Elections 2010 Hatari ya wapambe wa wagombea ubunge kuwakosesha wagombea wao kura

Jethro

JF-Expert Member
Mar 23, 2009
2,219
370
Wana JF,

Leo katika pita pita yangu nilikuwa kwenye msiba wa baba ya rafiki yangu na nikawa pembeni na wananchi walio hudhuria mazishi na mara ghafla wakapita wagombea wote wa jimbo hilo kwenda kutoa pole.

Hapo nilipo kuwa na vijana wenzangu kumbe kulikuwa na wanachama wa vyama tofauti na itikadi zao na pakaja mzozo wa kubishana mgombea huyu atatufanya nini na yule atatufanyia nini na mbaya zaidi wapambe wa mgombea mmoja(A) akatoa kashfa kuwa mgombea (B) wenu ni tapeli tuu hapa mjini mara hiki mara kile na huyu mwingine mpambe wa mgombea (B) akatoa kashfa na akasema neno zito kidogo na lika mghafirisha mpambe wa mgombea(A) aliyeanza kutoa kashfa na mbaya zaidi ni wa chama tawala na akaanza kutoa vitisho vikubwa kwa huyo mpambe wa mgombea (B) ooh ngoja tukishinda utao ni kuwa weka ndani wete(esp watako mpinga mgombea (A)) na Huyo mpambe wa mgombea B tukamwambia we choropoka nenda sie tutasawazisha hii hali hapa na kweli yaka isha ila kwa jinsi nilivyo ona huyo mpambe wa mgombea A lazima atamfuatilia huyo mpambe wa B kwani anamfahamu fika.

Sasa nashindwa fahamu na kujiuliza tabaka lile ambalo tulilo hofia litakuja la udini au ukabila sasa kumbe sio na litakuwepo tabaka la wewe ni chama fulani kwa chama fulani hii itakuwa mbaya sana na kwa kuangalia tuu baaada ya uchaguzi mgombea yeyote atakae shinda ndie kiongozi ya hawa wote wanachama na ndio wananchi.

Nina shaka ya kutokea malipizano ya vyama. Na hili NEC/POLICE(idala ya Upelelezi) waliangalie sana. kwa kuona mabadiliko yanakuja na watu wanajaribu kutishiana mgombea wangu anafa na mwingine anasema huyu hafai ila haya yote twatakiwa kubishana kwa sera na si kwa ubabe ati kwa kuwa wewe hapo mjini ni aruhatani na wamtishia mwenzio mpaka anakosa uhuru ndani jimbo lako na ndani ya nchi yenu nyote?? Hii ni njaaaaa au hizo pesa za wagombea mpewazo au??

Mtawaalibia wagombea wenu kura na kuleta vurugu baina yenu na sio ya udini wala ukabila.

Twatakiwa kubisha kidemocrasia na sio vitu vya upuuzi tuuuu. na kama twabishania democrasia hatuwezi tishiana maisha hata kidogo.
 
hILI NI TATIZO KATIKA UONGOZI WA kITAIFA TUNAPASWA KUMUOMBA NA KUWAHIMIZA VIONGOZI WA KITAIFA WATOE KAULI ZITAKAZOSIMAMIWA NA KUTEKELEZWA. WANAPOTOA KAULI HIZO WAZITOE WAKIMAANISHA NA WAKITAZAMWA USONI IONEKANE WANAMAANISHA
 
Back
Top Bottom