Hivi kwanini wanawake wa kitanzania huwa hawapendi kula viporo?

Hapo inategemea na mazingira ya kila mwanamke unaweza kuta mwingine kwao hawana tabia ya kuacha msosi wengine ukibaki au unaachwa kwa ajili ya kesho hio ni kawaida tuuu
 
Hakuna anaependa kula kiporo sema tu ugumu wa maisha unachangia
 
Kama mtu hawez kula kiporo kwann aspike chakula chakulika usiku tu na kikaisha kulko kupika chakula kingi alf asubuh unamwaga simpo tuu.... Sipend mtu anaemwaga chakula mim jamani ni dhambi.... HULI AU HUWEZ KIPORO PIKA CHAKULA KIISHE... MUNGU ANAWAONA
 
kwenye midomo

Mdomo au midomo, mtu akisema lips zio lazima iwe midomoni, lips inaweza ikawa upper lip na lower lip.
Back to question, namaanisha mkoa upi hizo lips zinapatikana, nataka kuzichum, hata zikiwa na mabaki ya viporo
 
Mdomo au midomo, mtu akisema lips zio lazima iwe midomoni, lips inaweza ikawa upper lip na lower lip.
Back to question, namaanisha mkoa upi hizo lips zinapatikana, nataka kuzichum, hata zikiwa na mabaki ya viporo
 
Hawajui utamu wa viporo hao yaan siku wapate kiporo cha wali na maharage na chai iliyotiwa viungo vyote mbona watajilaumu siku zote walikua wap...Nakumbuka boyfriend wang alikua hali kiporo eti anaogopa tumbo litamuuma nikamwambia wala sio kwel nikakipasha moto kiporo changu pale tukala vzur hajaumwa tumbo wala nn tangu siku ile n mlaj kiporo mzur sanaaa
 
Ukiwa mjamzito wataalam wanahamasisha kutokula viporo
Ndio, tena unasisitiziwa clinic kuwa usijaribu kula kiporo maana wakati wa kujifungua lazima ujisaidie haja kubwa.
Sasa sijui kuna uhusiano gani....japo kweli huwa inayokea kujisaidia.

Sasa nikijisaidia si watajua nilikuwa natoa ndogo?
 
Kwema wakubwa?

Kuna hii ishu huwa inanishangaza sana, ni kuhusu wanawake wa kitanzania kutopenda kula msosi uliolala{kiporo}, hii ishu nimekua nikiiobserve toka kipindi nikiwa naishi nyumbani, dada zangu pamoja na mama walikuwa huwezi kuwalisha kiporo cha chakula chochote kile, mwanzo nikawa nahisi hawa labda wanaleta pozi coz wanajua vipo tu na wala hawajui mzee anavyohangaika kuvipata lakini mpaka leo wamekua watu wazima wanaojitegemea hawali kitu kinachoitwa kiporo kabisa.

Sasa nina mpenzi wangu nae naona anataka kunitia umasikini mchana kweupe coz nae ana tabia hizo, yani juzi kati kaja gheto kapika ubwabwa na tambi, sasa ule msosi uliobaki si tunatakiwa tuule asubuhi au mchana ya kesho yake coz tunakua tumeuhifadhi vizuri, mwenzangu yeye kaamka kaumwaga jalalani, kumuuliza ananijibu simple tu kuwa yeye halagi viporo hivyo akajua na mie silagi, pia wakati niko nasoma nilikuwa nasikia wadada wengi wakisema kuwa kwao ni mwiko kula viporo vya msosi wowote. Sasa nilitaka kujua hivi ni kwa nini hawa wanawake wa kitanzania hawalagi viporo?
Mkuu huyo mpenzi wako kwao mambo safi? Maana hawa ndugu zetu sikuhizi maisha ya tamthilia yamewaathiri sana.
 
Back
Top Bottom