Haya wale wasiomjuwa jini (pepo) ndio huyo picha yake anatisha usiangalie please

Status
Not open for further replies.
Kama haikuingii akili sawa amini usiamini huo ndio mfano wa Mapepo aliowaumba Mungu hatuwezi kuwaona lakini wao wanatuona ukiamini au usiamini nakuacha kama ulivyo mkuu kazi kwako... Bosi Michembe

Kama hatuwezi kuwaona tumejuaje kuwa wako hivyo kama ilivyo kwenye huo mchoro?? TUMEBUNI KWA HISIA AU??
 
Kama hatuwezi kuwaona tumejuaje kuwa wako hivyo kama ilivyo kwenye huo mchoro?? TUMEBUNI KWA HISIA AU??
Kuna Binadamu kamuona Mungu? Mbona tunamini kuwa kuna Mungu? kuna kiumbe yoyote aliyemuona Mungu? Kuna mtu aliyewaona Malaika ? mbona tunaamini Viumbe malaika wapo?
 
ndio ni kweli kabisa Majini ni wengi sana kuliko binadamu . Katika kila binadamu mmoja basi kuna majini unaweza kufananishana majini zaidi ya 1000. Usiogope hawa ni viumbe kama binadamu ila hawaonekani kwa macho lakini wapo kila sehemu, wanapenda kuishi majangwani,sehemu za takataka,chooni na kwenye miti mikubwa kwamfano mibuyu miembe, misufi, mivinje bahri na sehemu kwenye giza............ gfsonwin


Ok, umenena kuwa majini ni viumbe kama sie binadamu ila hawaonekani. Sasa ni nini haswa faida ya hawa majini kwetu sie binaadamu?
 
Ufalme wa Majini



WANA WA KIFALME NA WATAWALA WAKUU


(Princes and Grand Dignataries)


1. Beelzebuth, Chifu Mkuu wa Majini (Supreme Chief of the Infernal Empire).


2. Satan, Kiongozi wa Upinzani (Leader of Opposition).


3. Euronymous, Mwanamfalme wa Kifo (Prince of Death).


4. Moloch, Mwanamfalme wa Ardhi ya Machozi (Prince of the Land of Tears).


5. Pluto, Mwanamfalme wa Moto (Prince of Fire).


6. Leonard, Bwana Mkubwa wa Sabato (Grand Master of Sabbaths).


7. Baalberith, Waziri anayeshughulikia Mikataba (Minister of Treties).


8. Proserpine, Jini Mtawala wa Kike; Binti mfalme Mwenye Mamlaka juu ya Majini wenye Kudhuru (Sovereign Princes of Mischievous Spirits).


BARAZA LA MAWAZIRI:


1. Adramelek, (Lord High Chancellor)


2. Astaroth, (Grand Treasurer).


3. Nergal, (Chief of Secret Police).


4. Baal, (Commander-in-Chief of the Infernal Armies).


MABALOZI:


1. Belphegor, ni Balozi wa Majini katika nchi ya Ufaransa.


2. Mammon, ni Balozi wa Majini katika nchi ya Uingereza.


3. Belial, ni Balozi wa Majini katika nchi ya Uturuki.


4. Rimmon, ni Balozi wa Majini katika nchi ya Urusi.


5. Thamuz, ni Balozi wa Majini katika nchi ya Hispania.


6. Hutgin, ni Balozi wa Majini katika nchi ya Italy.


7. Martinet, ni Balozi wa Majini katika nchi ya Uswisi


MAJAJI KATIKA SERIKALI YA MAJINI:


1. Lucifer, ... Jaji Mkuu ..(Lord Chief Justice).


2. Alastor, .... Kamishna wa Kazi za Serikali ...(Commissioner of Public Works).
 
WASIMAMIZI KATIKA UFALME WA MAJINI:


1. Verdelet, ... Mwendeshaji Sherehe ..MC...(Master of Ceremonies)


2. Succor Benoth, ... Chifu wa Matowashi...(Chief of the Eunuchs)


3. Chamos, .... Msimamizi Mkuu wa Nyumba ya Mfalme ....(Lord High Chamberlain)


4. Melchom, ... Mlipaji Mkuu ...(Paymaster)


5. Misroch, ... Mhudumu Mkuu ... (Grand Steward)


6. Behemoth, ... Mbebaji Mkuu wa Kombe la Mfalme ...(Grand Cup Bearer).


7. Dagon, ... (Grand Pantler).


8. Mullin, (First Gentleman of the Bedchamber).


WASIMAMIZI WA MATAMASHA (SHEREHE):


