Mdharuba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2011
- 824
- 517
- Thread starter
- #241
RIWAYA: Historia Batili (Fake History)
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba( Jk)
+255718274130
+255719274130
EPISODE 21
2⃣1⃣
ILIPOISHIA...
Hisham amempigia simu Khatib kumueleza juu ya majibu ya HIV yalivyokuwa kwa Regina, Khatib anamshauri Hisham atekeleze mauaji halafu watatengeneza ushahidi.
Je, Hisham atafanikisha mauaji??
Hii hapa Historia Batili na Mtunzi wako Jk..
SONGA NAYO.....
Baada ya kukata simu ya Hisham, Khatib aliona ampigie mamaake tena kwa mara nyingine..
Unajua nilisema sitaki kuonana na Mzee J4 kabisa leo, lakini nafikiria kwanini nisionane nae tu ili nikiondoka huku niwe nimemaliza kazi? Maana mambo mengi sana sidhani kama nitaweza kurudi tena huku, na nisipokuja kuonana nae si ataona nimemdharau? Alijaribu kushauriana na mamaake.
Kama ni hivyo sawa, ila usiende mpaka nimpigie Sheikh Lesangwa simu kwanza.. Akituruhusu utaenda Mama Mdharuba alishauri.
Mama, nimekwambia jambo la Mzee J4 liacheni, acha kabisa kumpigia simu Lesangwa..acheni tu mimi niende nikaonane nae, naamini hawezi kuniita kwa ubaya Khatib alionyesha msimamo wake kuhusu Mzee J4, yeye aliamini Mzee J4 ni mtu mstaarabu sana, na hawezi kuwa na nia mbaya na yeye..
Naona siku hizi umekua, haya fanya unavyotaka Mama Mdharuba alikasirika na kukata simu. Khatib akawasha gari yake mpaka nyumbani kwa Marehemu mkewe. Bahati nzuri na Mzee J4 naye alimkuta, wakasalimiana na kuongea mambo mengi na wanafamilia..lakini cha ajabu ambacho kilimpa maswali mengi sana Khatib ni kuwa hakuna aliyemuongelesha wala kumuuliza kuhusu kutofika kwake katika arubain ya marehemu mkewe.. Kichwa chake kilijawa na mawazo mengi..alijifikiri sana, na kuhisi amewakosea sana hawa wazee... Ila aliamua na yeye kupotezea..
Nadhani muda wowote ambao mtakua tayari mniambie ili nitafute usafiri wa kuvihamisha vile vitu vya marehemu vije huku Jambo la mwisho aliloamua kuliongelea Khatib kuhusu mirathi ya Sauda.
Siku yoyote wewe panga tu sisi tutamuagiza mtu Mama Sauda aliamua kujibu ili kuondoa utata na kufupisha habari ili jambo lisiwe refu.
Sawa basi, nitaweka mambo sawa halafu tutawasiliana Khatib alikubaliana na rai ya mama mzazi wa marehemu mke wake, kisha akamuangalia Mzee J4, Safari hii pia imeitika wito wako Mzee J4, vipi tunaongea hapa au unataka faragha kidogo?
Maongezi yangu mimi na wewe ni maongezi ya kiume bana, hakuna haja ya kusikilizwa na wanawake Mzee J4 alitania na kuwafanya wote waliopo pale wacheke..
Sawa basi, mimi jamani naomba niwaage, jamani tutaonana tena, siku mbili hizihizi Khatib aliwaaga wanafamilia huku akiwapa mikono kila mmoja.. Baada ya hapo akageuka kuelekea nje ambapo Mzee J4 alimfuata. Wakaingia kwenye gari na Khatib akawasha gari wakaelekea moja kwa moja maeneo ya Mkonge hotel ambapo Khatib alihisi kutokana na utulivu uliopo hotelini pale, pangekua ni sehemu sahihi zaidi kwenda kufanya mazungumzo na Mzee J4. Mzee J4 hakupinga wazo hili, wakaongozana. Wakafika na kukaa katika viti vilivyoizunguka meza moja iliyojitenga katika mti mmoja ulio katika bustani ya Hotel ile iliyokuwa na mandhari ya kuvutia, muhudumu ambaye alikua makini tangu wanaingia, alikuja haraka na kuwauliza watatumia nini..
Nipe maji, yasiwe baridi Mzee J4 ndiye alikua wa kwanza kuagiza.
Kuna uhai, Dasani, Kilimanjaro, Mt Uluguru, Usambara na Udzungwa, nikupe yapi? Aliuliza Muhudumu ambaye alimtaka Mzee J4 awe 'specific' bila kujua kuwa ataitibua akili ya huyu Mzee hivi karibuni.
Wewe lete hata ya bombani hata yawe kwenye kibakuli, mradi tu yasiwe ya baridi Ndivyo alivyojibu.
Mimi niletee Mountain Dew.. ya baridi Khatib aliongea baada tu ya mhudumu kumuangalia..
Baada ya kuletewa, maongezi yao yakaanza..
Kiukweli unajitahidi sana katika kazi zako, unafanya vizuri mno, na kwa vijana wenzio wenye umri kama wako nadhani wana vingi sana vya kujifunza kutoka kwako, ilaaaa..nimeanza kuwa na mashaka na utajiri wako, kwa kiasi kikubwa upo vizuri sana, lakini unaonekana ni mtu mwenye tamaa sana.. Mzee J4 hakuona sababu ya kupindisha maneno, akaona agonge msumari moja kwa moja.
Mimi usinione hivi hapa leo, nimepitia mambo mengi saana..yaani nimepitia mengi mazito, na kuna muda niliishi maisha ya shida sana..ilishafika kipindi nikawa 'Pastor' tena ilikua Afrika Kusini.. Nikikuangalia wewe nakuona ndani kabisa katika mambo ambayo watu wengine hawawezi kuyaona.. Mimi nataka nikushauri kitu kimoja, ambacho kitakuweka salama zaidi kuliko unavyofanya sasa.. Dhambi ya kuua huwa inazunguka, ogopa sana damu za watu..ni kitu kibaya sana kuua..kibaya sana..sana tena sana.. Mzee J4 ambaye alikua akiongea bila kumpa Khatib nafasi ya kutia neno, aliendelea kusisitiza kuwa mauaji sio mazuri.. Na kumfanya aanze kukumbuka maneno ya Hisham ambayo alimwambia wakati akimueleza kuhusu Mzee J4, akakubali kuwa ni kweli huyu Mzee alimwambia Hisham kuhusu kuua..Hapa alijifunza pia kuwa Mzee J4 anafahamu sana kuhusu kifo cha Sauda..wazo la kumkimbia kwa hoja au kumkatalia kama alivyotaka kufanya, akalifuta. Safari hii alikua akimsikiliza kww makini sana ili akimaliza akiri makosa yake halafu ampe wazo Mzee J4 kama atakubali kuwa mmoja kati ya 'Surbodinates' wake.
★★★★★★★★★★★★★★★★
Hisham, pamoja na kuwa unanifariji sana, lakini najua kuwa huwezi kuendelea kuishi na mimi tena, huwezi Hisham, nakufahamu vizuri na naijua hatma yangu endapo nitaendelea kukaa na wewe hapa Hisham.. Baada ya machozi kukauka, Regina aliamua kutoa ya moyoni. Alishaishi na Hisham kwa miaka saba sasa, sio mtu wa aina hiyo eti aweze kuvumilia usaliti ambao umemfanya akwae na ukimwi, alijua kuwa hii kwa Hisham ni 'geresha -----' tu, na kama angejipendekeza kulala hata usiku mmoja tu 'ingekula kwake'..
Unataka kunambia kuwa huniamini? Hisham wa kipindi kile sio Hisham wa sasa..mimi nakupenda sana mke wangu, ni kazi ngumu sana kwa sasa kwenda kuanzisha uhusiano na mtu mpya nisiyemjua vizuri..nitapata tabu, naomba usiondoke, baki hapa kwa ajili yangu mke wangu, au unataka kuniwekea picha mbaya kwa watu kuwa nimekufukuza sababu umeathirika? Tafadhali usifanye hivyo Hisham alimbembeleza Regina mpaka akafikia kutokwa na machozi, kitendo kilichomfanya Regina alainike.. Akaamua kubaki nyumbani, licha ya kuwa na wasiwasi mkubwa..
Akaanza kukumbuka alipokutana na Hisham kwa mara ya kwanza, usiku wakati Hisham akiwa amelewa sana na kumkuta amelala katika mtaro uliokuwa pembeni ya nyumba ambayo Regina alikuwa akiitumia kama danguro..
Alishangazwa na muonekano wa mlevi yule ambaye alikuwa mtanashati, akaamua kumsaidia.. Ndio kutokea hapo wakazoeana mpka wakafikia hatua ya kuwa wapenzi na mwisho kabisa wakaamua kuoana..na ni kwa ushauri wa Hisham ndo Regina akaacha biashara ile haramu..akamiliki baadhi ya maduka ya vtu mbalimbali pale mjini, Hisham akiwa bado anasafiri sana nje kwenda kuchukua 'unga' kama alivyoagizwa na mabosi wake, mpaka alipokutana na Khatib Canada na kumfanya rafiki, ambaye leo hii ndiye amemfikisha hapa.. Regina alikua na majuto makubwa sana, ila hakuwa na cha kufanya.
Hisham nae alikua na mawazo mengi sana juu ya Regina, hasira alizokuwa nazo ni zaidi ya simba jike aliyefiwa na mwanawe.. Kazi ya kubembeleza ilishaisha na kwa sasa alikua bize sana na simu yake kuangalia 'contact' ambayo huenda angeipunguzia mzigo ule wa mawazo, walau kwa kumpa taarifa tu, habari ile ya Regina ilimuelemea sana, ingawa alijikaza kiume mbele ya Regina kwani hakutaka afahamu mpango wake..
Akiwa ametulia bado 'akisearch contacts' zake, simu yake iliita, alikuwa ni Dr Mwinyi.
Vipi umemaliza hiyo kazi? Aliuliza Dr Mwinyi mara tu baada ya simu yake kupokelewa..
Kazi gani tena Dokta? Hisham anaonekana hakuwa 'aware' kabisa na anachokiulizia Dr Mwinyi.
"Khatib amenitaka nitengeneze ushahidi na kunambia muda si mrefu unakuja na mwili..sasa nimeona kimya ndo maana nikakupigia kukuuliza..
Hisham aliduwaa, akamuangalia mkewe ambaye alikua amelala chali pale kitandani macho yake yakiwa yanaangalia 'gypsum' ya chumbani mle.. Hisham akakosa jibu la kutoa.
★★★★★★★★★★★★★★★★
Je, Mpango wa mauaji utakamilika??
Je, unajua Mzee J4 atampa ushauri gani Khatib??
Huu ni mwanzo tu..kuna zaidi ya episode 300 zinakuja..
Usiache pia kufollow: jk.stories huko instagram..utapitwaa..
Tukutane Episode ya 22..
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba( Jk)
+255718274130
+255719274130
EPISODE 21
2⃣1⃣
ILIPOISHIA...
Hisham amempigia simu Khatib kumueleza juu ya majibu ya HIV yalivyokuwa kwa Regina, Khatib anamshauri Hisham atekeleze mauaji halafu watatengeneza ushahidi.
Je, Hisham atafanikisha mauaji??
Hii hapa Historia Batili na Mtunzi wako Jk..
SONGA NAYO.....
Baada ya kukata simu ya Hisham, Khatib aliona ampigie mamaake tena kwa mara nyingine..
Unajua nilisema sitaki kuonana na Mzee J4 kabisa leo, lakini nafikiria kwanini nisionane nae tu ili nikiondoka huku niwe nimemaliza kazi? Maana mambo mengi sana sidhani kama nitaweza kurudi tena huku, na nisipokuja kuonana nae si ataona nimemdharau? Alijaribu kushauriana na mamaake.
Kama ni hivyo sawa, ila usiende mpaka nimpigie Sheikh Lesangwa simu kwanza.. Akituruhusu utaenda Mama Mdharuba alishauri.
Mama, nimekwambia jambo la Mzee J4 liacheni, acha kabisa kumpigia simu Lesangwa..acheni tu mimi niende nikaonane nae, naamini hawezi kuniita kwa ubaya Khatib alionyesha msimamo wake kuhusu Mzee J4, yeye aliamini Mzee J4 ni mtu mstaarabu sana, na hawezi kuwa na nia mbaya na yeye..
Naona siku hizi umekua, haya fanya unavyotaka Mama Mdharuba alikasirika na kukata simu. Khatib akawasha gari yake mpaka nyumbani kwa Marehemu mkewe. Bahati nzuri na Mzee J4 naye alimkuta, wakasalimiana na kuongea mambo mengi na wanafamilia..lakini cha ajabu ambacho kilimpa maswali mengi sana Khatib ni kuwa hakuna aliyemuongelesha wala kumuuliza kuhusu kutofika kwake katika arubain ya marehemu mkewe.. Kichwa chake kilijawa na mawazo mengi..alijifikiri sana, na kuhisi amewakosea sana hawa wazee... Ila aliamua na yeye kupotezea..
