Hivi kwanini wanawake wa kitanzania huwa hawapendi kula viporo?

Chakula kilicho hifadhiwa kwenye friji hakina madhara kiafya. Unaki microwave kukipasha moto, mlo safi tu.
 
Fanya hivi nunua bonge la jogoo leta home mwambie mwenzio amkaange au atengeneze makange. Kwa kuwa watu wawili hamuwezi kumaliza jogoo kitakacho baki asubuhi mwambie akatupe maana ni kiporo uone kama atatupa...
 
Kwa Nn msipike chakula kinachotosha kwa wakati/siku hiyo mnakula mnamaliza, mambo ya kulazalaza misosi ndg yangu unataka viumbe visivyoonekana vichezee ule tena, Ndiyo maana mnajambajamba, mnazeeka haraka, vimbiwa na kusinzia/kuchoka hovyo virutubisho vyote vinakwisha. Lkn pia ni hatari kula kiporo coz unaweza kuwekewa sumu. Pika kidogo kula maliza mara nyingine mnapika tena.
Mafriji yana kazi gani?
 
Majidai hayafai. Hao kina dada ndio wanaopika chakula kingi na matokeo yake kinabaki, halafu wanashindwa kukila pindi kinapolala. Hiyo ni dhambi na ukumbuke kuna watu wanakitafuta na hawakipati!
 
Kiporo nimekula na bado nakula sana tu.
Siku hizi kuna baadhi ya viporo sili mana tumbo langu si zuri so vile ambavyo havinisumbui napiga kama kawa.
Ila muda mwingine malezi pia yanachangia coz nilikuwa na rafiki yangu ila yeye alikuwa anasema hali kiporo mana nyumbani kwao hata kama ni wali wanamwaga nikawa namshangaa.
Ila nilimsema mpaka akakiri kuwa sio vizuri kumwaga chakula akaanza kula au anapika kinachotosha
 
Kwanini unajua idadi ya watu wanaokula chakula na unajua kiasi chao wanachokula halafu unapika chakula kingi mnakula kina baki, huu ni uharibifu na ujinga kutupa chakula
 
Viporo vya wali na ugali tu ndio hawali.
Ila viporo vya ndizi nyama mbona hawakatai.
Yf alishanileteaga hiz swaga ila hata sijui what is happening maana sikulipaga attention hilo suala mpaka leo.Sasa sijui hali kwel au anakula maana sijawah kufuatilia.Lakin mm nakula sana..
 
Sema viporo navyo vina mabalaa sana.Nakumbuka miaka flan nikiw std 5 pale ilala primary Iringa niliaibika sana kwasababubya hiz viporo.Tumegonga kiporo cha ugali na majani ya maboga asbh tukaelekea shulen.Inafika saa 3 brother akaumwa tumbo la ghafla akatapika kwel kwel yan.Sasa kucheknhiv ni vipande vya ugali tu na majani ya maboga.Teacher mmoja wa kuitwa Mwanjisi (r.i.p) akanipiga madongo kwel mbele ya darasa halaf akanmbie nimrudishe bro home."acheni kula viporo asbh" basi darasa zima ni vicheko na sie ikawa full aibu..duh..viporo achen tu wadada wavikatae.
 
Hujui utamu wa kiporo cha wali kisanvu au wali maharagwe,,,,,, yaani mimi nisile kiporo????
 
Back
Top Bottom