1. Kobal,... Msimamizi wa Jukwaa...(Stage Manager)


2. Asmodeus, ... Msimamizi wa Makasino...(Superintendent of Casinos)


3. Nybbas, ... Chifu wa Uigizaji ...(Chief Mimic).


4. Antichrist, ... ni Mkuu wa Mazingaombwe na Maigizo (Juggler and Mimic).

MAUMBO NA SURA ZA MAJINI KULINGANA NA SAYARI ZAO


1. Majini wa Saturn (Zohal) - Majini wa Jumamosi


Majini hawa huwa ni warefu, wembamba na wenye sura ya ukatili na kutisha, wana nyuso nne ambazo kila moja iko kila upande wa kichwa, yaani kwa mbele na nyuma sura inakua na midomo kama ya ndege.


Pia wana sura nyeusi inayon'gaa katika kila goti. Mwendo wao ni kama mwendo wa upepo ambao huambatana na radi.
Alama yao ni ardhi nyeupe kuliko theluji.
Umbo lao maalum ni kama Mfalme mwenye ndevu anaemuendesha DRAGON.
Umbo lingine ni la mtu mzee mwenye ndevu
Umbo lingine ni la Bibi kizee ambae anaegemea kitu
Umbo lingine ni la Mvulana
Umbo lingine ni la Dragon
Umbo lingine ni la Bundi (Owl)
Umbo lingine ni la Nguo nyeusi isiyo na mwili
Umbo lingine ni la Ndoano au Mundu
Umbo lingine ni la mti wa Mreteni
2. Majini wa Jupiter (Mushtara) - Majini wa Alhamisi


Majini wa sayari hii wanakuwa na mwili mwekundu na umbo la kati siyo wakubwa wala siyo wadogo, mwendo wao na mwondoko wao ni wa kutisha na wa kuogopesha lakini na wapole na wanao ongea taratibu.


Wana rangi ya chuma ambayo inawaunganisha wao na Sayari ya Mars (Mariikh). Mwendo wao ni ule wa umeme ukiambatana na ngurumo za radi.


Alama yao ni ya mizuka ya watu ambao miili yao ni kama iliyojeruhiwa na Simba.
Umbo lao maalum ni la Mfalme mwenye Upanga akiwa mgongoni mwa Simba akimwendesha.
Umbo lingine ni la Mtu aliyevalia rasmi Nguo za Chuma za Kivita.
Umbo lingine ni la Kijakazi aliyevaa Taji lililopambwa kwa Maua.
Umbo lingine ni la Ng'ombe Dume.
Umbo lingine ni la Paa dume
Umbo lingine ni la Tausi
Umbo lingine ni la Nguo ya rangi ya bluu isiyokua na mwili.
Umbo lingine ni la Upanga.
Umbo lingine ni la Mti wa Mbuyu.
 
3. Majini wa Mars (Mariikh) - Majini wa Jumanne


Majini wa Mars (Mariikh) wanakuwa na Umbo refu, Mwili Mwekundu, mchafu na hutoa harufu yenye kutia kinyaa. Huwa wanajitokeza pia katika mwili wenye rangi Nyekundu, Kahawia au Nyeusi. Wana mapembe kama ya mnyama aitwaye Ayala (Hart), kucha kama za Simba, Wanatoa sauti kama za Nyati (Mbogo).


Mwendo wao ni kama mwendo wa moto unaowaka na Alama yao ni radi na umeme unaowaka kwa katikati.
Umbo lao maalum ni la Mfalme aliyevalia kivita akiwa amempanda Mbweha (Mbwa mwitu).
Umbo lao lingine ni la Mwanamme aliye na silaha.
Umbo lao lingine ni la Mwanamke aliyeshikilia Ngao kwenye mapaja yake.
Umbo lao lingine ni la Mbuzi Jike.
Umbo lao lingine ni la Farasi.
Umbo lao lingine ni la Paa.
Umbo lao lingine ni la Nguo Nyekundu isiyokuwa na mwili.
Umbo lao lingine ni la Sufi.
4. Majini wa Sayari ya Jua (Shams) - Majini wa Jumapili


Majini wa Sayari ya Jua (Shams) wana viungo na umbo la kati, wasiovutia na dhalimu, wana Sura nyekundu na rangi ya dhahabu iliyochanganyikana na Damu.


