Quemu
JF-Expert Member
- Jun 27, 2007
- 984
- 128
Hivi kwa nini tunaendekeza sana imani za kishirikina?
Yaani imefikia hali ambayo hatuwezi kufanya chochote au kukubali matokeo yoyote bila kuhusisha imani za kishirikina. Maneno uchawi na ushirikina yametukaa sana midomoni mwetu. Haipiti siku bila kujikuta kwenye maongezi yahusuyo imani za kishirikina (uwe ni mshiriki wa maongezi au mpita njia tu mwenye masikio makubwa).
Nakumbuka miaka ya utoto wangu, ilikuwa ni kawaida kuvizia chakula kwa jirani. Ukijua ratiba ya nyumbani ni ugali maharage, basi unasogea kwa jirani kutaka kujua ratiba ya msosi ya kwao. Kama ya kwao ni mzuri, basi siku mzima utashinda kwao. Siku hizi watoto kula kwa jirani ni mwiko. Well, hata zamani ilikuwa ni mwiko. Lakini sababu ya zamani ilikuwa ni "tabia mbaya kula kwa watu." Siku hizi sababu ni "huwezi jua jirani ameweka nini kwenye chakula." Majirani hawaaminiki tena.
Siku hizi ni mwiko kwa mtu yoyote (isipokuwa ndugu wa karibu sana) kumfunga khanga kiunoni bibi harusi. Kisa? Eti kuna hofu kuwa wengine wanakuja na kanga zilizowekwa ‘mambo' ya kufunga kizazi. Mke wa rafiki yangu mmoja alipokuwa mjamzito, mama yake alihakikisha anamnunulia khanga mpya kabisa, na kumkataza asizivae zile khanga za zamani. Kisa? Eti kunaweza kuna na khanga zilizofanyiwa ‘mambo' kutaka kumdhuru mtoto ingali bado tumboni.
Siku hizi wafiwa wanahakikisha kwenye shughuli za uoshaji wa mwili wa marehemu ni lazima kuwe na mtu ambaye kazi yake ni kuhakikisha hakuna mwoshaji yoyote anayenyofoa kiungo cha marehemu. Kisa? Eti watu huwa wanatabia ya kunyofoa viungo vya marehemu na kupeleka wa wanganga wao au hata kwenda kuviuza.
Yaani tunaendekeza na kuogopa ushirikina kiasi kwamba hatuwezi tena kuwa huru kufanya chochote tukiwa na amani moyoni. Siku hizi hakuna matokeo mabaya yasiyohusishwa na imani za kishirikina. Inasikitisha. Nahisi hata hao ‘waitwao washirikina' wamefikia wakati hata hawapotezi ‘resources' zao tena. Wanachofanya ni "kubwaka tu…..bila ya kung'ata." I mean, kama ukitishia unapishwa njia, kwa nini utumie raslimali zako pasipo sababu?
- Umefukuzwa kazi kwa sababu ya uzembe - unamtafuta mchawi wako
- Mmejaribu kwa miaka kadhaa kupata mtoto bila ya mafanikio - lazima kutakuwa na mtu kawafunga kizazi.
- Mwanao alikuwa anafanya vizuri darasani, lakini ghafla performance imeshuka – kuna mtu amemroga.
- Biashara yako imedorora, lakini ya jirani yako imechanganya – jirani mchawi
- Jamaa kakolea ile mbaya kwa mpenzi/mke wake – si bure, kawekewa limbwata au kaendewa kwa mganga
- Unataka utajiri wa haraka haraka – tafuta kiungo cha Albino
- Na kadhalika, na kadhalika
Yaani imefikia hali ambayo hatuwezi kufanya chochote au kukubali matokeo yoyote bila kuhusisha imani za kishirikina. Maneno uchawi na ushirikina yametukaa sana midomoni mwetu. Haipiti siku bila kujikuta kwenye maongezi yahusuyo imani za kishirikina (uwe ni mshiriki wa maongezi au mpita njia tu mwenye masikio makubwa).
Nakumbuka miaka ya utoto wangu, ilikuwa ni kawaida kuvizia chakula kwa jirani. Ukijua ratiba ya nyumbani ni ugali maharage, basi unasogea kwa jirani kutaka kujua ratiba ya msosi ya kwao. Kama ya kwao ni mzuri, basi siku mzima utashinda kwao. Siku hizi watoto kula kwa jirani ni mwiko. Well, hata zamani ilikuwa ni mwiko. Lakini sababu ya zamani ilikuwa ni "tabia mbaya kula kwa watu." Siku hizi sababu ni "huwezi jua jirani ameweka nini kwenye chakula." Majirani hawaaminiki tena.
Siku hizi ni mwiko kwa mtu yoyote (isipokuwa ndugu wa karibu sana) kumfunga khanga kiunoni bibi harusi. Kisa? Eti kuna hofu kuwa wengine wanakuja na kanga zilizowekwa ‘mambo' ya kufunga kizazi. Mke wa rafiki yangu mmoja alipokuwa mjamzito, mama yake alihakikisha anamnunulia khanga mpya kabisa, na kumkataza asizivae zile khanga za zamani. Kisa? Eti kunaweza kuna na khanga zilizofanyiwa ‘mambo' kutaka kumdhuru mtoto ingali bado tumboni.
Siku hizi wafiwa wanahakikisha kwenye shughuli za uoshaji wa mwili wa marehemu ni lazima kuwe na mtu ambaye kazi yake ni kuhakikisha hakuna mwoshaji yoyote anayenyofoa kiungo cha marehemu. Kisa? Eti watu huwa wanatabia ya kunyofoa viungo vya marehemu na kupeleka wa wanganga wao au hata kwenda kuviuza.
Yaani tunaendekeza na kuogopa ushirikina kiasi kwamba hatuwezi tena kuwa huru kufanya chochote tukiwa na amani moyoni. Siku hizi hakuna matokeo mabaya yasiyohusishwa na imani za kishirikina. Inasikitisha. Nahisi hata hao ‘waitwao washirikina' wamefikia wakati hata hawapotezi ‘resources' zao tena. Wanachofanya ni "kubwaka tu…..bila ya kung'ata." I mean, kama ukitishia unapishwa njia, kwa nini utumie raslimali zako pasipo sababu?
Last edited by a moderator: