Hela za matunzo ya mtoto wanakula na mwanaume mwingine

sasa solution ni kumnyang'anya mama mtoto au kuwashauri waishi nyumba kubwa zaidi kwa ajili ya privacy? mtoto si nguo ni binadamu. hekima na busara zinatakiwa kutumika badala ya mihemko. hapo mtoto anaishi na mama aliyemzoea, tatizo nyumba ndogo hakuna usiri. huko mkoani ataenda kuishi na baba mzazi lakini mgeni na mama mlezi mgeni. hawa wazazi wajishushe wakae wajadili hatma ya mtoto badala ya kukomoana.
mkuu wewe unaweza lipia nyumba akae mwanaume mwenzio? any way ngoja niingie huko nione
 
Mchukue Mwanao kaishi nae mwenyewe

Huyo mwanamke si mstaarabu kabisa
Aliemzalisha mwanamke asiye mstaarabu ndiye si mstaarabu.
Kumchukua mtoto siyo suluhisho, unadhani hata akimchukua huyo mtoto atakua anajisikiaje kwa maisha anayoishi mama yake!? Litakua jeraha sana na huenda ikamharibu kisaikolojia.
 
chukua huyo mtoto tupa bording kule mbeya aendelee kula sembe likizo sio ndefu atakaa kwako hata akiteswa cku mbili sio mbaya xn vinginevyo huyo mtoto atajifunza tabia chafu,cku zote ustawi wa jamii huwa upande wa beijing huwa hawamsadii mwanaume
 
Tafuta sehemu nzuri ya kumpeleka mtoto nashauri kama wazazi wako wapo sehemu nzuri ambayo mtoto anaweza kupata huduma zote mpeleke huko au kwa dada yako au hata kwa shangazi yako ila hakikisha hao watu wana upendo wa kweli na huyo mwanao, baada ya hapo rudisha nyumba kwa mwenyewe.
 
M kukaa kwa mwanamke siwez lkn hilo jamaa limeka kwa dem thn matumiz from mwanaume mwingine.
 
umeandika kwa chuki sana na kumuita mwenzio jitu! ulitaka mwenzio aishije kama umeenda nje kama maalimu seif??

kwa ulivyoandika napata wasiwasi hutoi hela zote ulizoandika hapo kilichokuuma kawa na mtu huwezi kukumbushia.
 
hujakosea sana sema unaingiza hisia kwenye mambo yanayohitaji mantiki. mzazi mwenzio ana haki ya kuwa na mwanaume mwingine kama ambavyo na wewe una mwanamke mwingine. kwa hiyo mtoto amepata baba mlezi. huyo jamaa si alimsindikiza mpenzi wake jamani? mambo ya mpenziwe ni yake. Halafu ni baba mlezi, tatizo kitonga. haya yaliyotokea ni matokeo tarajiwa kabisa pale wazazi halisi wanapotengana wakiwa bado vijana. tatizo pekee ninaloona ni kwamba mama mzazi na baba mlezi ni watu wasiojituma.

kwamba wanalalaje humo ndani wanajua wenyewe, labda wanafanzana mchana mtoto akiwa shule. kuanza kushughulika na adabu ya mama saa hizi sijui kama utaweza maana huna ushahidi. na wewe kwa nini uliwapangishia nyumba ya chumba kimoja? mama alitakiwa kuwa na chumba chake, na mtoto chumba chake. mambo ya mama kubadilisha nguo huku katoto kanajidai kamelala kumbe kanachungulia si mazuri kwa hiyo madhara ya chumba kimoja si kukiwa na mwanaume tu. ningekuwa mi ndo wewe labda ningepunguza matumizi kama kodi ya nyumba na chakula. huna mamlaka ya kusema huyo njemba aondoke.

ukisema uchukue mtoto utuambie ni kwa nini hukumchukua toka siku nyingi ilihali ulijua mama yake hana uwezo wa kumlea, au ulifikiri huyo mwanamke ataishi kiseja mpaka mtoto afike chuo kikuu?? na umejiandaaje wewe na mke wako kumlea huyo mtoto? muache mama aishi maisha yake. wanaume wengi mkizaa kabla hamjaoa huwa hamtaki wazazi wenzenu wawe na mahusiano wakati tayari mmewaacha. hata ikitokea wanaolewa bado mnaleta shida..ooh sitaki mtoto wangu aishi na baba mwingine!! Na mama naye hataki mtoto aishi na mama mwingine. kwa hiyo unaskia wengine wana-resolve kupeleka watoto boarding ili wakose wote! Ukweli ni kwamba hata huyo mwanamke angehamia kwa huyo mwanaume bado ungekasirika. Jifunze kuishi na matokeo ya makosa yako. rekebisheni tu hapo kwenye matumizi.
mtoto amefika miaka saba kwa hiyo anaweza kumchukua , kabla ya hapo isingewekana kwa kuwa umri ulikuwa hauruhusu kufanya hivyo
 
sasa solution ni kumnyang'anya mama mtoto au kuwashauri waishi nyumba kubwa zaidi kwa ajili ya privacy? mtoto si nguo ni binadamu. hekima na busara zinatakiwa kutumika badala ya mihemko. hapo mtoto anaishi na mama aliyemzoea, tatizo nyumba ndogo hakuna usiri. huko mkoani ataenda kuishi na baba mzazi lakini mgeni na mama mlezi mgeni. hawa wazazi wajishushe wakae wajadili hatma ya mtoto badala ya kukomoana.
huyu dada anataka kumgeuza mtoto kitega uchumi, hao ustawi hawana maana
 
mkuu wewe unaweza lipia nyumba akae mwanaume mwenzio? any way ngoja niingie huko nione
mimi nilihoji suluhisho lako kuwa mama anyang'anywe mtoto kwa sababu tu anakaa na mwanaume kwenye nyumba inayolipiwa na baba mtoto. suluhisho si kumnyang'anya mama mtoto bali kukubaliana juu ya gharama za nyumba na chakula. ukiingia ndo utajua inaumaje kunyang'anywa mtoto uliyemlea mwenyewe toka umemzaa kwa sababu tu umepata mwanaume mwingine.
 
Back
Top Bottom