Mwendo wao ni mfano wa Umeme na Alama yao kubwa ni kusababisha mwenye kumuita kutokwa na jasho jingi (ambapo hii ni kawaida kwa Viumbe hivi ambavyo ni vigumu kuelezeka).


Umbo lao maalum ni la Mfalme aliyebeba fimbo ya kifalme huku akiwa amempanda Simba.
Umbo lao lingine ni la Mfalme aliyevikwa Taji.
Umbo lao lingine ni la Malkia mwenye Fimbo ya Kifalme.
Umbo lao lingine ni la Ndege wa aina yeyote isipokuwa wale ndege ambao wanawakilisha peponi.
Umbo lao lingine ni la Simba.
Umbo lao lingine ni la Jogoo.
Umbo lao lingine ni la Nguo ya Dhahabu isiyokuwa na mwili.
Umbo lao lingine ni la Fimbo ya Kifalme.
Umbo lao lingine la mwisho ambalo kwa kweli ni la kutisha sana; ni lile la Kiumbe ambaye haeleweki eleweki vizuri na ni vigumu kumuelezea ila ana mkia.
5. Majini wa Sayari ya Venus (Zuhura) - Majini wa Ijumaa


Majini wa Sayari ya Venus wana Umbo la kati na ambalo ni zuri kwa kuliangalia ambapo sehemu yao ya juu ni ya dhahabu na sehemu yao ya chini katika mwili ni ya rangi nyeupe au kijani.


Mwendo wao ni kama wa mwendo wa Nyota inayong’aa. Alama yao ni ile inayofanana na Wanawake wanaocheza katikati ya Mduara, huku wakimshawishi na kumtamanisha Mwanamazingaombwe ajiunge nao.

Umbo lao maalum ni:-


Ni la Mfalme aliyebeba Fimbo ya Kifalme huku akiwa anamwendesha Ngamia.
Umbo lao lingine ni la Mwanamke aliye Uchi.
Umbo lao lingine ni la Mbuzi Mwanamke.
Umbo lao lingine ni la Ngamia; ambaye huwakilisha Shetani mbaya aitwae Cazote.
Umbo lao lingine ni la Njiwa.
Umbo lao lingine ni la Nguo isiyokuwa na mwili ya rangi Nyeupe au Kijani.
Umbo lao lingine ni la Mmea uitwao “Savine”.
6. Majini wa Sayari ya Mercury (Attwarid) - Majini wa Jumatano


Majini wa Sayari ya Mercury (Attwarid) mara nyingi hutokea na mwili wa Kati, Baridi, Majimaji, Unyevu nyevu. Kwa ujumla maana yake ni kusema kuwa Majini hawa wa Sayari ya Mercury wanafanana na maumbile ya Mercury (Zebaki).


Muonekano wa Majini hawa ni wa kuridhisha, ni Wachangamfu katika maongezi, wana Umbo la Kibinadamu, na wanaonekana kama Shujaa aliye na silaha.


Mwendo wao ni kama wa Mawingu ya rangi ya Fedha. Alama yao ni kuwa wanasababisha Vitisho, Hofu na Woga kwa mwenye kuwaita.
Umbo lao Maalum ni la Mfalme anaemuendesha Dubu.
Umbo lao lingine ni la Kijana Mzuri wa Kuvutia.
Umbo lao lingine ni la Mwanamke aliyebeba Kijiti cha kukunjia Uzi chenye bonge la uzi.
Umbo lao lingine ni la Mbwa.
Umbo lao lingine ni la Dubu Jike.
Umbo lao lingine ni la Kunguru; Kunguru hawa hutumwa kwenda kusaidia katika Kazi za Kichawi na Kijini kwa Kuchukua Nguo za Ndani za Watu, Soksi, Vijiko, na vitu vingine vidogo dogo kama hivyo. Ndio maana katika aina nyingi za Ndege, Kunguru mara nyingi ndio huchukua vitu vya ajabu ajabu ambavyo ndege wengine hawawezi kuvichukua.
Umbo lao lingine ni la Nguo isiyo na mwili yenye kubadilika badilika rangi.
Umbo lao lingine ni la Fimbo, Rungu, Bakora au Gongo dogo.
7. Majini wa Sayari ya Moon (Qamar) - Majini wa Jumatatu


Majini wa Sayari ya Moon – Mwezi (Qamar) wana Maumbo makubwa, Laini, Tulivu na rangi yao ni kama wingu jeusi.


Muenekano wao ni umbo lililotuna, Vichwa vyao vina upara, Macho yao ni Mekundu na yanatoa Majimaji, Meno yao ni kama ya Nguruwe Mwitu.


Mwendo wao ni kama Dhoruba kubwa Baharini. Alama yao ni ni Mvua kubwa inayonyesha katika Mduara.
Umbo lao Maalum ni:-
Ni la Mtu kama Mfalme anayerusha Mishale huku akiwa anamuendesha Swala Jike.
Umbo lao lingine ni la Kijana Mdogo wa Kiume.
Umbo lao lingine ni la Mwindaji wa Kike mwenye Upinde na Mishale.
Umbo lao lingine ni la Ng’ombe.
Umbo lao lingine ni la Swala Mdogo.
Umbo lao lingine ni la Bata.
Umbo lao lingine ni la Nguo isiyokuwa na Mwili yenye rangi ya Kijani au Fedha.
Umbo lao lingine ni la Mshale.
Umbo lao lingine ni la Kiumbe mwenye Miguu Mingi mfano wa Tandu.
 
SERIKALI YA MAJINI


Majini wana Utawala wao ambao ni Majini Wakuu na Majini wa Kawaida wanaopewa Kazi za kufanya na Wakuu wao, Katika Serikali yao kuna Wakuu wa Serikali, Wakuu wa Majeshi, Wakuu wa Mahakama na wengineo wengi.


Utawala katika Serikali yao umegawanyika katika sehemu Kuu mbili (2);


Utawala katika Ulimwengu wa Kijini.
Utawala katika Ulimwengu huu wetu wa Kibinadamu.
Majini Wakuu kabisa wapo Watatu (3) ambao Majina yao ni;


Lucifer.................ambae ndio Mfalme wao (Emperor),
Beelzebuth.......... ambae ni Mtoto wa Mfalme (Prince),
Astaroth ..............ambae ni Mtawala Mkuu wa Majimbo (Grand Duke).
Hawa Watawala Wakuu kabisa watatu, iwapo Binadamu anataka kuwaita na kuwatumia inambidi atumie njia Maalum;


Mtu anayewaita anatakiwa achore alama zao kwa kutumia Damu yake mwenyewe, au anaweza pia kutumia Damu ya Kobe wa Baharini (Kasa) katika kuandikia.


Iwapo atashindwa haya yote basi anaweza pia kuwaita kwa kuchora alama za Majini hao kwenye Kito cha Ruby au Emarald; kwani vito hivi vinaendana sana na Majini hasa wale wa Ukoo wa Jua, ambao huwa na Busara, wazuri na Marafiki zaidi kuliko aina nyingine ya Majini.


Alama hizi za Majini zinatakiwa zivaliwe na Mtu ambae anataka kuwaita. Ikiwa muitaji ni Mwanamme, anatakiwa aiweke kwenye Mfuko wake wa Kulia na iwapo ni Mwanamke, anatakiwa aiweke katikati ya Matiti yake ikielekea upande wa Kushoto.


Alama hizi zinatakiwa ziandikwe katika siku ya Jumanne saa Kumi na mbili (12) mpaka saa moja asubuhi au saa saba mchana mpaka saa nane kwa majini wote.


Majini hawa watatu wana uwezo wa kufanya mambo yote, na kwa Mtu ambae anawaita hawa anatakiwa aheshimu wale tu ambao watamheshimu kwani Majini hawa Wakuu wanawaheshimu wale tu ambao ni Marafiki wao Wakuu na wa karibu, hivyo mtu anaeamua kuwaita anatakiwa ajihadhari kwa lolote ambalo linaweza kutokea.


Utawala wa hawa umegawanyika baina yao wote kwani kila mmoja ana Wasaidizi wake wakuu Wawili ambao nao huwa wanawatuma Majini wengine kuhusu mambo ambayo Mfalme wao Lucifa ameagiza yafanyike Duniani kote.


Wasaidizi walio chini ya Lucifa ni;


Put Satanachia na


Agaliarept;.............Ambao wanaishi Bara la ULAYA na ASIA.


Wasaidizi walio chini ya Beelzebuth ni;


Tarchimache na


Fleurety...................Ambao wanaishi Bara la AFRIKA.


Wasaidizi walio chini ya Astaroth ni;


Sargatanas na


Nebiros.............Ambao wanaishi Bara la AMERIKA.


Majini katika Serikali yao kulingana na Kazi zao ni kama ifuatavyo;


LUCIFUGE ROFOCALE....ambae ni Waziri Mkuu (Prime Minister)
SATANACHIA.........ambae ni Amiri Jeshi Mkuu (Commander-in-Chief)
AGALIAREPT......ambae ni Kamanda wa Majeshi
FLEURETY.........ambae ni Luteni Jenerali (Lieutenant-General).
SARGATANAS.....ambae ni Brigedia Meja (Brigadier-Major)
NEBIROS....ambae ni Jemedari Mkuu na ni Inspekta Jenerali (Field-Marshal and Inspector-General).
Kama jinsi ilivyoonekana hapa ya kuwa Utawala wao katika Ulimwengu wao wa Kijini umekaa KIJESHI lakini Utawala wao hapa Duniani sio wa Kijeshi kwani;


1. LUCIFUGE ROFOCALE; ana Mamlaka ambayo amepewa na LUCIFA ya kudhibiti Mali na Hazina zote za hapa Duniani.


Wasaidizi wake ni Baal, Agares na Marbas.


2. SATANACHIA ana Mamlaka juu ya Wake, Wanawake, na Wasichana wote ambapo ana uwezo wa kuwafanyia kama jinsi atakavyopenda yeye.


Wasaidizi wake ni Pruslas, Aamon na Barbatos.


3. AGALIAREPT


Ana Mamlaka na Uwezo wa kugundua Siri zote zilizopo katika Mabaraza na Mahakama zote hapa Duniani.


Anavumbua Siri za hali ya juu sana.


Anaamuru Kikosi cha Pili cha Majini wasiopungua 3,000).


Wasaidizi wake ni Buer, Gusoyn, na Botis.


4. FLEURETY


Ana Mamlaka na Nguvu za Kufanya Kazi yeyote Usiku na anasababisha mvua ya Mawe katika sehemu yeyote ile itakayoitajika.


Anaongoza na Kudhibiti Jeshi kubwa la Majini.


Wasaidizi wake ni Bathsin (au Bathim), Pursan, na Eligor.


5. SARGATANAS ana Nguvu na Mamlaka ya;


Kumfanya Mtu yeyote asionekane.


Anasafirisha Mtu yeyote kwenda sehemu yeyote ile.


Kufungua Loki na Kufuli zote Duniani,


Kuonyesha na kuweka wazi mambo yote yanayofanyika ndani ya Nyumba za Watu binafsi.


Anafundisha mbinu zote za Uchungaji wa Wanyama.


Anadhibiti na Kuamuru Vikosi Kadhaa vya Majini wasiopungua 5,000 kwa kila kikosi.


Wasaidizi wake ni Zoray, Valefar na Faraii.
 
6. NEBIROS ana uwezo wa;


Kushurutisha Uovu kwa Mtu yeyote amtakaye.


Ana uwezo wa Kumletea Mtu Fahari Kuu.


Ana uwezo wa Kumuonyesha Mtu vitu Bora kama vile; Madini, Mawe, Mboga, na Wanyama.


Ana uwezo Mkubwa wa Kutabiri vitu vitakavyotokea hapo baadae; kwani Huyu ndiye Mkuu wa Utabiri katika Ulimwengu wa Kijini.


