Bishanga
JF-Expert Member
- Jun 29, 2008
- 15,323
- 10,050
Mwanaume unapewa mkong'oto wa nguvu na mkeo,unakimbilia Polisi,kaunta unaulizwa 'kulikoni?','nimepigwa na mke wangu,angalia ninavyovuja damu kichwani'unajibu huku chozi linakutoka,unaona polisi anaanza kutabasamu kwa mbali na anamminyia jicho askari wa kike.'tukusaidie nini sasa?' anakuuliza kwa zarau.'Naomba pf3' unajibu. ''Kwani wakati anakutwanga we ulikuwa wapi?' anakuuliza kwa mshangao kabisa.'Kanikamata akanibonda' unaitikia,mara unasikia kicheko kwa mbaalii kituoni. Ndo nini sasa hii? Angekuwa mwanamke karipoti kesi ya kupigwa wangu wangu RB inafunguliwa.
Kinababa hebu tuulizane hapa,ukiiwa 'abused'(kwa lugha ya AD) kimbilio lako wapi? Wenzetu kina mama vikishindikana utasikia wamekwenda kwa Mrema(mid 90's),mara TAWLA,mara TAMWA,mara LHRC,hata mashirika ya kimataifa kibao yapo kwa ajili ya kuwalinda na kuwatetea,hata Bunge sexual offences act ipo kuwalinda wao na watoto,kinababa je ulinzi uko wapi?
Kinababa hebu tuulizane hapa,ukiiwa 'abused'(kwa lugha ya AD) kimbilio lako wapi? Wenzetu kina mama vikishindikana utasikia wamekwenda kwa Mrema(mid 90's),mara TAWLA,mara TAMWA,mara LHRC,hata mashirika ya kimataifa kibao yapo kwa ajili ya kuwalinda na kuwatetea,hata Bunge sexual offences act ipo kuwalinda wao na watoto,kinababa je ulinzi uko wapi?