Hii tabia ni mke wangu tu au?

sarikoki

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
1,194
721
Sisi tunatumia gari moja namshusha ofisini kwake na jioni nampitia tunarudi.. sasa asubui toka tunaamka mpaka tuaondoka yeye ni kutoa maagizo tu..... sasa kali zaidi wakati ndo tunatoka ndani kuelekea parking..Men, it takes another 5 to 10 mnts mpaka afike. Anaanza upya, - mmenielewa?...usahau.... watoto muhakikishe.....usafi ...

Sasa na wakati wa kumpitia jioni kurudi nyumbani nampigia simu namwambia baada ya nusu saa nitakua hapo.. yaani nikifika it will take another 15 mnts atoke huko ofisini.. ukimuuliza eti nilikua nazima computer.... mwanzoni ilinipa shida sana ila imebidi nizoee tu... kama nawai mahali lazima nianze kuondoka 1hr before.

But ilove her to death.
 
ndio tuko hivyo, ila in my case mimi ndio nipo sharp kuliko yeye! yaani huwa nawahi kwenye majority of the things! so its normal!
 
ndio tuko hivyo, ila in my case mimi ndio nipo sharp kuliko yeye! yaani huwa nawahi kwenye majority of the things! so its normal!

Aisee. the dude is luck, mwanzoni unaweza mrukia mtu kichwa kama huna staha.
 
% kubwa ya wamama wako hivyo, ingawa kuna tafiti zinazoonyesha kuwa watu wanaopenda kutoa maagizo sana ama kutuma zaid ni wavivu ukilinganisha na wale wasiopenda kutoa maagizo ama wasiopenda kutum.

pia watu wengi ambao huwa hawako systematic na mambo yao like hawana ratiba kamili nayofuatwa ni wahanga sana wa kuchelewa kufanya mambo ya msingi na mara nyingi huwa na hofu sana ya perfomance kwenye baadhi ya mambo.

kama ni tabia yake waweza kumtrain kwa kumtegenezea ratiba ambao yeye ataiweka kwenye diary yake. kila akiamka baada ya kusali asome diary kuangalia kazi zake za siku, na azifanye kwa muda alioupanga, hii itamfanya awe systematic zaid na punctual pia kama ni mvivu wa kazi za mikono basi itamlazimisha kufanya kazi.
 
duh sijui mmziwanda wangu naye atakuwa hivyo.... ntamvumilia tu ndo maisha. kwa shida na raha till dealth.
 
% kubwa ya wamama wako hivyo, ingawa kuna tafiti zinazoonyesha kuwa watu wanaopenda kutoa maagizo sana ama kutuma zaid ni wavivu ukilinganisha na wale wasiopenda kutoa maagizo ama wasiopenda kutum.

pia watu wengi ambao huwa hawako systematic na mambo yao like hawana ratiba kamili nayofuatwa ni wahanga sana wa kuchelewa kufanya mambo ya msingi na mara nyingi huwa na hofu sana ya perfomance kwenye baadhi ya mambo.

kama ni tabia yake waweza kumtrain kwa kumtegenezea ratiba ambao yeye ataiweka kwenye diary yake. kila akiamka baada ya kusali asome diary kuangalia kazi zake za siku, na azifanye kwa muda alioupanga, hii itamfanya awe systematic zaid na punctual pia kama ni mvivu wa kazi za mikono basi itamlazimisha kufanya kazi.

Hasante sana kwa kunielimisha... yaani kama umesoma vizuri nimeandika nishamzoea, inamaana mbinuzote hizo nilishazifanya... house girl ana ratiba zote za usafi, mlo wa watoto na mlo wetu hata nikaweka na simu kabisa kama kuna kitu kinamtatiza tupigie. I think ni hulka tu ya mtu. Kikubwa ni kumuelewa na kumpenda zaidi.
 
