Kwa kawaida hakuna mahusiano yanayokosa changamoto hata kama mpo ndani ya ndoa, vikombe kabatini tu vinagongana sembuse binadamu wawili waliokutana ukubwani na wote wakiwa na meno 32.
Huwa inatokea kuna wakati mnafurahia sana mapenzi yenu lakini pia kuna wakati shetani anaingilia kati na kuanza kuwabadirisha.
Kwa wale ambao hawapo ndani ya ndoa na kila mtu anaishi kwake silaha kubwa kabisa ya mahusiano ni mawasiliano mana bila mawasiliano hakuna mapenzi.
Kuna kipindi mawasiliano kati yenu yanaanza kuwa hafifu yani kama mlikua mnawasiliana asubuhi mchana na jioni mnajikuta kwa siku mnawasiliana tu mara moja tena sms hazijibiwi kwa wakati, yaani unatuma sms saa moja asubuhi lakini mwenzi wako anakuja kuijibu saa saba mchana kwa kisingizio tu kwamba alikua busy.
Kuna msemo unasema no one is busy, it depends on the priority.Kwako anaweza akawa busy lakini kuna mwenzako anasumbuliwa na sms mpaka anaona kero.
Inapotokea hali ya namna hii ewe dada ewe kaka fanya yafuatayo;
1. Kaa chini na mwenzi wako muulize kuna tatizo gani mpaka mawasiliano yenu yameyumba na hayapo kama zamani, mana inawezekana ukamuelewa vibaya kumbe mwenzi wako ana tatizo linamsibu ambalo huenda ungemsaidia hata kwa ushauri.
2. Kama atakuambia hakuna tatizo ni ubize tu wa hapa na pale basi yakupasa umueleze wazi kwamba hufurahishwi na hiyo hali na unahitaji kuona mabadiriko kwenye mawasiliano, ubize wa mwanamke au mwanaume unaweza ukawa wa kweli au sio kweli na mara nyingi hutokea pale ambapo either mwanamke ameanza kutongozwa na njemba mpya au mwanaume amepata namba ya mwanamke mpya kwahiyo muda mwingi anautumia kuwasiliana na huyo mtu mpya.
3. Ukishamkanya mara mbili au mara tatu kwa siku tofauti tofauti na ukiona anarudia yaleyale uliyomkataza basi hiyo inatosha sana, huna sababu ya kuendelea kila siku kumkumbusha wajibu wake.Hizo zinakua ni red flags za waziwazi.
4. Kwakua umemuonya na hataki kubadirika basi wewe nenda vile anavyotaka yeye, kama umemtumia ujumbe saa 2 asubuhi na akaja kuujibu saa 10 jioni wewe wale usihoji na badala yake mjibu tu vizuri lakini usioneshe tena kukasirishwa na hilo suala.
5. Wanaume kila siku tunatongoza na wanawake kila siku wanaombwa namba za simu na wanatongozwa pia, shida ni kwamba mwanamke au mwanaume hawezi kukuambia waziwazi kwamba tuvunje mahusiano mana anakua hajiamini kama huyo aliemkubalia ni mtu sahihi kwake kama ulivyo wewe au la.
Mara nyingi watu wana tabia ya kulinganisha kwamba je huyu na yule tofauti yao ni nini, kuna mwanaume unakuta ana kila kitu lakini kawapanga wanawake zaidi ya 20 na kiasi kwamba kwa mwanamke anaehitaji mtu serious kwenye mahusiano hawezi kudumu nae na badalaa yake atarudi mbio kwa mtu wake wa awali.
5. Usiwe mtu wa kuombaomba msamaha kila mara kwa mwenzi wako hata kwa kosa ambalo unajua hukufanya mana kwa kufanya hivyo ni kama unapandisha 'ego' yake.
Mbio za sakafuni siku zote huishia ukiongoni mana mwanamke au mwanaume anaweza akampata mwenzi mpya ilhali yupo kwenye mahusiano lakini mwisho wa siku anakuja kugundua kumbe wewe ni bora kuliko huyo aliempata.
Mwanamke anaweza akawa mzuri sana lakini akawa anachukulika kirahisi na kila anayemtongoza vilevile kiasi cha thamani yake kushuka na pia mwanaume anaweza akawa na kila kitu pesa, nyumba na gari zuri la kutembelea lakini unakuta ana wanawake wengi kupita kiasi anawatumia tu na hana mpango wa kuoa hata mmoja.