Anazunguka zunguka huko na huko kila sehemu kwa ajili ya Kuangalia, kuchunguza na Kukagua aina zote za Maangamizi.


Wasaidizi wake ni Ayperos, Naberrs na Glassyalabolas.


Kuna Mamilioni ya Majini wengine ambao nao wapo chini ya hao waliotajwa hapo juu na hutumika tu pale inapoonekana ya kuwa kuna Kazi ya kufanya kutoka kwa Wakuu wao, kwani wao hutumiwa na Wakuu wao kama Wafanyakazi au Watumwa.


Hata hivyo kuna Majini Wasaidizi Muhimu Kumi na Saba (17) ambao wao hufanya Kazi kama Mawaziri wa Wale Majini Wakuu Sita (6), Majini hao pamoja na Kazi zao ni kama ifuatavyo;


1. CLAUNECK;


Ana Nguvu na Mamlaka juu ya Vitu na Utajiri,


Anaweza Kuvumbua Hazina iliyofichwa, kwa yeyote atakayeweka Mkataba nae,


Ana uwezo wa Kumzawadia Mtu Utajiri mkubwa kwani yeye anapendwa sana na Lucifer,


Ana uwezo wa kukuletea Pesa kutoka mbali;


Mtii naye atakutii!


2. MUSISIN;


Ana Nguvu juu ya Mabwana Wakuu, anawapa Maelekezo kuhusu yale yanayotokea na kupitishwa katika Serikali zao na za Washirika wao.


3. BECHARD;


Ana Nguvu na Mamlaka juu ya Upepo, Dhoruba (Tufani), Radi, Umeme, Mvua na Mvua ya Mawe, kwa kutumia uchawi wa Chura na Vitu vingine vya namna hii.


4. FRIMOST


Ana uwezo juu ya Wake na Wanawali na ana uwezo wa kukusaidia kuwafurahia.


5. KHIL ....Husababisha Mtetemeko wa Ardhi.


6. MERSILDE: Ana uwezo wa kukusafirisha mara moja sehemu yeyote uitakayo.


7. CLISTHERET: Ana uwezo wa kukugeuzia usiku na mchana kwa kupenda kwako.


8. SIRCHADE: Ana uwezo wa kukuonyesha wewe aina zote zile za wanyama katika umbo lolote lile walilonalo.


9. SEGAL: Ana uwezo wa kukuonyesha dhahiri miujiza yeyote iwe ya kawaida au ya kimazingaombwe.


10. HIEPATCH: Ana uwezo wa kukuletea mtu aliye mbali papo hapo.


11. HUMOTS: Ana uwezo wa kusafirisha aina zote za vitabu kwa starehe yake.


12. FRUCIESSEIERE: Ana uwezo wa kuwafufua wafu.


13. GULAND: Ana uwezo wa kusababisha aina yote ya maradhi.


14. SURGAT: Ana uwezo wa kufungua aina zote za Loki.


15. MORAIL: Ana uwezo wa kufanya vitu vyote Duniani visionekane.


16. FRUTIMIERE: Ana uwezo wa kukupa kila aina ya sherehe.


17. HUICTIIGARA: Ana uwezo wa kusababisha kutembea usingizini na kwa wengine kuwakosesha usingizi kabisa.


Satanachia na Satanisie wanawatawala majini 45 au 50 wanne katika hao ni Surgutthy, Heramael, Trimasel na Sustugriel. Wawili wa hawa ni machifu na waliosalia hawana umuhimu wowote.


Hawa ni Majini watumikao kwa binadamu kwa urahisi na haraka lau ikiwa wanaelewana na anaemuita,


Serguthy ana uwezo juu ya wake za watu na wanawali


Heramael anafundisha elimu ya madawa na anatoa na ujuzi kamili wa magonjwa yote, tiba zake sahihi, anafundisha aina ya mimea yote, sehemu mimea hiyo inapatikana, nyakati nzuri ya kuipata, umuhimu wa mimea hiyo na namna ya kuchanganya mimea hiyo ili kupata dawa sahihi kwa maradhi ya aina yeyote ile.


Trimasel na Sustugriel hawa wawili ni Machifu na wanatoa elimu ya kichawi kwa wale wanaowapenda.


