Kazi za kisiasa sharti zifanywe na wanasiasa. Polisi hata siku moja hawawezi kufanya kazi za kisiasa kwa ufanisi! ccm kama chama cha kisiasa kimewaachia polisi wakifanyie kazi zake za kisiasa na kazi kubwa sasa hivi kwa ccm ni kukabiliana na CHADEMA. ccm inaamini mabavu yatasaidia katika kukabiliana na CHADEMA kwamba utawapiga watu virungu, utawabambika kesi, na kuwatisha tisha, kuiba uchaguzi na kadhalika. Mbinu hizi zinaweza kufanya kazi kwa kipindi fulani tu wakati hali si mbaya sana. Katika kipindi hiki ambapo Watanzania wanaona uporaji unaofanywa mchana kweupe, serikali iliyoshindwa kuongoza ugumu wa maisha na matatizo mengine kibao kamwe hawawezi kutishika!
Hivyo mbinu zinazotumiwa na polisi kufanya kazi ya ccm haziwezi kufanikiwa, matatizo/changamoto za kisiasa hujibiwa kisiasa kujificha nyuma ya kivuli cha dola na kuwaachia polisi wafanye kazi za kisiasa hakutafanya kazi kwamwe. ccm tokeni mjibu hoja za wananchi, matumizi ya mabavu (nyuma ya mgongo wa jeshi la polisi) hayatawavusha hapa. Mnategwa kisiasa mnaingi wazima wazima,
Hivi hakuna wanasiasa ccm?
Hivyo mbinu zinazotumiwa na polisi kufanya kazi ya ccm haziwezi kufanikiwa, matatizo/changamoto za kisiasa hujibiwa kisiasa kujificha nyuma ya kivuli cha dola na kuwaachia polisi wafanye kazi za kisiasa hakutafanya kazi kwamwe. ccm tokeni mjibu hoja za wananchi, matumizi ya mabavu (nyuma ya mgongo wa jeshi la polisi) hayatawavusha hapa. Mnategwa kisiasa mnaingi wazima wazima,
Hivi hakuna wanasiasa ccm?