Hela za matunzo ya mtoto wanakula na mwanaume mwingine

Hahaha et lijamaa lenyewe kama linavuta bange.Itakuwa pesa unazotuma zingine ananunulia bangi ili apate stimu ya kukulelea mwanao.
 
Wadau nawasalimu,

Kuna mtoto nilizaa na binti mmoja wakati makazi yangu yakiwa Dar, kwa sasa ana miaka 7 na darasa la pili.Nilipoondoka Dar na kuamia mwanza kwa shughuli zangu binafsi niliamua kumpangishia huyu binti chumba na sebule waweze kuishi na mwanangu hapo, na natuma hela za mahitaji yote, ikiwemo kodi, kula, afya na ada ya mtoto, huyu mzazi mwenzangu hana shughuli yeyote kwenye maisha, namhudumia mimi kila kitu.

Sasa hivi karibuni ameleta jitu moja hapo nilipompangisha na linaishi nae humo humo na mtoto wangu, binti na hili jitu wanasubiri hizi hizi hela za matunzo ninazotuma ndio waishi, Je hii ni haki?

Ina maana huyu mwanaume anatembea na mama wa mtoto wangu humo humo huku mtoto akiwa amelala humo maana ni chumba na sebule tu, Je hii ni haki?

Hizi taarifa nilizisikia muda mrefu kupitia kwa mwenye nyumba ambae tuna mawasiliano ya karibu,sasa kuanzia January nikaacha kutuma pesa za matunzo, tukawa na mzozo, akanipeleka ustawi wa jamii, wakanipigia simu niende Dar, hivi juzi ndio nimekuja, ustawi wa jamii wakanieleza mambo ya ajabu sana na sifuati hata moja.

Masharti yangu ni haya, huyo mwanaume aondoke hapo, kama anaendelea kukaa hapo alipe hiyo kodi mwenyewe, au wanipe mtoto niondoke nae pia hawataki.

Nimeenda ustawi wa jamii kwenye hiyo kesi nashangaa kumkuta na yule jamaa pale kaja na mzazi mwenzangu, ikabidi niwaulize wale maafisa huyu anahusikaje hapa.

Nilitaka nimpe kipigo kizito huyo jamaa, bahati yake nikakuta ana li mwili la kuinua vyuma, halafu ni kama anavuta bang,e hivi kikao kiliisha bila muafaka.

Nimempa mwanamke masharti akiyafuata ndipo narudisha huduma

Au wadau nimekosea?
Dah pole sana mkuu
Hata mie ingeniuma
Fanya mchakato mchukue mtoto wako hamna jinsi
 
Mchukue mtoto peleka bording , akitoka unakaa nae mwenyewe. Kisheria motto akifikisha miaka 7 inaruhusiwa kuchukuliwa na baba ake. Uctoe hta mia kwa sasa.
Huyo Dada hajitambui kabisa
 
Acha ujinga, wambie nataka mtoto kwa lazma la cvyo acha kutoa pesa. Wanamtumia mtoto kula pesa zako
 
Mtoto apelekwe kwa bibi yake wa pande yeyote kisha kata mirija yote ya ulaji kwa huyo mwanamke. Fedha ziende kwa bibi. Kama hilo haliwezekani fanya haraka kumuhamisha huyo mtoto haraka. Hilo libwana wanapanga njama mbaya sana dhidi yako beleive me
 
wtoa matumizi mambo ya mahusiano achana nayo...kama huwezi toa ya mtoto ye aishi na jamaaa watalipia kodi na mengine....labda nia ya kutoa kodinamengine nini...coz kuna matunzo kwa ajili ya kufaya mtoto alalewe vizuri kama kodiinauma acha ili jamaa alale ndani kwa kodi ya mzazi mwenzio.....maana mahitaji ya mwili ameyakosa so anayahitaji
 
Mtoto apelekwe kwa bibi yake wa pande yeyote kisha kata mirija yote ya ulaji kwa huyo mwanamke. Fedha ziende kwa bibi. Kama hilo haliwezekani fanya haraka kumuhamisha huyo mtoto haraka. Hilo libwana wanapanga njama mbaya sana dhidi yako beleive me
hivi hii tabia ya kuwapelekea wazazi wenu kina bibi mizigo ya kulea wajukuu mnaitoa wapi? Wazazi wanahitaji kupumzika na kula mema ya uzee na si kulea wana wa wana. Mbebe mizigo yenu wenyewe. Watoto waende kwa bibi kusalimia au kuwapa company wakishakuwa wakubwa.
 
Peleka mtoto boarding mkoa unaishi. Hii itasaidia kupunguza gharama za maisha na kumaliza wizi anaoufanya huyo mwanamke.
 
Sio wivu, yaani mm nimlishe baba mzima!!

Nina Maswali Kazaa ambayo yatakufanya ufanye maamuzi....

Najua mtu ulimwacha hana haki ya kupenda na kupendwa baada ya kuachwa kukizi haja zake za mwili...I hope unajua ilo...

Pili kila mtu ana choice yake inawezekana kabisa ukawa unamlisha jamaa ila wewe unachotakiwa kujua na kufatilia mtoto wako hela unayotuma inamfaidisha... mambo muimu uwa nenda kalipe mwenyewe na sio kumpa mwanamke hela kama shule, tuisheni lipa mwenyewe direct.. hela ya chakula ndo unampa plus mavazi najua una ndugu kama ni wa kike unamchukua mke wako unampitia mnaenda kumfanyia shopping waanze kujenga uhusiano wa kuzoeana na mama yake wa kufikia...

Ukitaka kufanya kwa kukumoa unamkomoa mtoto wako ambapo inakuwa aina tija katika ilo jambo
 
Hapo pagumu unless umuhamishie nyumba kubwa alternative ni wewe kumuhamisha either umchukue uishi nae au umpeleke say kwa dada yako au mama yako ili.kumridhisha mama.mtoto.kuwa mwanae hatattoswa na mama wa kambo maana ni ukweli uliowazi mama wa kambo wanawatesa watoto.wa kambo. Zaidi ya happ mtafutie shule nzuri ya boarding aishi huko wakati wa likizo awe anapokezana kati ya kwako na kwa mama then utatosa support.wakati.akiwa kwa mama tu.
 
Mkeo anajua kuwa una mtoto nje???usije ukawa unangangania kumchukua mtoto kumbe hata mamake wa kufikia hajui
 
Na wanaume kwa wanawake ni kujitahidi kuwa makini ili kuepusha migogoro kama hii tuepuke watoto kabla ya ndoa mnawatesa watoto na kuwaharibu saikolojia zao
 
Mnaosema chukua mwanao sina uhakika kama mnajua uchungu wa mwana kwa mamaye kabisa kwangu Mimi siko tyari mtoto wangu alelewe na mama mwingine kama bado unaishi kwenye hii dunia hata kama sina uwezo ntapigana kwa ajili ya wanangu /mwanangu.
 
Teh teh teh teh teeeeeh!! Muoe huyo mama wa mwanao, case closed.
 
Back
Top Bottom