Kwa leo naomba niishie hapa ila zingatia sana hizo nondo zangu 5 hapo juu na jifunze kusoma mabadiriko ya mwenzi wako, sio kila kila jambo ni la kupuuzia.
Huwa inatokea kuna wakati mnafurahia sana mapenzi yenu lakini pia kuna wakati shetani anaingilia kati na kuanza kuwabadirisha.
Kwa wale ambao hawapo ndani ya ndoa na kila mtu anaishi kwake silaha kubwa kabisa ya mahusiano ni mawasiliano mana bila mawasiliano hakuna mapenzi.
Kuna kipindi mawasiliano kati yenu yanaanza kuwa hafifu yani kama mlikua mnawasiliana asubuhi mchana na jioni mnajikuta kwa siku mnawasiliana tu mara moja tena sms hazijibiwi kwa wakati, yaani unatuma sms saa moja asubuhi lakini mwenzi wako anakuja kuijibu saa saba mchana kwa kisingizio tu kwamba alikua busy.
Kuna msemo unasema no one is busy, it depends on the priority.Kwako anaweza akawa busy lakini kuna mwenzako anasumbuliwa na sms mpaka anaona kero.
Inapotokea hali ya namna hii ewe dada ewe kaka fanya yafuatayo;
1. Kaa chini na mwenzi wako muulize kuna tatizo gani mpaka mawasiliano yenu yameyumba na hayapo kama zamani, mana inawezekana ukamuelewa vibaya kumbe mwenzi wako ana tatizo linamsibu ambalo huenda ungemsaidia hata kwa ushauri.
2. Kama atakuambia hakuna tatizo ni ubize tu wa hapa na pale basi yakupasa umueleze wazi kwamba hufurahishwi na hiyo hali na unahitaji kuona mabadiriko kwenye mawasiliano, ubize wa mwanamke au mwanaume unaweza ukawa wa kweli au sio kweli na mara nyingi hutokea pale ambapo either mwanamke ameanza kutongozwa na njemba mpya au mwanaume amepata namba ya mwanamke mpya kwahiyo muda mwingi anautumia kuwasiliana na huyo mtu mpya.
3. Ukishamkanya mara mbili au mara tatu kwa siku tofauti tofauti na ukiona anarudia yaleyale uliyomkataza basi hiyo inatosha sana, huna sababu ya kuendelea kila siku kumkumbusha wajibu wake.Hizo zinakua ni red flags za waziwazi.
4. Kwakua umemuonya na hataki kubadirika basi wewe nenda vile anavyotaka yeye, kama umemtumia ujumbe saa 2 asubuhi na akaja kuujibu saa 10 jioni wewe wale usihoji na badala yake mjibu tu vizuri lakini usioneshe tena kukasirishwa na hilo suala.
5. Wanaume kila siku tunatongoza na wanawake kila siku wanaombwa namba za simu na wanatongozwa pia, shida ni kwamba mwanamke au mwanaume hawezi kukuambia waziwazi kwamba tuvunje mahusiano mana anakua hajiamini kama huyo aliemkubalia ni mtu sahihi kwake kama ulivyo wewe au la.
Mara nyingi watu wana tabia ya kulinganisha kwamba je huyu na yule tofauti yao ni nini, kuna mwanaume unakuta ana kila kitu lakini kawapanga wanawake zaidi ya 20 na kiasi kwamba kwa mwanamke anaehitaji mtu serious kwenye mahusiano hawezi kudumu nae na badalaa yake atarudi mbio kwa mtu wake wa awali.
5. Usiwe mtu wa kuombaomba msamaha kila mara kwa mwenzi wako hata kwa kosa ambalo unajua hukufanya mana kwa kufanya hivyo ni kama unapandisha 'ego' yake.
Mbio za sakafuni siku zote huishia ukiongoni mana mwanamke au mwanaume anaweza akampata mwenzi mpya ilhali yupo kwenye mahusiano lakini mwisho wa siku anakuja kugundua kumbe wewe ni bora kuliko huyo aliempata.
Mwanamke anaweza akawa mzuri sana lakini akawa anachukulika kirahisi na kila anayemtongoza vilevile kiasi cha thamani yake kushuka na pia mwanaume anaweza akawa na kila kitu pesa, nyumba na gari zuri la kutembelea lakini unakuta ana wanawake wengi kupita kiasi anawatumia tu na hana mpango wa kuoa hata mmoja.
Kwa leo naomba niishie hapa ila zingatia sana hizo nondo zangu 5 hapo juu na jifunze kusoma mabadiriko ya mwenzi wako, sio kila kila jambo ni la kupuuzia.