Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Gazeti la Nipashe leo limemnukuu Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema na mgombea ubunge wa jimbo la Hai akiwaahutubia wananchi katika jimbo hilo akisema:
"Ni aibu mikutano ya kampeni za CCM kupambwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya na vikundi vya vichekesho, wakato taifa linakabiliwa na matatizo makubwa kama vile umasikini na huduma mbaya za jamii."
Alisema hali ya maisha ya Watanzania wengi inasikitisha kwani hawana uwezo wa kupata milo mitatu kwa siku.
Aliongeza: "Lakini katika kama hiyo, mgombea urais kupitia CCM, rais Jakaya Kikwete anaambatana na wasanii wa kizazi kipya pamoja na kikundi cha vichekesho cha Ze Komedi. Hauwezi kuzungumzia matatizo ya taifa kimzahamzaha, tuna mambo mengi kuhusu mustakabali wetu na sio kutazama vichekesho…huwezi kucheka wakati tupo kwenye msiba wa umasikini, wizi wa rasilimali zetu na huduma mbovu za afya na elimu."
My take;
Katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni katika Viwanja vya jangwani mwezi uliopita, Chadema ilipambwa na kikundi cha muziki wa kizazi kipya cha Sugu. Lakini baadaye nilisikia kwamba baadhi ya viongozi wa Chadema waliona ni vyema wakaachana na mambo hayo, hivo hivi sasa mikutano ya Chadema haipambwi na muziki.
"Ni aibu mikutano ya kampeni za CCM kupambwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya na vikundi vya vichekesho, wakato taifa linakabiliwa na matatizo makubwa kama vile umasikini na huduma mbaya za jamii."
Alisema hali ya maisha ya Watanzania wengi inasikitisha kwani hawana uwezo wa kupata milo mitatu kwa siku.
Aliongeza: "Lakini katika kama hiyo, mgombea urais kupitia CCM, rais Jakaya Kikwete anaambatana na wasanii wa kizazi kipya pamoja na kikundi cha vichekesho cha Ze Komedi. Hauwezi kuzungumzia matatizo ya taifa kimzahamzaha, tuna mambo mengi kuhusu mustakabali wetu na sio kutazama vichekesho…huwezi kucheka wakati tupo kwenye msiba wa umasikini, wizi wa rasilimali zetu na huduma mbovu za afya na elimu."
My take;
Katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni katika Viwanja vya jangwani mwezi uliopita, Chadema ilipambwa na kikundi cha muziki wa kizazi kipya cha Sugu. Lakini baadaye nilisikia kwamba baadhi ya viongozi wa Chadema waliona ni vyema wakaachana na mambo hayo, hivo hivi sasa mikutano ya Chadema haipambwi na muziki.