Bana likasi
JF-Expert Member
- Jan 7, 2020
- 6,927
- 6,417
Rubbish.mnapowaapisha kwann mnatunyesha liveNimemsikiliza mtani akiongea kuhusu barua waliyomwandikia mkuu wa nchi. Japo alijisahau mara kadhaa akisema "niliyo mwandikia"! Nafsi inanituma niamini kaandika yeye hakushirikisha wenzake. Lakini hilo sio tatizo! Tatizo haswa ni pale alipoulizwa je ikiwa hatajibiwa atafanyaje?
Ndipo ushetani ulipojichomoza! Alijibu kuwa yeye keshamkabidhi mkuu barua atake au asitake kujibu wanamuachia yeye. Swadakta tawile! Na akaulizwa tena je amempa mkuu deadline ya kujibu? Akajibu kuwa si heshima kumpangia mkuu wa nchi muda wa kujibu. Swadakta tawile!
Lakini ushetani ni huu: kama kweli ameamua kumuachia mkuu wa nchi uamuzi wa kujibu au kutojibu na akaheshimu asimpangie muda wa kujibu iweje akaisome barua hadharani?
Ni heshima sampuli gani hii? Imemuongezea nini kwa kuisoma barua hadharani? Sasa hii barua kamwandikia raisi au katuandikia sisi wote? Ni barua ya raisi tena? Kwa nini raisi aijibu wakati waliopelekewa hii barua tuko wengi sasa?
Katika hotuba yake alidai yeye ni mkubwa sana hawezi kujibizana na mtu mdogo kama DC wa Hai! Lakini ajue wakati anatusomea barua na DC wa Hai naye alikuwa msikilizaji? Naye anaweza kumjibu.
Hivi chadema wanajua maana ya BARUA YA SIRI? Confidential Letter! Hii si ingestahili kuwa confidential ili iwe nzito?
Sasa hata sisi katupatia nakala! Ngoja tumjibu maana na sie si walengwa?
Sasa hivi tunataka Serikali ishughulike na matatizo yetu na sio yako na ya kakikundi kako. Katiba mpya na Tume Mpya sio shida kwetu! Haitatuongezea chakula, matibabu, elimu wala kipato. Tunahitaji maji, mawasiliano na usafiri. Shida yako usiifanye ndio yetu.
Siku nyingine kuwa na nidhamu ya uandishi na mawasiliano. Ulichofanya ni sawa na mwanafunzi amuandikie baba yake barua kuomba pocket money halafu kabla baba hajamjibu aende sokoni aisome barua kwa wachuuzi!
Au ndio maana Selasini hakuandikiwa barua? No office ethics!