Ndivyo walivyo. Mimi wa kwangu nilimpa funzo mara mbili na alishabadilika. Siku ya kwanza chakula kilichelewa kwa kujizungushazungusha na wasaidizi wake, nikawasha gari nikaenda kula nyama choma. Siku nyingine akachelewa kujiandaa kwenda kazini na kutoa maelekezo ambayo mengine yangetolewa jioni, nikawasha gari nikaondoka na nikapita ofisini kwao na kugeuza gari na kwenda ofisini kwangu. Niliporudi jioni nikaja na kilo ya kitimoto ikiwa imesheheni chilli, tomato sause na kachumbali, kicheko juu. Hadi leo ana panctuality ya hali ya juu
ONYO
Tafadhali usiige mbinu hii maana kwa wanawake wengine hii inaweza kuleta mgogoro mkubwa sana
 
Wote wako hivyo hivyo, mimi huwa nawasha gari naanza kabisa kuondoka anafanya kunifukuzia. Maana ukisema umsubiri hamalizi! Ila huwa ananiweza wakati wa kurudi, maana ukimpitia ofisini kwake atakuweka hapo hata saa zima. But there was a day niliamua kuondoka, nikampa adhabu ya kupanda daladala, angalau siku chache baadaye alishika adabu, although with time akarudi kulekule. Nafikiri hawa wenzetu ndiyo wapo hivyo.
 
Hasante sana kwa kunielimisha... yaani kama umesoma vizuri nimeandika nishamzoea, inamaana mbinuzote hizo nilishazifanya... house girl ana ratiba zote za usafi, mlo wa watoto na mlo wetu hata nikaweka na simu kabisa kama kuna kitu kinamtatiza tupigie. I think ni hulka tu ya mtu. Kikubwa ni kumuelewa na kumpenda zaidi.

anyway so you were just curious to know about the rest of women, mimi nimekupa corrective means so just ignore it. and sorry kwa kukufanya usome maelezo ambayo hayana faida kwako.

but nimependezwa sana na tabia yako kwamba despite her weakness wewe unazidi kumpenda zaidi. hiyo ni nzuri sana. ni wanaume wachache sana ambao mpungufu ya wenzi wao wanayakubali na kuongeza upendo
 
Ndivyo walivyo. Mimi wa kwangu nilimpa funzo mara mbili na alishabadilika. Siku ya kwanza chakula kilichelewa kwa kujizungushazungusha na wasaidizi wake, nikawasha gari nikaenda kula nyama choma. Siku nyingine akachelewa kujiandaa kwenda kazini na kutoa maelekezo ambayo mengine yangetolewa jioni, nikawasha gari nikaondoka na nikapita ofisini kwao na kugeuza gari na kwenda ofisini kwangu. Niliporudi jioni nikaja na kilo ya kitimoto ikiwa imesheheni chilli, tomato sause na kachumbali, kicheko juu. Hadi leo ana panctuality ya hali ya juu
ONYO
Tafadhali usiige mbinu hii maana kwa wanawake wengine hii inaweza kuleta mgogoro mkubwa sana

Hehehehe... mkuu unatisha.. yaani mimi nikijaribu ndani ya nusu saa simu ya mama angu inaingia. Na nitapata semina kila siku si chini ya mwezi mmoja..aisee Du!
 
Wote wako hivyo hivyo, mimi huwa nawasha gari naanza kabisa kuondoka anafanya kunifukuzia. Maana ukisema umsubiri hamalizi! Ila huwa ananiweza wakati wa kurudi, maana ukimpitia ofisini kwake atakuweka hapo hata saa zima. But there was a day niliamua kuondoka, nikampa adhabu ya kupanda daladala, angalau siku chache baadaye alishika adabu, although with time akarudi kulekule. Nafikiri hawa wenzetu ndiyo wapo hivyo.

Hehehehehe
 
Huyo mwanamke ana dharau za hali ya juu. Hajui kuheshimu muda wala kumheshimu mumewe. She is "self centered".
 
ni kweli tatizo hilo lipo sana kwa wanawake,lakini mara nyingi nimeobserve nikaona mama anaamka ahakikishe kila kitu kipo sawa nyumbani ndipo atoke wakati mwanaume anajiandaa na mara nyingi anaweza kunywa chai wakati mke wake hapati huo muda.atatoka nje honi kwa wingi.saidia majukumu mnapoamka itapunguza kuchelewa.pendeni wake zenu
 
mimi ndivyo nilivyo kabisaa nimeachwa na gari na mume wangu mpaka ,sikuhizi nimegoma kupanda natumia daladala,hata asubuhi namwambia we nenda tu ,alafu najikuta naninapoishi hamna daladala mpaka utembee 1km,du ila nshazoea ,kuachwa tena jumapili nimeachwa kwenda kanisani hahahahah yani siwezi acha kabisa,
Kwanini inatokea hivi???????
wanawake tuna majukumu mengi sana hujaagiza chakula mchana ,usiku ,una mtoto mdogo hujaacha maelekezo,hujasisitiza usafi,yaani mambo mengi,mwanamme yeye akiamka asubuhi hawazi lolote zaidi yakuuliza umenipigia pasi?avae achukue funguo aende kwenye gari aanze kupiga horne,thats all,kumbuka pia mara nyingi mwanamke ni wamwisho kulala ahakikishe nyumba yake safi jion kila kitu kipo sawa principle hii inaitwa LIFO -Last in First out,mfano unatoka na mtoto ujiandae wewe then mtoto,yeye anajiandaa yeye tu then hapo hakuna uwiano,yaani binafsi mume wangu ananiudhi jinsi anavyonishurtisha kuwahi nimefika mwisho nikamwambia we nenda tu ntapanda daladala na nimezoea sababu anawasha gari anasogea taratibu taratibu unakuta yuko mbali ,basi nasema tu shida ya nini?
 
Nakushukuru sana Sarikoki kwa kumbeba wenzi wako jinsi alivyo! Kwa jinsi navyojua wanaume walivyo angeanza kumtusi na kumpa kero zisizo na maana.
 
ni kweli tatizo hilo lipo sana kwa wanawake,lakini mara nyingi nimeobserve nikaona mama anaamka ahakikishe kila kitu kipo sawa nyumbani ndipo atoke wakati mwanaume anajiandaa na mara nyingi anaweza kunywa chai wakati mke wake hapati huo muda.atatoka nje honi kwa wingi.saidia majukumu mnapoamka itapunguza kuchelewa.pendeni wake zenu
Asnte mkuu kwakuliona hili
 
mimi ndivyo nilivyo kabisaa nimeachwa na gari na mume wangu mpaka ,sikuhizi nimegoma kupanda natumia daladala,hata asubuhi namwambia we nenda tu ,alafu najikuta naninapoishi hamna daladala mpaka utembee 1km,du ila nshazoea ,kuachwa tena jumapili nimeachwa kwenda kanisani hahahahah yani siwezi acha kabisa,
Kwanini inatokea hivi???????
wanawake tuna majukumu mengi sana hujaagiza chakula mchana ,usiku ,una mtoto mdogo hujaacha maelekezo,hujasisitiza usafi,yaani mambo mengi,mwanamme yeye akiamka asubuhi hawazi lolote zaidi yakuuliza umenipigia pasi?avae achukue funguo aende kwenye gari aanze kupiga horne,thats all,kumbuka pia mara nyingi mwanamke ni wamwisho kulala ahakikishe nyumba yake safi jion kila kitu kipo sawa principle hii inaitwa LIFO -Last in First out,mfano unatoka na mtoto ujiandae wewe then mtoto,yeye anajiandaa yeye tu then hapo hakuna uwiano,yaani binafsi mume wangu ananiudhi jinsi anavyonishurtisha kuwahi nimefika mwisho nikamwambia we nenda tu ntapanda daladala na nimezoea sababu anawasha gari anasogea taratibu taratibu unakuta yuko mbali ,basi nasema tu shida ya nini?
Na kutoka ofisini je? Huko huwa mnafanya nini?
 
hakuna kitu kigumu kama kutumia muda kwa wakati sahihi, hili huathiri wengi kwa kuwa hawajali muda.. ni tabia lakin inaweza kurekebishika japo inachukua muda ..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom