Nimeisikia hotuba ya Lowassa na akadai kwamba hakutendewa haki ya kutokuitwa na kuhojiwa katika tume ya Dr. Mwakyembe
Kumbukumbu zangu kama ziko sahihi wafuatao walifukuzwa kazi na Lowassa mara moja bila kupewa nafasi ya kujieleza (natural justice)
1: Engineer wa Temeke baada ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa
kule temeke. Wana JF mtakumbuka, kijana alitimuliwa kazi on
the spot bila nafasi ya kujieleza nini kilitokea
2:Mkurugenzi wa wilaya ya Same,wakati wa mahindi ya msaada
wakati wa njaa. Mkurugenzi huyo alisimamishwa au kufukuzwa
kazi on the spot bila kupewa nafasi yeyote ya kujieleza na
Lowassa.
Swali: Ina maana Lowasa wakati huo alikuwa hajui maana ya
NATURAL JUSTICE? Sipati majibu kamili
Si hao tu
Ongeza na mwanasheria wa TANESCO aliyetoa amri afukuzwe mara moja lakini ikagonga mwamba, jamaa akasevu