Nadhani muda wowote ambao mtakua tayari mniambie ili nitafute usafiri wa kuvihamisha vile vitu vya marehemu vije huku Jambo la mwisho aliloamua kuliongelea Khatib kuhusu mirathi ya Sauda.
Siku yoyote wewe panga tu sisi tutamuagiza mtu Mama Sauda aliamua kujibu ili kuondoa utata na kufupisha habari ili jambo lisiwe refu.
Sawa basi, nitaweka mambo sawa halafu tutawasiliana Khatib alikubaliana na rai ya mama mzazi wa marehemu mke wake, kisha akamuangalia Mzee J4, Safari hii pia imeitika wito wako Mzee J4, vipi tunaongea hapa au unataka faragha kidogo?
Maongezi yangu mimi na wewe ni maongezi ya kiume bana, hakuna haja ya kusikilizwa na wanawake Mzee J4 alitania na kuwafanya wote waliopo pale wacheke..
Sawa basi, mimi jamani naomba niwaage, jamani tutaonana tena, siku mbili hizihizi Khatib aliwaaga wanafamilia huku akiwapa mikono kila mmoja.. Baada ya hapo akageuka kuelekea nje ambapo Mzee J4 alimfuata. Wakaingia kwenye gari na Khatib akawasha gari wakaelekea moja kwa moja maeneo ya Mkonge hotel ambapo Khatib alihisi kutokana na utulivu uliopo hotelini pale, pangekua ni sehemu sahihi zaidi kwenda kufanya mazungumzo na Mzee J4. Mzee J4 hakupinga wazo hili, wakaongozana. Wakafika na kukaa katika viti vilivyoizunguka meza moja iliyojitenga katika mti mmoja ulio katika bustani ya Hotel ile iliyokuwa na mandhari ya kuvutia, muhudumu ambaye alikua makini tangu wanaingia, alikuja haraka na kuwauliza watatumia nini..
Nipe maji, yasiwe baridi Mzee J4 ndiye alikua wa kwanza kuagiza.
Kuna uhai, Dasani, Kilimanjaro, Mt Uluguru, Usambara na Udzungwa, nikupe yapi? Aliuliza Muhudumu ambaye alimtaka Mzee J4 awe 'specific' bila kujua kuwa ataitibua akili ya huyu Mzee hivi karibuni.
Wewe lete hata ya bombani hata yawe kwenye kibakuli, mradi tu yasiwe ya baridi Ndivyo alivyojibu.
Mimi niletee Mountain Dew.. ya baridi Khatib aliongea baada tu ya mhudumu kumuangalia..
Baada ya kuletewa, maongezi yao yakaanza..
Kiukweli unajitahidi sana katika kazi zako, unafanya vizuri mno, na kwa vijana wenzio wenye umri kama wako nadhani wana vingi sana vya kujifunza kutoka kwako, ilaaaa..nimeanza kuwa na mashaka na utajiri wako, kwa kiasi kikubwa upo vizuri sana, lakini unaonekana ni mtu mwenye tamaa sana.. Mzee J4 hakuona sababu ya kupindisha maneno, akaona agonge msumari moja kwa moja.
Mimi usinione hivi hapa leo, nimepitia mambo mengi saana..yaani nimepitia mengi mazito, na kuna muda niliishi maisha ya shida sana..ilishafika kipindi nikawa 'Pastor' tena ilikua Afrika Kusini.. Nikikuangalia wewe nakuona ndani kabisa katika mambo ambayo watu wengine hawawezi kuyaona.. Mimi nataka nikushauri kitu kimoja, ambacho kitakuweka salama zaidi kuliko unavyofanya sasa.. Dhambi ya kuua huwa inazunguka, ogopa sana damu za watu..ni kitu kibaya sana kuua..kibaya sana..sana tena sana.. Mzee J4 ambaye alikua akiongea bila kumpa Khatib nafasi ya kutia neno, aliendelea kusisitiza kuwa mauaji sio mazuri.. Na kumfanya aanze kukumbuka maneno ya Hisham ambayo alimwambia wakati akimueleza kuhusu Mzee J4, akakubali kuwa ni kweli huyu Mzee alimwambia Hisham kuhusu kuua..Hapa alijifunza pia kuwa Mzee J4 anafahamu sana kuhusu kifo cha Sauda..wazo la kumkimbia kwa hoja au kumkatalia kama alivyotaka kufanya, akalifuta. Safari hii alikua akimsikiliza kww makini sana ili akimaliza akiri makosa yake halafu ampe wazo Mzee J4 kama atakubali kuwa mmoja kati ya 'Surbodinates' wake.
