Nsanzagee
JF-Expert Member
- Jun 28, 2023
- 1,939
- 4,116
Leo tuna akina Abdul ambao utawaona na kina Museveni huko wakiwakilisha Watanzania na wakati huo huo hawajulikani wana nafasi gani hapo serikalini
Watoto wa Magufuli na familia yake kwa ujumla walifundwa siyo siri
Baba yao alikuwa kiongozi mkuu wa nchi hii, lakini niseme ukweli kuwa, sikuwahi kuwaona kwenye Hafla, Ikulu wala kwenye mkusanyiko wowote wa viongozi wakiwa kama watoto wa Rais
Haya ndiyo maadili twapaswa kuwajengea watoto wetu
Mtu unapata nafasi ya Kuongoza nchi, watoto wako nao unataka wawe viomgozi? Haya sidhani kama ni maadili ya kiuongozi!
Ofisi tumpe Rais, watoto nao tuwe tunawahudumia kama viongozi wetu? Watuhoji kwa nini tumechelewa ofisini?
Hii hapana
JPM apewe mauwa yake kwa maadili ya familia yake!
Tunapozungumzia maadili ya kiuongozi na kuondoa sintofahamu ya familia za viongozi wetu kufanya watoto wao wawe frontline kana kwamba nao ni viongozi wetu, sisi kama Taifa, yatupasa tuliweke jambo hili sawa!
Kwamba, tukipata Rais, basi hata watoto wake wawe sehemu ya uongozi wa mzazi wao na au itambulike kuwa, (baba/mama)yao ndiyo kiongozi wetu, watoto wao wawe kama watoto wa mkurugenzi ama kiongozi yeyote yule
Tumpigie kura mtu fulani, badala ya yeye tu kuwa ndiye kiongozi na anayepaswa aheshimiwe, badala yake kunakuwepo na watoto wake ambao nao anataka wawe sehemu ya uongozi wake na nusu ya heshima yake, ipelekwe kwa hao? Huku ni kukosa soni!
Je, hakuna utata wowote mtoto wa Rais kuwa sehemu ya kiuongozi?
Watoto wa Magufuli na familia yake kwa ujumla walifundwa siyo siri
Baba yao alikuwa kiongozi mkuu wa nchi hii, lakini niseme ukweli kuwa, sikuwahi kuwaona kwenye Hafla, Ikulu wala kwenye mkusanyiko wowote wa viongozi wakiwa kama watoto wa Rais
Haya ndiyo maadili twapaswa kuwajengea watoto wetu
Mtu unapata nafasi ya Kuongoza nchi, watoto wako nao unataka wawe viomgozi? Haya sidhani kama ni maadili ya kiuongozi!
Ofisi tumpe Rais, watoto nao tuwe tunawahudumia kama viongozi wetu? Watuhoji kwa nini tumechelewa ofisini?
Hii hapana
JPM apewe mauwa yake kwa maadili ya familia yake!
Tunapozungumzia maadili ya kiuongozi na kuondoa sintofahamu ya familia za viongozi wetu kufanya watoto wao wawe frontline kana kwamba nao ni viongozi wetu, sisi kama Taifa, yatupasa tuliweke jambo hili sawa!
Kwamba, tukipata Rais, basi hata watoto wake wawe sehemu ya uongozi wa mzazi wao na au itambulike kuwa, (baba/mama)yao ndiyo kiongozi wetu, watoto wao wawe kama watoto wa mkurugenzi ama kiongozi yeyote yule
Tumpigie kura mtu fulani, badala ya yeye tu kuwa ndiye kiongozi na anayepaswa aheshimiwe, badala yake kunakuwepo na watoto wake ambao nao anataka wawe sehemu ya uongozi wake na nusu ya heshima yake, ipelekwe kwa hao? Huku ni kukosa soni!
Je, hakuna utata wowote mtoto wa Rais kuwa sehemu ya kiuongozi?