikiliza watu wanafiki.
 
usiende mwaya,wengi baadae mnawaletea shida spouse wenu kwa mazoea mliyojijengea,tembelea wagonjwa na marafiki in your spare time....:sleepy:
 
Uko sahihi kabisa MAMMAMIA, lakini kumbuka kwamba these things are embedded in our culture, and it's always difficult to change the culture, you need time and patience to be able to do that. So you have got to blend yourself into a particular culture. Vinginevyo utaishia kuchukia wanaume wote wakati kumbe wewe mwenyewe ndo unakinzana na utamaduni wa society husika
mito Mkuu, si kila jambo lililomo katika utamaduni ni zuri na linapaswa kuendelezwa, hasa ikiwa "utamaduni" huo ni wa kuwadharau, kuwatenga, kuwanyanyasa na kuwazuwia wengine haki zao za msingi, bila ya kujali mipaka ya kijinsia. For example, if that thing "embedded" in the culture is FGM (Female Genital Mutilation), would you still be abided to such a culture, just because our forefarthers used to do it?

I agree with you that we can't change a culture as we change our clothes, but there must be someone to "bell the cat," to say ENOUGH!
 
Last edited by a moderator:
Ili tuweze kutoa majibu sahihi, tuwe na base moja ya ku-hinge arguments zetu. Let first define what is uhuni, then from there we will reach a valid conclusion. For example if I ask you: Is a whale a fish? You will first have define what are the characteristics of a fish and a whale -define the two terms!

Define sasa mbona umetuachia sie tena
 
charminglady, majibu yote A na B ni sawa kwani inategemea na situation, kwanza club au bar ni sehemu za kujifurahisha na kujichanganya na watu mbalimbali (hii ni sifa mojawapo ya binadamu yoyote), hivyo basi kwenda kule si uhuni so long hakuna kinachomzuia kwenda huko but inakuwa uhuni pale ambapo anamkimbia partner wake na kwenda kujirusha na wadau wengine huku akidanganya yupo nyumbani amelala but akimweleza ukweli hapo si uhuni.
 
Last edited by a moderator:
Huyu aliyeleta mada a-define uhuni-atuonyeshe kwa uhuni alikuwa anamaanisha nini, then tukikubali definition yake, we join the discussion, if we dont agree with his/her discussion we will find a compromise to what uhuni is! and start discussing
Uhuni hauna tafsiri moja kwa sababu ni suala linalotokana na matendo na tabia, wakati na mazingira; kwa hivyo huwezi kuwaridhisha au kuwachukiza wote. Unaliona wewe ni la kistaarabu mimi ninaweza kuliona la kihuni na kinyume chake.
 
Uhuni hauna tafsiri moja kwa sababu ni suala linalotokana na matendo na tabia, wakati na mazingira; kwa hivyo huwezi kuwaridhisha au kuwachukiza wote. Unaliona wewe ni la kistaarabu mimi ninaweza kuliona la kihuni na kinyume chake.

Uko sahihi kabisa. ndio maana hatuwezi kuchangia hoja hii tukapata muafaka maana lazima kwanza tukubaliane uhuni ni nini. We should define the term first! and agree to it
 
mito Mkuu, si kila jambo lililomo katika utamaduni ni zuri na linapaswa kuendelezwa, hasa ikiwa "utamaduni" huo ni wa kuwadharau, kuwatenga, kuwanyanyasa na kuwazuwia wengine haki zao za msingi, bila ya kujali mipaka ya kijinsia. For example, if that thing "embedded" in the culture is FGM (Female Genital Mutilation), would you still be abided to such a culture, just because our forefarthers used to do it?

I agree with you that we can't change a culture as we change our clothes, but there must be someone to "bell the cat," to say ENOUGH!

Kutokana na mfano wako uliotoa, naona kama hujanielewa ndg yangu MAMMAMIA. Ninachojaribu kusema hapa ni kwamba kuishawishi jamii ijue kuwa FGM ina madhara ni rahisi zaidi kuliko kuishawishi jamii hiyo hiyo iamini kuwa wasichana wanaenda disco, bar, club n.k si wahuni. Kwahiyo kwa kuzingatia hili, ndo maana nashauri hivi kwa msichana/mwanamke anayetaka kuolewa ni vizuri asifanye kile ambacho sehemu kubwa ya jamii inaamini ni kibaya. This is my major argument!
 
Back
Top Bottom