Escobar
JF-Expert Member
- Sep 16, 2011
- 574
- 440
Honestly sehemu kubwa ya wabunge wa CDM imeshiba vibaya kwa kujenga na kuwasilisha hoja zenye mguso wa kipekee kwenye jamii. Ni dakika chache tu Mh. Wenje alikuwa anamwaga facts kuhusu elimu yetu ya shule ya msingi kuwa mtaala unaelekeza kuwa lugha ya kufundishia ni kiswahili wakati wakati huo viongozi wote wa serikali wasomesha watoto wao kuanzia nursery kwenye shule zinazotumia kiingereza kama lugha ya kufundishia! Watu wamekuwa wakiomba mabadiliko katika hili lakini serikali inakataa kuwa kiswahili ndio lugha ya taifa hivyo lazima kiendelee! La pili alilonikosha zaidi ni kwanini wanajeshi wanapewa nafasi ya kununua vitu kwenye maduka yao ambapo wanapata punguzo la bei kwa kuondolewa baadhi ya kodi na wao wanamshahara mikubwa kuliko walimu, kwanini basi na walimu wasifanyiwe hivyo ili nao wapate japo vifaa vya ujenzi kwa bei poa?
This makes sense for sure!
This makes sense for sure!