Hivi hawa wanaishiaga wapi?

Nimeleta hii mada baada ya Kushtushwa na mdogo wangu mmoja aliponiambia the way wanavyofundishwa Kingereza

Jamani watoto siku hizi wanakaririshwa hata Kingereza? Imagine Mwalimu anawapa Mbinu wanafunzi kwamba

Katika Mtihani Ukiona If basi jawabu lake ni then kama ukiona Whom basi jibu lake ni You yaani kuna formula za namna ya Kujibu maswali ya Kingereza siku hizi!

Sasa najiuliza Tatizo liko wapi?

Walimu hawaandaliwi Vizuri au hawana knoledge ya kile wanachopaswa kufundisha au Wanafunzi wanasukumwa kutoka Primary kwenda Secondary!

Ni wapi makosa yamefanyika jamani kwa maana the situation is worse than what someone can imagine

Walimu sio wa kulaumiwa peke yao hapa. Consensus inasema kwamba elimu ya mtoto ni 30% Mwalimu, 30% Mzee, 30% Mtoto mwenyewe, na 10% ni bahati. Kwa hiyo wote hapa wanastahili lawama. Binafsi nafikiri wazee wetu wabebeshwe lawama zaidi kwa vile wengi hawajihusishi na elimu za watoto wao katika kiwango chochote. Katika jamii nyingi zenye wakali kama vile wahindi, wayahudi, wachina utaona wazee wao wanajihusisha sana na harakati za kila leo kuwasaidia watoto wao kufanikiwa kimasomo.

Kwa kweli hizo statistics za matokeo ya form IV haziko tofauti sana na nchi nyini za KiAfrica ukizivunja kwenye points. Labda ndio mila yetu waafrika kutegemea walimu kama ni walezi pia. Kama vile "Mwalimu" Nyerere alikuwa baba yetu wa Taifa. Alipofariki tumekuwa mayatima
icon10.gif

¬K
 
Back
Top Bottom