Agalierept na Tarihimal wanamtawala Elelogap, ambae nguvu zake zipo juu ya Maji.


Nebirots Wawili wawatawala Hael na Sergulath.


Hael anatoa maelezo juu ya Usanii wa kuandika kila aina ya Barua, anampa Mtu uwezo wa kuongea mara moja kila aina ya Lugha na anaelezea na kufumbua vitu vyote vya siri.


Sergulath ana uwezo wa Kufundisha Mtu njia mbalimbali za kuvunja pande ambazo hazielewani.


Hawa wana Wasaidizi wao Wanane (8) wenye nguvu


1. Proculo ambae ana uwezo wa kumpatia Mtu usingizi kwa muda wa masaa manane huku akiwa anafahamu yanayotokea usingizini.


2. Haristum ambae anampa Mtu uwezo wa Kupita kwenye Moto bila ya kuungua.


3. Brulefer, ambae ana uwezo wa Kumfanya Mtu apendwe na Wanawake.


4. Pentagnony, ambae anawapa Watu uwezo wa Kutokuonekana (Invisible), pia anapendwa sana na Watawala Wakuu


5. Aglasis, ana uwezo wa Kumsafirisha Mtu kwenda sehemu yeyote ile Duniani.


6. Sidragrosam, anawafanya Wanawake wacheze Uchi.


7. Minoson, ana uwezo wa Kumhakikishia Mtu kushinda katika Michezo yeyote ukiwepo wa Kamari.


8. Bucon ambae ana Uwezo wa kuanzisha Chuki na Wivu kati ya Jinsia mbili (Wanaume na Wanawake).
 
  • Thanks
Reactions: tz1
Kwa Mfano wewe nikikwambia unaweza kufanana na nyani utakubali?au utafurahi? naomba jibu? samahani ikiwa kama nitakukwaza..... jmushi1

Nilidhani "umeniacha" lol!mkuu neno "kulingana" mara nyingi hutumika kama tunazungumzia height ama vitu vinavyoweza kuwa quantified.

Na pia siyo mara zote maneno "kufananisha" na "kulinganisha" yanaweza kusubstitute.Kwa mfano unaweza kusema watu wamefanana lakini huwezi kusema wamelingana ukimaanisha kuwa wamefanana,however wanaweza wakalingana urefu lakini wasiwe wamefanana ie sura.The later inategemea na matumizi yake ndo maana nikatoa mfano wa sura.

Kuhusu nyani,binadamu anafanana na nyani kwa kiasi kikubwa kimaumbile.However binadamu wanaolingana kwa urefu na nyani ni wachache.
 
avatar38074_4.gif



kitab_al-bulhan_-_iblees.jpg
MziziMkavu kati ya hawa yupi ni jini la ukweli,kwa hiyo na jf tuna majini?
Ukiona Mtu akiweka picha inayofanana na majini basi yeye huyo atakuwa ni miongoni mwa hao Majini Mkuu wote hao wawili ni majini picha zake Mkuu. tz1
 
Last edited by a moderator:
avatar38074_4.gif



kitab_al-bulhan_-_iblees.jpg
MziziMkavu kati ya hawa yupi ni jini la ukweli,kwa hiyo na jf tuna majini?
Ukiona Mtu akiweka kwenye Avatar yake picha inayofanana na majini basi yeye huyo atakuwa ni miongoni mwa hao Majini Mkuu wote hao wawili ni majini picha zake Mkuu. tz1 si unaona picha inavyojieleza
 
Last edited by a moderator:
Nilidhani "umeniacha" lol!mkuu neno "kulingana" mara nyingi hutumika kama tunazungumzia height ama vitu vinavyoweza kuwa quantified.

Na pia siyo mara zote maneno "kufananisha" na "kulinganisha" yanaweza kusubstitute.Kwa mfano unaweza kusema watu wamefanana lakini huwezi kusema wamelingana ukimaanisha kuwa wamefanana,however wanaweza wakalingana urefu lakini wasiwe wamefanana ie sura.The later inategemea na matumizi yake ndo maana nikatoa mfano wa sura.

