Abtali mwerevu
JF-Expert Member
- May 5, 2013
- 638
- 434
Rais wa Zambia, Edgar Lungu amemwomba Mungu kuinusuru nchi yake dhidi ya kuendelea kuporomoka kwa thamani ya fedha nchini humo, huku mamlaka husika zikichukua hatua zaidi kukabiliana na halihiyo.
Serikali ya nchi hiyo imetangaza kufungwa kwa kumbi zote za burudani huku mechi zote za mpira zikiahirishwa kupisha siku maalumu ya kuliombea taifa.
Kiongozi huyo alitangaza hatua hiyo wiki iliyopita baada ya thamani ya fedha kuanguka kwa asilimia 45 dhidi ya Dola ya Marekani. Hali hiyo ilisemekana kuchangiwa na kuanguka kwa bei ya madini ya shaba ambayo ni tegemeo lake kuu la kiuchumi.
Bei za vyakula pia zimepanda pia uzalishaji wa umeme umepungua kutokana na kiwango kidogo cha maji katika Ziwa Kariba. Ziwa hilo linategemewa kwa uzalishaji wa umeme.
Hitimisho. Sasa kwa kiongozi aliyetayari hata kukopa ili watu wasome bure sijui uchumi utakuaje?
Serikali ya nchi hiyo imetangaza kufungwa kwa kumbi zote za burudani huku mechi zote za mpira zikiahirishwa kupisha siku maalumu ya kuliombea taifa.
Kiongozi huyo alitangaza hatua hiyo wiki iliyopita baada ya thamani ya fedha kuanguka kwa asilimia 45 dhidi ya Dola ya Marekani. Hali hiyo ilisemekana kuchangiwa na kuanguka kwa bei ya madini ya shaba ambayo ni tegemeo lake kuu la kiuchumi.
Bei za vyakula pia zimepanda pia uzalishaji wa umeme umepungua kutokana na kiwango kidogo cha maji katika Ziwa Kariba. Ziwa hilo linategemewa kwa uzalishaji wa umeme.
Hitimisho. Sasa kwa kiongozi aliyetayari hata kukopa ili watu wasome bure sijui uchumi utakuaje?