★★★★★★★★★★★★★★★★
Hisham, pamoja na kuwa unanifariji sana, lakini najua kuwa huwezi kuendelea kuishi na mimi tena, huwezi Hisham, nakufahamu vizuri na naijua hatma yangu endapo nitaendelea kukaa na wewe hapa Hisham.. Baada ya machozi kukauka, Regina aliamua kutoa ya moyoni. Alishaishi na Hisham kwa miaka saba sasa, sio mtu wa aina hiyo eti aweze kuvumilia usaliti ambao umemfanya akwae na ukimwi, alijua kuwa hii kwa Hisham ni 'geresha -----' tu, na kama angejipendekeza kulala hata usiku mmoja tu 'ingekula kwake'..
Unataka kunambia kuwa huniamini? Hisham wa kipindi kile sio Hisham wa sasa..mimi nakupenda sana mke wangu, ni kazi ngumu sana kwa sasa kwenda kuanzisha uhusiano na mtu mpya nisiyemjua vizuri..nitapata tabu, naomba usiondoke, baki hapa kwa ajili yangu mke wangu, au unataka kuniwekea picha mbaya kwa watu kuwa nimekufukuza sababu umeathirika? Tafadhali usifanye hivyo Hisham alimbembeleza Regina mpaka akafikia kutokwa na machozi, kitendo kilichomfanya Regina alainike.. Akaamua kubaki nyumbani, licha ya kuwa na wasiwasi mkubwa..
Akaanza kukumbuka alipokutana na Hisham kwa mara ya kwanza, usiku wakati Hisham akiwa amelewa sana na kumkuta amelala katika mtaro uliokuwa pembeni ya nyumba ambayo Regina alikuwa akiitumia kama danguro..
Alishangazwa na muonekano wa mlevi yule ambaye alikuwa mtanashati, akaamua kumsaidia.. Ndio kutokea hapo wakazoeana mpka wakafikia hatua ya kuwa wapenzi na mwisho kabisa wakaamua kuoana..na ni kwa ushauri wa Hisham ndo Regina akaacha biashara ile haramu..akamiliki baadhi ya maduka ya vtu mbalimbali pale mjini, Hisham akiwa bado anasafiri sana nje kwenda kuchukua 'unga' kama alivyoagizwa na mabosi wake, mpaka alipokutana na Khatib Canada na kumfanya rafiki, ambaye leo hii ndiye amemfikisha hapa.. Regina alikua na majuto makubwa sana, ila hakuwa na cha kufanya.
Hisham nae alikua na mawazo mengi sana juu ya Regina, hasira alizokuwa nazo ni zaidi ya simba jike aliyefiwa na mwanawe.. Kazi ya kubembeleza ilishaisha na kwa sasa alikua bize sana na simu yake kuangalia 'contact' ambayo huenda angeipunguzia mzigo ule wa mawazo, walau kwa kumpa taarifa tu, habari ile ya Regina ilimuelemea sana, ingawa alijikaza kiume mbele ya Regina kwani hakutaka afahamu mpango wake..
Akiwa ametulia bado 'akisearch contacts' zake, simu yake iliita, alikuwa ni Dr Mwinyi.
Vipi umemaliza hiyo kazi? Aliuliza Dr Mwinyi mara tu baada ya simu yake kupokelewa..
Kazi gani tena Dokta? Hisham anaonekana hakuwa 'aware' kabisa na anachokiulizia Dr Mwinyi.
"Khatib amenitaka nitengeneze ushahidi na kunambia muda si mrefu unakuja na mwili..sasa nimeona kimya ndo maana nikakupigia kukuuliza..
Hisham aliduwaa, akamuangalia mkewe ambaye alikua amelala chali pale kitandani macho yake yakiwa yanaangalia 'gypsum' ya chumbani mle.. Hisham akakosa jibu la kutoa.
★★★★★★★★★★★★★★★★
Je, Mpango wa mauaji utakamilika??
Je, unajua Mzee J4 atampa ushauri gani Khatib??
Huu ni mwanzo tu..kuna zaidi ya episode 300 zinakuja..
Usiache pia kufollow: jk.stories huko instagram..utapitwaa..
Tukutane Episode ya 22..