Kuhusu nyani,binadamu anafanana na nyani kwa kiasi kikubwa kimaumbile.However binadamu wanaolingana kwa urefu na nyani ni wachache.
Kwa maelezo yako inaonyesha unaipinga aya ya Mungu katika kitabu cha Biblia inayosema hivi nanukuu
(Mtanifananisha na nani, na kunisawazisha naye, na kunilinganisha naye, ili tuwe sawasawa?) Mungu hapa kasema

maneno ma 3 Kunifananisha na Viumbe wake alivyowaumba kwa mfano Binadamu ,Majini na Malaika. Kuwa sawasawa na Mungu

kamwe Mwenyeezi Mungu hawezi kufanana navyo hivyo viumbe alivyoviumba yeye Mwenyewe Mungu. Neno la pili Mungu kasema hivi

Kunisawazisha Mungu na Viumbe wake huwezi kumsawazisha Mwenyeezi Mungu na Viumbe wake Binadamu ,majini na Malaika kuwa sawa sawa

na aliye viumba yaani Mwenyeezi Mungu. Neno la 3 Mungu amesema hivi Kumlinganisha Mungu na Viumbe vyake

Binadamu ,Majini na Malaika hawawezi kulingana navyo kwa vyovyote vile haiwezikani hata haingii kiakili huwezi kulinganisha Viumbe

aliowaumba Mungu na yeye mwenyewe muumba Mwenyeezi Mungu .Mkuu.. @
jmushi1 jaribu kutumia akili yako alivyosema Mungu katika

Biblia hiyo aya kisha utapata jibu kamili nakuacha hapo.....
 
Nashukuru umetambua ya kuwa Yesu ni BWANA. Na sio wewe tu, hata pepo (japo kwa uwoga) walimtambua Yesu ya kuwa yu mwana wa Mungu.

Lakini Mathayo 27:43 inasema "Amemtegemea Mungu, na amwokoe sasa, kama anamtaka, kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu"

Na pia Mathayo 9:34 Hayo ni mamneno ya Mafarisayo ambao lengo lao ni kupotosha kile kilichotokea. Soma Mathayo 9:32-33 "[SUP]32[/SUP]Hata walipokuwa wanatoka, tazama, walimleta mtu bubu mwenye pepo. [SUP]33[/SUP] Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena, makutano wakastaajabu, wakasema, haijaonekana hivi katika Israeli wakati wowote"
Kwa hiyo utaona kuwa Yesu alitoa pepo, lkn wafarisayo wakakebehi kwa maslahi kama haya yako.

Mimi sijakuelewa unataka kueleza nini kwa hii mistari uliyojaza hapa. Ikiwa umeshasoma na kuamini kuwa Yesu aliwatoa mapepo, basi umeshajua kuwa Yesu si mpunga mapepo. Ameyatoa kwa kuwa hawatoki katika ufalme mmoja. Angekuwa na imani ya mapepo asingewatoa kwani angekuwa anaufitini ufalme wake mwenyewe. Na ndio alijibu maneno ya wafarisayo kuwa anatoa pepo kwa nguvu za pepo.

Unauliza tena Yesu mumuiteje, hakuna jina lingine zaidi ya ulilokwisha sema awali BWANA.
hata wewe pia ni bwana sio tu Yesu peke yake au mwenzetu wewe ni bibi?... Bumpkin Billionare Mimi pia ni bwana Mzizimkavu sio bibi mkuu kuitwa bwana ni heshima hakuna zaidi ya hapo wewe baba yako mzazi unaweza kumuita kwa jina lake pasipo na kutanguliza neno Baba Au mzee? sasa ukimuita Baba au Mzee si unampa tu heshima yake? acha hivyo wewe Bumpkin Billionare
 
Ok, umenena kuwa majini ni viumbe kama sie binadamu ila hawaonekani. Sasa ni nini haswa faida ya hawa majini kwetu sie binaadamu?
Majini wana faida kwa wale wanayoyafuga kuna binadamu wanayo yafuga hayo majini kulinda mali isiibiwe kuna yanayofanya kazi na Waganga wa kienyeji, kuna yanayofanya kazi na watu Matajiri duniani, Kuna majini yanayofanya kazi na Ma Rais wa Dunia FreeMason majini yana faida nyingi kwa binadamu ukiweza kuyatumia mkuu.. nakuacha hapo .. Mkereketwa
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom